Uchaguzi 2020 Jimbo la Singida Magaribi CCM tunaweza kulipoteza kwenda CHADEMA 2020

Uchaguzi 2020 Jimbo la Singida Magaribi CCM tunaweza kulipoteza kwenda CHADEMA 2020

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Naomba nilizungumze hili kwa moyo wa dhati kabisa na kwa mapenzi makubwa kabisa ya chama changu. Bado tunaamini kwamba chama chetu hakijapata mbadala wake na bado hakuna dalili hizo kwa maneno ya mzee wangu makamu mkuu wa chuo cha UDSM Prof Mukandara.

CCM chama changu pendwa, kuna malalamiko makubwa sana ya wananchi na wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya ya Ikungi kwamba aliyekua Mbunge wa jimbi hilo ndugu Elibariki Kingu anagawa rushwa kwa kila mjumbe hivi sasa ili aweze kupigiwa kura za kishindo. Haya si maneno yangu ni ya wajumbe wenyewe na mkitaka kujua fanyeni uchunguzi muone ukweli ulivyo. Mtu huyu anasaidiwa kufanya kazi hii na mwenyekiti kiti wa Wilaya ndugu Mika Likapakapa. Wananchi wana hasira sana na vitendo hivi na kiukweli kabisa wameapa kupiga kura za hasira kwa upinzani ili kumkomesha kwa vile hawamtaki kabisa.

Nayazungumza haya siyo kwa nia mbaya bali ni kwa maslahi mapana ya chama changu, jimbo na taifa kwa ujumla.Sina chuki yeyote wala hiyana na mbunge huyu mstaafu ila amefanya chama kichukiwe sana na wananchi kutokana na kutotimiza ahadi zake zote za mwaka 2015 alizotoa wakati wa kampeni. Kuna shida kubwa ya Maji, Umeme, miundombinu, Afya na Elimu ambapo mashule mengi madarasa hayana madawati jimboni humo. Twafahamu kua yeye hawezi kujenga kwa pesa zake mwenyewe, basi awsemee wananchi hawa ili serikali iwaonee huruma. Yeye amekua akisemwa kua siyo mkweli muda wote anatoa ahadi hewa.

Inasemekana vyama vya upinzani jimboni humo vinategea arudishwe na chama wataungana kwa kuweka mtu mwenye nguvu anayependwa na watu wengi waweze kumuondoa. Hili linawezekana kabisa chonde chonde chama changu nakipinda tusifanye kosa tunaangalia kwa macho.

Inasemekana pia ikiwa kweli Tundu Lisu atagombea Urais mwaka huu upepo wake unaweza kubadilika na tukapoteza majimbo yote mawili ya Magharibi na mashariki. Jimbo la Mashariki wananchi wanadai kua Mbunge aliyepo sasa ndugu Miraji Mtaturu hana mvuto wa kisiasa na pia hamudu majukwaa ya kisiasa vizuri. Huko pia tukiwekewa na upinzani mtu mwenye nguvu anayejua kusema vizuri tunaweza kupoteza jimbo kwa mara ya tatu sasa. Inasemekana naye anagawa rushwa kwa kiasi kikubwa sana kujihakikishia ushindi kwenye kura za maoni.

USHAURI WANGU
Haya yote yanafanyika kwa sababu ya udhaifu na uzembe wa Mwenyekiti wa Wilaya ndugu Mika Likapakapa. Ndiye inasemekana anasuka mipango yote ya rushwa na haelewani kabisa na timu ya viongozi wengine wa Wilaya.Menyekiti huyu aondolewe kwenye nafasi yake na ikaimishwe. Tutakuja kukumbuka maneno yangu haya huu ushauri ni kwa nia njema kabisa kwa chama changu. Tumelalamikia mitendo hivi ngazi mbali mbali za chama kuanzia mkoa hadi taifa tunaona kimya tu. Tusije tukajutia na atutaki kujutia kwa hili wakati tunaangalia na twajua
 
Wanyiramba nanyie mkishanunuliwa nyama na pombe za kienyeji mnachagua mtu na kusahau shida zenu zote.
 
