KERO Jimbo la Ubungo la Kitila Mkumbo ni miezi 3 watu hawayajui maji

KERO Jimbo la Ubungo la Kitila Mkumbo ni miezi 3 watu hawayajui maji

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
9,846
Reaction score
20,319
Na ni waziri wa mipango na uwekezaji, proffesor nzima huyu[emoji22]hivi huwa wanapewa wizara wakati majimboni mwao ni tabu?

Huyu kitila mkumbo ni kama kalitelekeza jimbo lake la Ubungo. Barabara nyingi za ndani zina hali mbaya sana.

Jamaa haonekani jimbon zaidi ya kukikaribia uchaguzi. Kuna maeneo mengine ya kimara, ubungo na Goba watu hawajayaona maji kwa miezi miwili sasa.

Ubungo Kibangu watu wana miezi kibao bila maji mara ya mwisho yalitoka mwezi wa nane wanavyodai.

Makoka wana mwezi hawana maji kabisa na hayajatoka mda

Kajima napo watu hawana maji inadaiwa ni mwaka sasa maji yanatoka mara moja tu kila baada ya miezi 3

Mabibo hostel eneo lile maji yamekua kama Lulu. Maeneo ya kimara baruti pia kuna maeneo maji hayatoki kabisa.

Ubungo kibo ni shida maji hutoka kwa mgao! Huku Goba ndo usiseme sijui nianzie wapi maji yamekua ni anasa kwa maeneo mengi.

Halafu jamaa ni waziri, kuna uzi niliona humu mtu analalamika ubungo kibangu kajima wana miezi 6 bila maji, huku Goba maeneo mengi ni shida tupu!!

Bado sijasemea maeneo mengine ya hili jimbo lake, najiuliza kwanini tatizo sugu la maji Dar es salaam ni jimboni kwa Kitila tu ndo pana matatizo kuzidi popote?

Jimboni kwa kitila biashara ya maji kuuzwa dumu 1000 imerudi, juzi nimeona hapa Goba watu wananunua dumu la maji 1000 au uagize gari ya maji nyumbani wakuletee bei inaanzia elfu 60 kwa tank la lita 3000 ambazo ni ndoo 150 means ndoo unauziwa 400 ukiagiza lile gari la Maji

#Shame on you Kitila Mkumbo, nitashangaa sana wananchi wenzangu wa Goba na Ubungo mkipigia kura huyu mtu tena au kuchagua maccm kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa its shame and disgusting
 
Mbona ni sehemu nyingi tu Dar maji ni shida waziri ametoa maelekezo Dawasa hawatekelezi wanamdharau waziri.
 
Phd holder wa mchongo.. His time is giving him farewell
 
Kwani serikali haiwezi kutafuta wawekezaji wa nje wasimamie dawasa kama ilivyo kwenye miradi mingine? At least iwe kwa dar na pwani tu. Tunateseka hasa hii makuburi
 
Back
Top Bottom