Jinsi Nyerere alivopiga chini mpango wa kutaifisha maduka

Jinsi Nyerere alivopiga chini mpango wa kutaifisha maduka

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Unaposoma Bayographia ya Mwalimu iliyotayarishwa na wanazuoni watatu ukurasa wa 125 hadi 126 kuna simulizi fupi ifuatayo

Mwanzoni mwa miaka ya 80 kulikuwa na tatizo la baadhi ya wamiliki wa maduka kuhodhi bidhaa kisha kuja kuziuza baadae kwa bei juu baada ya kuadimika.

Kwa kuliona hili Baraza la Mawaziri wakati huo chini ya uongozi wa Baba wa Taifa wakaazimia watafutie ufumbuzi suala hili.

Basi Waziri wa Kilimo wakati huo hayati Joseph Mungai (ambae hata sie vizazi vya baadae tulimkuta huyu bwana kwenye utawala wa bwana Ben) akatoa wazo kwa wenzake chini ya Mw/kiti baba wa Taifa kwaamba "tutaifishe maduka yote nchini" ili kukomesha hii tabia ya kuhodhi bidhaa madukani.

Tafsiri yake kwamba, maduka yote sasa yangemilikiwa na serikali ili tatizo la kukosekana kwa baadhi ya bidhaa liishe.

Mwalimu Nyerere hakulikubali kwa haraka wazo hili, ingawa wenzake kwenye kabineti almost wote walikuwa wameunga mkono hoja ya Mungai.

Na kwa kuwa Ministers walikuwa wameshakubalii, basi ikasalia uamuzi wa mwisho wa Mwenyekiti Rais J.K.N ambae bado hakukubaliana na wazo hilo kiurahisi.

Itaendelea...
 
Ahsante kwa taarifa. Baada ya hapo ikawaje?
 
Mungai baadae alikuja kuikarabati elimu aliyoitengeneza Jackson Makweta na wenzake ikawa hivi ilivyo sasa. Mpaka michezo walisema ni anasa.
Kuna Taifa gani linaloendeshwa bila kuwa na wanamichezo? Maana kuna kazi ambazo mtu anayeweza kuzifanya ni lazima awe mwana michezo. Na iko hivyo dunia nzima
 
Jeilikuwa ni baada au kabla ya kuwepo kwa RTC? Regional Trading Company? A
 
Mungai baadae alikuja kuikarabati elimu aliyoitengeneza Jackson Makweta na wenzake ikawa hivi ilivyo sasa. Mpaka michezo walisema ni anasa.
Kuna Taifa gani linaloendeshwa bila kuwa na wanamichezo? Maana kuna kazi ambazo mtu anayeweza kuzifanya ni lazima awe mwana michezo. Na iko hivyo dunia nzima
Pamoja alikuwa tajiri mkubwa na maviwanda ya chai kule mufindi na mashule Ila alikuwa Waziri wa hovyo sana ameharibu sana elimu na michezo na akaja ndalichako ndio heea kabisa profesa mjinga kabisa.
 
Pamoja alikuwa tajiri mkubwa na maviwanda ya chai kule mufindi na mashule Ila alikuwa Waziri wa hovyo sana ameharibu sana elimu na michezo na akaja ndalichako ndio heea kabisa profesa mjinga kabisa.
Sijui alikuwa ana agenda gani na Taifa letu. RIP Mungai
 
Nyerere alishaumwa na nyoka kipindi cha kubinafsisha viwanda asingeweza kubinafsisha tena maduka maana anajua matokeo ya ubinafsishaji
 
Back
Top Bottom