Ccm na rushwa ukiviachanisha ni sawa na kichaa aingie ICU awachomulee wagonjwa mipira ya kusaidia kupumua...
 
watoa rushwa wote taarifa zao zipo,hawatapita ndani ya chama.
 
Naomba nilizungumze hili kwa moyo wa dhati kabisa na kwa mapenzi makubwa kabisa ya chama changu. Bado tunaamini kwamba chama chetu hakijapata mbadala wake na bado hakuna dalili hizo kwa maneno ya mzee wangu makamu mkuu wa chuo cha UDSM Prof Mukandara.

CCM chama changu pendwa, kuna malalamiko makubwa sana ya wananchi na wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya ya Ikungi kwamba aliyekua Mbunge wa jimbi hilo ndugu Elibariki Kingu anagawa rushwa kwa kila mjumbe hivi sasa ili aweze kupigiwa kura za kishindo. Haya si maneno yangu ni ya wajumbe wenyewe na mkitaka kujua fanyeni uchunguzi muone ukweli ulivyo. Mtu huyu anasaidiwa kufanya kazi hii na mwenyekiti kiti wa Wilaya ndugu Mika Likapakapa. Wananchi wana hasira sana na vitendo hivi na kiukweli kabisa wameapa kupiga kura za hasira kwa upinzani ili kumkomesha kwa vile hawamtaki kabisa.

Nayazungumza haya siyo kwa nia mbaya bali ni kwa maslahi mapana ya chama changu, jimbo na taifa kwa ujumla.Sina chuki yeyote wala hiyana na mbunge huyu mstaafu ila amefanya chama kichukiwe sana na wananchi kutokana na kutotimiza ahadi zake zote za mwaka 2015 alizotoa wakati wa kampeni. Kuna shida kubwa ya Maji, Umeme, miundombinu, Afya na Elimu ambapo mashule mengi madarasa hayana madawati jimboni humo. Twafahamu kua yeye hawezi kujenga kwa pesa zake mwenyewe, basi awsemee wananchi hawa ili serikali iwaonee huruma. Yeye amekua akisemwa kua siyo mkweli muda wote anatoa ahadi hewa.

Inasemekana vyama vya upinzani jimboni humo vinategea arudishwe na chama wataungana kwa kuweka mtu mwenye nguvu anayependwa na watu wengi waweze kumuondoa. Hili linawezekana kabisa chonde chonde chama changu nakipinda tusifanye kosa tunaangalia kwa macho.

Inasemekana pia ikiwa kweli Tundu Lisu atagombea Urais mwaka huu upepo wake unaweza kubadilika na tukapoteza majimbo yote mawili ya Magharibi na mashariki. Jimbo la Mashariki wananchi wanadai kua Mbunge aliyepo sasa ndugu Miraji Mtaturu hana mvuto wa kisiasa na pia hamudu majukwaa ya kisiasa vizuri. Huko pia tukiwekewa na upinzani mtu mwenye nguvu anayejua kusema vizuri tunaweza kupoteza jimbo kwa mara ya tatu sasa. Inasemekana naye anagawa rushwa kwa kiasi kikubwa sana kujihakikishia ushindi kwenye kura za maoni.

USHAURI WANGU
Haya yote yanafanyika kwa sababu ya udhaifu na uzembe wa Mwenyekiti wa Wilaya ndugu Mika Likapakapa. Ndiye inasemekana anasuka mipango yote ya rushwa na haelewani kabisa na timu ya viongozi wengine wa Wilaya.Menyekiti huyu aondolewe kwenye nafasi yake na ikaimishwe. Tutakuja kukumbuka maneno yangu haya huu ushauri ni kwa nia njema kabisa kwa chama changu. Tumelalamikia mitendo hivi ngazi mbali mbali za chama kuanzia mkoa hadi taifa tunaona kimya tu. Tusije tukajutia na atutaki kujutia kwa hili wakati tunaangalia na twajua
Du CCM mnaiogopa CDM mpaka mnatetemeka kabisa. Mimi nafurahi mno ninapoona hivyo na ninawapongeza sana CDM mashujaa wakubwa pamoja na kuteswa vibaya sana na Nduli bado mpo imara na mtatisha wale watu hawalali kabisa. Peopleeeeeeees!....
 
Back
Top Bottom