KERO Jiji la Dodoma lina changamoto ya upatikanaji wa maji ya uhakika

KERO Jiji la Dodoma lina changamoto ya upatikanaji wa maji ya uhakika

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Revolution

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2008
Posts
960
Reaction score
927
Dodoma ni Jiji linalokuwa kwa kasi sana na ni Mji wa Kiserikali kama ilivyo kwa Lagos, Nigeria na Pretoria, Afrika Kusini.

Kero mojawapo kubwa ambayo inakera kweli kweli ni kutopatikana kwa maji ya uhakika. Maji Dodoma kwa baadhi ya maeneo ni nadra sana kupatikana.

Rai yangu ni kuwa Serikali chini ya Kiongozi wetu mpendwa na mpenda maendeleo Mh. Dkt Samia, itatue hii kero mara moja na kwa haraka ili kulifanya Jiji hili kuwa ni mji wa kisasa wa Serikali wenye hadhi kama majiji mengine.

Serikali inashindwa nini kuvuta maji kutoka Mtera? Au Mto Wami na kuyaleta hapa kuliko kutegemea maji ya visima?

Population inaongezeka kwa kasi lakini upatikanaji na usambazaji wa maji haundani na ongezeko la watu. Mfano eneo la AREA D ambapo kuna viongozi wengi kuna shida ya maji sana, swaswa, Meliwa na Kisasa ni tabu kweli kweli.

Ni ipi kero nyingine unayokumbana nayo hapa Dodoma?
 
Dodoma kwanza imekuwa jiji by Force
Baada ya forced labour kuondoka imebaki jina tu
 
Dodoma ni Kijiji siyo jiji. Mleta amafa kuwa makini sana.
 
Dodoma kwanza imekuwa jiji by Force
Baada ya forced labour kuondoka imebaki jina tu
Na dodoma itaishia hapo hapo, nashangaa watu wanao wekeza pesa ndefu dodoma kwa matumaini ya ukuaji badaye.......JPM aliansisha jiji bila plan and bajeti.
 
Na dodoma itaishia hapo hapo, nashangaa watu wanao wekeza pesa ndefu dodoma kwa matumaini ya ukuaji badaye.......JPM aliansisha jiji bila plan and bajeti.
Kila kitu kina mwanzo. Dar inajaa hii na watu wengi wanaichoka
 
Mmh hatutaki aje na stori zake za watu kububujike na machozi ya furaha wakiona dodoma anavo endelea kwa utawaka utakatifu wa raisi ......lakini huyu jama ni chawa kweli kweli
We Lucas Mwashambwa usinipe "like" yako uchawa wako siupendi mwanaume gani unasifia mwanaume mwenzio kama demu loh
 
Moja kati ya hasara kubwa aliyolisababishia taifa ni kuhamishia shughuli zote za serikali Dodoma.

JPM aliwaza nini?

Dodoma ni Jangwani na ili kuiwezesha kuwa na huduma toshelevu inahitajika pesa nyingi Sana Sana .

Hakufanya kabisa utafit,, inshort ulikuwa mkurupuko.
 
Kila kitu kina mwanzo. Dar inajaa hii na watu wengi wanaichoka
Wewe unajua Dar inazaidi ya miaka 100. Mwanza miaka 70 dodoma ndo uitegemea baada ya miaka 10 tu......
 
Hakika shida ya maji Dodoma inazidi kukua, maeneo ya Nkuhungu na Ndachi siku ya Jana na leo kuna vijiwe vingi vya watu wameweka foleni kusubiri maji ya kununua.
 
Maji yapo mtera ya uhakika. Km kama 150 hadi dodoma.
 
Back
Top Bottom