Jiji la Nairobi lakumbwa na mafuriko makubwa hivyo kutatiza watu kufika kazini na magari kukwama

Jiji la Nairobi lakumbwa na mafuriko makubwa hivyo kutatiza watu kufika kazini na magari kukwama

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
FB_IMG_1521111091763.jpeg
FB_IMG_1521109234981.jpeg
FB_IMG_1521109217624.jpeg
Mvua kubwa iliyonyesha Alhamisi asubuhi imesababisha mafuriko makubwa jijini Nairobi nchini Kenya, na kutatiza watu kufika kazini na magari kukwama.

Mvua hiyo iliyoanza saa 12 asubuhi pia imesababisha msongamano mkubwa wa magari huku watu wakilazimika kupita juu ya maji.

Maji yameshuhudiwa yakielekea katika ya barabara nyingi za katikati ya jiji hilo kubwa la Afrika Mashariki, mafuriko ambayo wakazi wanasema hayajawahi kushuhudiwa katika miaka ya hivi karibuni.

Barabara zilizoathiriwa na mafuriko hayo ni pamoja na Moi Avenue, Tom Mboya, Racecourse, Ronald Ngala, Haile Selassie Avenue, Temple Road na barabara ya Kimathi.

Barabara kuu ya kwenda mji wa pili kwa ukubwa Mombasa pia imeathiriwa na mvua hiyo na kujaa maji.

Mvua kubwa imekuwa ikinyesha nchini Kenya katika siku za hivi karibuni huku mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa nchini humo ikionya kuwa mvua kubwa itaendelea kushuhudiwa katika siku zijazo.

Wito umetolewa kwa watu katika maeneo ambayo kuna mafuriko, kwenda katika maeneo yaliyoinuka, kuepuka maafa zaidi.
 

Attachments

  • FB_IMG_1521109234981.jpeg
    FB_IMG_1521109234981.jpeg
    28.9 KB · Views: 37
Kipindi cha mvua kuwe na likizo tu kwa wafanyakazi maana wanapoteza muda mwingi kwenda kazini
 
Back
Top Bottom