Jinsi ya kuendelea kuwa maskini

Husna Muba

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2017
Posts
14,524
Reaction score
44,577
1.Usiamke mapema.
2. Usipange matumizi ya Pesa zako.
3. Usiweke akiba mpaka utakapo-kuwa tajiri.
4. Chagua kazi. Mimi nimesoma siwezi kufanya hii kazi.
5. Usifikirie kuanzisha biashara mpaka malaika akishuka kutoka mbinguni na kukukabidhi mtaji.
6. Endelea kuilahumu serikali na wazazi ambao hawakukupa Elimu.
7. Tumia Pesa nyingi kuliko kipato chako.
8. Hakikisha unaenda na fashion. Kila toleo jipya la nguo, viatu, simu lazima na wewe ununue.
9. Wanunulie watoto wako chochote watakacho kuomba.
10. Endelea kutumia muda mwingi zaidi kwenye social networks. Kama Whatsapp, Facebook na Instagram.
 
Nakubaliana kabisa na huu "uzi" wako, lakini hebu nikuulize, hivi "utajiri" ni nini hasa?? Hivi kuwa tajiri hapa duniani ni muhimu sana kuliko kitu chochote kile, au kuna vitu muhimu vya kufanya kuliko kuutafuta utajiri???
 
Huu uzi umeuweka sehemu stahiki.
 
Daaaah hii ni kweli kwa asilimia mia asee yaai ni ukweli mutupu muraaa!!!!
 
Umeandika kiaina fulani ambapo kwa upande wangu naona vya kujifunza ni vingi katika hivyo ulivyoandika kwani kwa kila mwenye moja kati ya hilo na akalifanya kinyume chake basi nadhani walio wengi watazidi kuuepuka huo umasikini badala ya kuukumbatia.

Hongera zako mleta uzi.
 
Very touching Quote,nimeisave mahala ili nianze kujitafakari!Mwezi huu huu,wiki hii hii kuanzia Kesho!!
 
mmmh Mchambuzi nimetia tim
 
wengine tunaupenda na tumeridhika kabisa na umsikini wetu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…