The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 1,497
- 2,681
Kiuhalisia hakuna anayependa kuishi na mwenzi wake mbali mbali, mnapokuwa kwenye mahusino ni muhimu mkawa pamoja, lakini kuna muda inatokea maisha yanawatenganisha kwa muda, katika hali hii ni nini mnatakiwa kufanya ili mahusiano yenu yadumu? Tuone mambo kadhaa ambayo mnatakiwa kufanya;
1. AMINIANENI.
Uaminifu ndio nguzo ya kila mahusiano, huu uhusiano hauji tu ila zipo sababu, ni lazima uwe muaminifu kweli ili uaminiwe. Kwa watu walio mbali mbali kitu cha muhimu ni uwazi katika kila jambo unalofanya. Ajue ratiba zako kama unatoka na mambo mengine, sio mwenzako anakupigia simu anasikia upo kwenye gari, anakuuliza unaenda wapi ndio unaanza kutoa maelezo sijui naenda kwa rafiki yangu, sijui naenda wapi, hiyo haifai. Ukiachana na maelezo nengine yote ila unatakiwa kuwa kuaminifu kweli.
2. KUWENI NA MAWASILIANO IMARA.
Tofauti na mahusiano mengine ambayo wao wapo pamoja muda wote, ila nyinyi mnaunganishwa na mawasiliano ya mara kwa mara. Hii itawasaidia kuendelea kuwa na hisia za pamoja muda wote. Msiache ipite siku bila mawasiliano.
3. AMBIANENI CHANGAMOTO ZENU.
Zungumzeni kuhusu hisia zenu, kile mnachopitia kila siku, ambianeni kuhusu huzuni zenu na furaha zenu, kama kuna shida hakikisheni mnajadili suruhisho la hilo. Manapokuwa mbali haimaanishi kuwa unapokuwa mpweke basi utafute mtu wa karibu kumuelezea upweke wako au shida zako, mueleze mwenzi wako.
4. LENGO LENU LIWE MOJA.
Lazima lengo lenu liwe moja, hii itawasaidia kuvumiliana, yani kila mtu anajua kwanini nipo mbali na mwenzangu, na hiyo sababu ya kuwaweka mbali iwe na mashiko.
5. MUWE NA RATIBA.
Mpo mbali mbali kwa sasa iwe muwe na ratiba ya lini sasa mtakuwa pamoja, hamuwezi kuishi hivyo siku zote. Kunapokuwa hakuna ratiba kamili inachosha, yani kutojua lini tutakuwa pamoja ni ngumu kuvumilika, watu huvumilia wanachokijua, kama hakijulikani ni ngumu kuvumilika.
6. EPUKENI MIGOGORO ISIYO YA LAZIMA.
Kama mnaishi mbali mbali halafu mnagombana bila sababu za msingi
1. AMINIANENI.
Uaminifu ndio nguzo ya kila mahusiano, huu uhusiano hauji tu ila zipo sababu, ni lazima uwe muaminifu kweli ili uaminiwe. Kwa watu walio mbali mbali kitu cha muhimu ni uwazi katika kila jambo unalofanya. Ajue ratiba zako kama unatoka na mambo mengine, sio mwenzako anakupigia simu anasikia upo kwenye gari, anakuuliza unaenda wapi ndio unaanza kutoa maelezo sijui naenda kwa rafiki yangu, sijui naenda wapi, hiyo haifai. Ukiachana na maelezo nengine yote ila unatakiwa kuwa kuaminifu kweli.
2. KUWENI NA MAWASILIANO IMARA.
Tofauti na mahusiano mengine ambayo wao wapo pamoja muda wote, ila nyinyi mnaunganishwa na mawasiliano ya mara kwa mara. Hii itawasaidia kuendelea kuwa na hisia za pamoja muda wote. Msiache ipite siku bila mawasiliano.
3. AMBIANENI CHANGAMOTO ZENU.
Zungumzeni kuhusu hisia zenu, kile mnachopitia kila siku, ambianeni kuhusu huzuni zenu na furaha zenu, kama kuna shida hakikisheni mnajadili suruhisho la hilo. Manapokuwa mbali haimaanishi kuwa unapokuwa mpweke basi utafute mtu wa karibu kumuelezea upweke wako au shida zako, mueleze mwenzi wako.
4. LENGO LENU LIWE MOJA.
Lazima lengo lenu liwe moja, hii itawasaidia kuvumiliana, yani kila mtu anajua kwanini nipo mbali na mwenzangu, na hiyo sababu ya kuwaweka mbali iwe na mashiko.
5. MUWE NA RATIBA.
Mpo mbali mbali kwa sasa iwe muwe na ratiba ya lini sasa mtakuwa pamoja, hamuwezi kuishi hivyo siku zote. Kunapokuwa hakuna ratiba kamili inachosha, yani kutojua lini tutakuwa pamoja ni ngumu kuvumilika, watu huvumilia wanachokijua, kama hakijulikani ni ngumu kuvumilika.
6. EPUKENI MIGOGORO ISIYO YA LAZIMA.
Kama mnaishi mbali mbali halafu mnagombana bila sababu za msingi