Japo nikiri, mie muumini wa ugali mweupeee tena nataka mahindi yalowekwe kwanza. Dona halishuki asilani. Na chapati za atta zinanishinda, nimefanikiwa tu kwa kupenda kutumia brown rice.
Mkuu Brooklyn Maji hayo uliyoyataja kama yamethibitishwa na wataalam kuyatumia kwa kunywa yanafaa kunywa lakini kama wataalam wamesema hayafai kunywa basi usiyanywe na itakuwa jambo la maana maji ya kunywa ukayachemsha kidigo yawe maji ya uvuguvugu kisha ndio unywe itakuwa ni vizuri kiafya.
Wewe unataka nini Zion Daughter
Mkuu UKI unaweza kutumia lakini sio ndio kila siku kula chips au kunywa soda haifai hata kidogo ukitaka kula kila sikuyaani nimeipenda kweli mada hii lakini sasa dah yaani vyote vilivyosemwa havifai mimi ndio muumini wake jamani mbona maisha yanakuwa magumu hivyo? chips ndio nyumbani, soda ndio kabisaa maana huwa situmii pombe nyma choma sasa dah hapo penyewe, ule ugali wa sembe ulinishinda kwa kweli, nilinenepa vibaya nikaonekana kama simtank nikaenda kwa doctor akaniambia dawa pekee ni mazoezi nilianza mazoezi mwaka mzima na nikapunguza kula hayo mavitu nikawa slim kabisa watu wakaanza kusema mngonjwa mwezi huu nimeanza tena kuona uvivu wa mazoezi naona hali inatakiwa kujirudia, dah maisha nayaona magumu kweli aisee
Mkuu Chasha waache washangae kwa sababu hawaujuwi thamani yake huo mkate wa Brown bread mimi ndio chakula changu chaSafi sana Mzizi Mkavu, Mimi kwa sasa nina Miaka Miwili tangia niachane na Soda na mwaka mmoja tangu niache Juice za Makopo na Mabox, Hata Sembe huwa naitumia nikiwa safarini tu tena mara moja moja, Ila nikiwa nyumbani ni Dona kwenda Mbele ingawa watu huwa wananishangaa sana kwa nini nakula Dona, na hata Hotelini mara Nyingi huwa naulizia Dona ingawa ni hoteli chache mno unazo weza kukuta wanapika Dona,
Na hata ishu ya Mikate kwa kweli Mikate myeupe ilisha nishinda siku nyingi sana, na Huwa natumia sana Brown Bread ingawa ni Ghali sana, na ni kikosa bora kula viazi vitamu kuliko kula Mandazi na Chapati,
MKUU TATIZO NI KWAMBA WATANZANIA WENGI WANAAMNI MTU ANAYE KULA MIKATE YA BROWN ANA KISUKARI NA MIMI NISHA ULIZWA MARA NYINGI SANA KAMA NINA KISUKARI AU LA
Mkuu Chasha waache washangae kwa sababu hawaujuwi thamani yake huo mkate wa Brown bread mimi ndio chakula changu cha
kila siku asubuhi hivi sasa nimeuagiza huo mkate wa brown kutoka katika duka wananiletea nimewapigia simu na uwe unakunywa sana maji ya Uvuguvugu asubuhi kabla ya kunywa kitu glasi 2 na ukisha maliza kupiga mswaki unywe tena
maji ya uvuguvugu glasi moja asubuhi kabla ya kula kitu na ukae kama dakika 45 ndio waweza kunywa chai ya asubuhi. Na mchana unywe glasi moja kabla ya kula chakula cha mchana kisha kaa kama saa 1 ndio ule chakula na usiku kabla ya kula kitu kunywa maji ya uvuguvugu glasi1 kisha kaa kama saa
1 kisha ule chakula na usiku wakati wakulala unywe glasi moja maji ya uvuguvugu kisha lala utaona afya yako itakavyokuwa ni nzuri hutawezatena kuumwa ovyoovyo na unaweza kukaa mwaka pasipo na kuumwa na kitu .
Tembelea Thread yangu hii hapa bonyeza https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/365977-muujiza-ya-matibabu-kwa-maji-ya-moto-kunywa-2.html