Uchaguzi 2020 Jinsi Mpiga Kura anavyoweza kutambua Kituo chake cha Kupigia Kura

Uchaguzi 2020 Jinsi Mpiga Kura anavyoweza kutambua Kituo chake cha Kupigia Kura

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
3rg.png

Orodha ya wapiga kura kwa kila kituo itabandikwa siku nane (8) kabla ya Siku ya Uchaguzi ili wapiga kura walioandikishwa wapate fursa ya kutambua vituo watakavyopigia kura.

Vilevile, Tume imeandaa utaratibu utakaomuwezesha mpiga kura kukagua taarifa zake zilizomo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kutambua kituo atakachopigia kura. Mpiga kura anaweza kujua kituo chake cha kupigia kura kwa kufuata utaratibu ufuatao:-

1. Kuhakiki kwa kutumia mfumo wa Voters’ Interaction System (VIS) ambapo mpiga kura atafanya yafuatayo:-

(i) Atabofya namba *152*00#.
(ii) Atachagua namba 9 (Uchaguzi Mkuu).
(iii) Atachagua namba 1 (Uhakiki wa taarifa za mpiga kura).
(iv) Ataingiza namba ya kadi ya mpiga kura bila kuweka herufi “T” wala alama “- “.
(v) Ataona ujumbe unaosomeka “ombi lako limepokelewa na linashughulikiwa, utajulishwa kwa ujumbe mfupi (SMS) hivi punde”.
(vi) Atapokea ujumbe mfupi utakaonesha taarifa zake na kituo cha kupigia kura.

2. Kuhakiki kwa kupitia kituo cha huduma kwa wapiga kura (Call Centre) ambapo wapiga kura watapaswa kupiga simu Na. 0800112100 na kupata usaidizi wa kuhakiki taarifa zao.

3. Kuhakiki kwa kutumia tovuti ya Tume ambayo ni www.nec.go.tz ambapo mpiga kura atafanya yafuatayo:-

(i) Ataona sehemu iliyoandikwa”Uhakiki”.
(ii) Atabofya sehemu iliyoandikwa “mfumo wa uhakiki taarifa za mpiga kura”.
(iii) Itatokea sehemu iliyoandikwa ingiza namba ya mpiga kura na ataingiza namba yake kama ilivyoandikwa kwenye kadi ya mpiga kura. Kwa mfano T-1400-0073-149-0.
(iv) Akikamilisha atabofya sehemu iliyoandikwa “tafuta” na taarifa zake zitaonekana.
 
Upvote 6
Kama jina langu haliko ama halipatikani kwenye kituo changu nitafanyaje?? Tume itanisaidia vipi?
 
Inaweza kuwa mtego wa kutumia namba za watu kutengeneza Kura feki ili fulani yule wskumtaka Gwajima apite!

Tume sio huru, time ya hovyo, time imejaa CCM mwanzo Hadi mwisho ,
 
Mniletee Gwajima
Mniletee Gwajimaaa
Mniletee Gwajimaaaaaaaaaaaaaa!
Flyover hoyee
Mvua hoyee
Mafuriko hoyeeee
 
Hii huduma iwe bure Sasa wasijekuwa wanataka kukusanya Kodi, kila ukibonyeza kutaka kuhakiki unakatwa 300
 
Mbona wanachelewa kutuma huo ujumbe sasa au ndo washachukua namba wanaifanyia mipango
 
Nashauri majina yote yawe on line na kituo Cha kupigia kura hii inaweza kua rahis mtu anaingia anaangalia Jimbo lake halipojiandikisha bas mbona hii ndo njia raisi kuliko kuanza kuweka namba ya kadi ya mpiga kura
 
Kwanini tusimalizie na kupiga kura kwa mfumo huo kabisa,

mambo ni mengi muda mchache
 
NEC wangekuwa wanaona umhimu wa wananchi kupiga kura wangekuwa hata na option ya mtu kujihamisha kwenda kituo kilicho karibu angalau hata siku 14 kabla ya uchaguzi ili angalau watu wengi washiriki.
 
NEC wangekuwa wanaona umhimu wa wananchi kupiga kura wangekuwa hata na option ya mtu kujihamisha kwenda kituo kilicho karibu angalau hata siku 14 kabla ya uchaguzi ili angalau watu wengi washiriki.
Fact
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom