Jinsi ya kuanza biashara ya mabango

BarakaMaiseli

Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
9
Reaction score
5
Watanzania, napenda kufahamu kuhusu hii biashara ya mabango makubwa kwa ajili ya kutangaza biashara za makampuni mbalimbali. Na, nina interest zaidi na mabango ya ki elekroniki, au niseme ambayo yanatumia umeme na yanakuwa yanaonesha tangazo zaidi ya moja kwa awamu awamu. Kwa mfano, inaweza ikawa ni makampuni matatu yote yanatangaza kwenye bango moja, yanakuwa tu yanapewa muda kama dakika 3 hivi kila moja, baadae mzunguko unajirudia. Sasa maswali yangu ni haya hapa chini (tunaweza kurahisisha kwa kuchukua bango la 1m x 1m, au 1 square meter):
(1) Mchanganuo wa faida kwa hii biashara uko vipi? Kwa wastani, makampuni huwa yanalipa gharama kiasi gani kwa mwezi? Nadhani hii pia inaweza ikawa inategemea na mahali bango lilipo, tufanye assumption kwamba bango lipo eneo lenye watu wengi.
(2) Utaratibu wa kuanzisha biashara ya mabango ukoje? (TANROADS, Halmashauri, na TRA)
(3) Changamoto za hii biashara ni zipi? Naweza ku guess moja kuwa ni suala la nishati ya umeme, kwa vile mabango yatakuwa yanaendeshwa kwa nishati hiyo.
(4) Gharama za uendeshaji wa biashara ni zipi?
(5) Ushindani wa biashara ya mabango ya Electroniki uko vipi kwa sasa Tanzania?
(6) Ni maeneo Tanzania ambayo ni potential na yanayoweza kutoa faida nzuri?
(7) Ni makampuni gani yanayoendesha biashara kama hii Tanzania? (kama ntapata websites zao au contacts ntashukuru)
Ushauri mwingine pia, ambao labda haujagusa hayo maswali, nitashukuru kuupokea. Kuna kiambatanisho kinachoonesha mfano wa bango la Electroniki (kwa Dar es Salaam, kule Posta kuna mabango flani yanakuwa yanabadilisha matangazo kila baada ya muda; au pale opposite na mlimani city oilcom kuna moja linalotumia LED)
Ahsanteni sana.
 

Attachments

  • IMG-20161126-WA0005.jpg
    10.8 KB · Views: 138
Duh hii biashara ina sheria kibao mtu wangu, sikukatishi tamaa cha msingi sajili kampuni kwanza, nenda TRA na upate leseni ya biashara baada ya hapo mahitaji yatakayokuwa yamebakia madogo sana. Kama matangazo yatakuwa Digital ka yenyewe kuna sheria zake. Kila lakheri
 
Ahsante sana kwa maoni
 
wasikukatishe tamaa hili ni biashara nzuri na haina vizingiti vingi kama wanavyosema.

miongoni mwa kampuni kubwa hapa tz za namna hii ni a1 outdoor,pro24 na a town masters.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…