Jino bado linasumbua pamoja na kuelekezwa dawa humu jf!

Mwamgunda

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
247
Reaction score
48
Poleni na majukumu wapendwa! Wiki iliyopita niliandka thread hapa kuomba ushauri juu ya tatizo la kusumbuliwa na jino. Nilipewa ushauri na Mzizi Mkavu juu ya kukinga mkojo wangu na kusukutua kila niamkapo asubuhi kabla cjapiga mswaki na kukaa dk 10 ndo nipge mswaki, kimsingi nilipiga moyo konde na kufuata ushauri huo japo kiukweli yataka uwe na roho ngumu. Lakini mpaka sasa bado maumivu yapo palepale wapendwa, kiukweli nateseka na kung'oa nahisi ntakuwa kibogoyo ktk umri mdg kwani hapa nilipo nina miaka 25 nishang'oa meno 7. Je, kuna njia nyingne mbadala? Msaada tafadhalini ndg zangu, na mungu awabariki na kuwaongoza ktk kila jambo!
 
Pole sana ndugu yangu mtu akisema anasumbuliwa na meno najua anamaanisha nini maana mimi ni mhanga pia.

Mtafute mtu mmoja anaitwa Dr. Sebbo yupo maeneo ya Mbezi ana dawa nzuri sana ya mitishamba. huyu bwana yeye mwenyewe ni muhanga wa meno ukionana nae kitu cha kwanza ni kukuonesha meno yake ambayo nina uhakika ya kwako yana nafuu na hiyo dawa imemsaidia sana. mimi nilielekezwa kwake na jamaa mmoja ambaye mkewe alikuwa na matatizo makubwa ya meno na baada ya kutumia dawa ya huyu bwana maumivu yamemwisha kabisa. Hata mimi imenisaidia kwa asilimia 95, nilikuwa nimefikia pabaya sana.

Nakushauri umtafute huyu bwana namba zake ni 0714 865 146/ 0767 865 145 mwambie umepata namba zake kwa mtu aliyemuuzia dawa zake anaishi Mikocheni atakuelewa.
 
Nitafute kwa namba hii 0769142586, kuna dawa moja imetengenezwa kwa mitishamba mingi nimeitumia kama wiki 2 zilizopita imeponya kabisa maumivu ya jino langu mpaka sifikirii tena kuja kung'oa. Ninauhakika itakusaidia pia.

 
Pole sana Mkuu.@Mwamgunda Jaribu kutumia dawa hii ya Jino kuuma.

MATAYARISHO

Chukua majani ya Mtunda(Muarubaini),majani ya Mpera na Magome ya Muembe.Tia kwenye sufuria kisha

chemsha kwa maji yaliyo safi kwa muda wa dakika 15 hadi 20.

Kisha chukua Dafu kubwa lenye nyama, likate sehemu ya juu kwa lengo la kutengeneza mlango

mdogo.Yatoe maji yote ya dafu kwa vile hayahitajiki na bakisha nyama tu.

MATUMIZI

Chukua maji yako ya dawa yaliyo moto na mimina kwenye dafu kiasi kwamba yakaribie kujaa.Kisha weka

mdomo wako juu ya mdomo wa dafu kwa lengo la kuingiza mvuke wa dawa kwenye mdomo.Weka kisha

ondosha kulingana na umoto wa maji ya dawa kwa muda wa dakika 3 hadi 5.

Kisha sukutua kwa maji ya dawa ambayo yameshapungua joto.

Endelea na zoezi hili asubuhi,mchana na jioni kwa muda wa siku tatu na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu

utapona. Ukisha maliza kutumia uje hapa utupe Feedback.
 
Kama haujawahi kumwona dentist, tafadhali fanya hivyo mapema. Kusukutua kwa mkojo au ushauri wowote hapa kwa case yako ni kupoteza muda.
 
Kama haujawahi kumwona dentist, tafadhali fanya hivyo mapema. Kusukutua kwa mkojo au ushauri wowote hapa kwa case yako ni kupoteza muda.

May be ina sinus or heart problem .Nenda kwa Dr usije pata infection .pole sana
 
Jina linaweza kutibiwa bila kuliondoa. Daktari wa meno anaweza kutumia njia ya kuiua ile nerve iliyopo kwenye jino na kuziba-nafikiri inaitwa root canal. Mimi nilifanyiwa hiyo procedure belgium 1996 na mpaka leo sina tatizo tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…