Jina linalotumiwa na makabila mengine Afrika Mashariki

Jina linalotumiwa na makabila mengine Afrika Mashariki

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
18,037
Reaction score
33,681
Barani Afrika unaweza kujua kabila la mtu fulani kwa kuzingatia jina lake la ukoo. Mfano; Massawe ( Mchaga ), Mulokozi ( Muhaya ), Pazi ( Mzaramo ), Masanja ( Msukuma ), Mwaikimba ( Mnyakyusa ), Mwita ( Mkurya ), Onyango ( Mjaluo ), Mhina ( Msambaa ) , Ngonyani ( Mngoni ) na Mollel ( Mmasai ) kwa kutaja machache. Lakini uchunguzi wangu binafsi umeniwezesha kugundua kwa llipo jina moja la ukoo ambalo hutumiwa na zaidi ya makabila matano ya Afrika Mashariki , kusini na kati . Jina hilo ni " MBOGO ". Jina hili hutumiwa na :1. WANYAMWEZI .WASUKUMA wa MWASHITA ( Mwanza, Shinyanga Tabora ), 2. WANYATURU wa SINGIDA, 3. WANGONI wa RUVUMA 4. WAKURYA wa MARA. 5. Wazaramo wa Pwani 6. Wabondei wa Muheza na WAKIKUYU wa Nairobi Kenya... Hayo ni makabila ninayo yafahamu, inawezekana yapo makabila mengine yanayo tumia jina hili.. Jina hili lina maanisha kitu gani cha maana sana hadi kutumiwa na watu kutoka makabila mengi kiasi hiki?. Tujuzane waungwana.







" Ukisikia ndugu yako yuko polisi Chang'ombe, fanya mpango umtoe kabla hajafika ngome "
 
pia Mbogo hutumiwa na na watu wa Kilimanjaro sina uhakika kama ni wapale au la,ila ni jambo la kawaida kwa majina kutumiwa na makabila mbalimbali kwa sababu ukichinguza sana asili ya makabila yetu ni moja ,mfano jina la Mgaya hutumiwa na wabena na wazigua,pia jina la Msigwa hutumiwa na wabena,wawanji na waha.

Pia jina la Tembo au Matembo hutumiwa na wangoni na baadhi ya makabila ya Zimbabwe.
 
Ni majina tu ndugu wala hakuna la zaidi.
 
Anyway,ukishajua asili ya majina,hili halitakupa shida.Huko nyuma kabla ya haya mambo ya kujifanya wazungu/wasomi ilikuwa kawaida kuitana majina ya asili.Kutokana na utamaduni wetu wa kuoana makabila tofauti ilikuwa lazima majina kuingiliana.Chukulia mfano kama wewe ni mkuria umemuoa mnyamwezi halitakuwa jambo la ajabu kukuta jina la Kalunde miongoni mwa watoto wako.Ikiwa Mmakua au Mnyakyusa wataoa unyamwezini nao watazaa jina kama hilo.Sasa kama muingiliano huo utaongezeka lazima hilo jina litaonekana ktk makabila mengi tofauti.Lakini pamoja na hivyo,hii haiondoi mantiki ya uasilia wa jina fulani.Kalunde litabaki kuwa ni jina la kinyamwezi japo linaonekana ktk makabila mengine.

Kwa upande mwingine,majina yetu ya kiasili mengi ni ya kibantu.Historia ya majina yetu ya kibantu inaonesha kuwa majina yanakuwa na tafsiri zake;na mara nyingi tafsiri hizo zinafanana kati ya kabila moja na lingine.Kwa mfano Mrimi (usijali sana ID yangu!) ni jina la kibantu na lina tafsiri ya mkulima.Jina hili linatumika ktk makabila zaidi ya manne hapa nchini tena likiwa na tafsiri moja;ingawa kunaweza kuwepo tofauti katika utamkwaji lakini bado linaendelea kuwa ni jina moja na tafsiri moja.Kwa hiyo si jambo la ajabu sana kukuta mambo kama haya.
 
Huku Malawi wanawaita watanzania "a Taifa" na wanopoongea kiingereza husema "the Taifas"
 
Back
Top Bottom