Jinsi ya kumjua tapeli kabla hajakupiga: Dalili za mawinga walafi

Jinsi ya kumjua tapeli kabla hajakupiga: Dalili za mawinga walafi

Davidmmarista

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
1,367
Reaction score
2,451
Wadau wa Jamiiforums, poleni na mihangaiko ya kutafuta tonge!

Kama hujawahi kupigwa kwenye biashara, basi ama wewe ni mjuzi wa hali ya juu, ama bado hujaingia kwa kina kwenye soko la Bongo! Wale ndugu zetu wa Kariakoo, Sinza, Tegeta na hata wale wa mikoani wanajua, "biashara ni akili" lakini pia "winga ni sehemu ya soko."

Leo nawaletea kisa cha jamaa yangu mmoja (mwenye jina nitalihifadhi kwa sababu za kiusalama). Jamaa huyu aliamua kununua gari kupitia dalali mmoja pale Mwenge. Akaambiwa gari lina hali nzuri, mwenyewe anahama nchi, bei ni ya mshikaji, na kwa bahati mbaya, "muhimu usichelewe maana kuna mtu mwingine ametangaza kulilipia kesho."

Jamaa akaenda benki fasta, akatoa pesa, akadondosha mkwanja kwa mzee wa watu! Wiki mbili baadaye, gari limepiga mluzi injini imekufa(engine ime nok), chombo kina deni la TRA na limeshakuwa reported kama "lost & found" huko polisi. Wadau, siyo kila biashara inatakiwa kumalizwa na haraka kama umeme wa TANESCO unavyokatika ghafla!

Kwa hiyo, ili tusijemaliza jasho letu bure kwa wajanja wa mjini, hizi hapa ni
"DALILI 11 ZINAZOKUONYESHA UNAFANYA BIASHARA NA TAPELI:*

1. Anakufanya Uhisi Fursa Imebaki Dakika Chache Tu
Tapeli atakutengenezea mazingira ya dharura ili uamue haraka, bila kufikiria sana. Atakwambia "Dogo, hii bidhaa iko hapa leo tu, kesho usije ukalia." Wanatumia mbinu hii kuhakikisha unafanya maamuzi bila kufanya uchunguzi wa kina.
Mfano: Unataka kununua kiwanja, dalali anakwambia kuna mzee mmoja ameshakilipia advance ila hajamalizia pesa, ukiwahi unakipata. Ukikubali bila kuhakiki, kesho unakuta mmiliki halali hajui chochote!

2. Anazungumza Lugha Nzuri Kupita Maelezo
Hawa watu wana vipaji vya kuzima hofu yako ili usijae upepo mapema kupitia maneno matamu. Atakupa "bro, mi ni mtu wa dini, sifanyi dhuluma" au atajitambulisha kama "rafiki wa rafiki yako."
Mfano: Unanunua simu, anakwambia "mimi ni fundi pia, ukiwa na shida nitakutunza, tena nina warranty ya miezi sita." Ukirudi kesho, simu haifanyi kazi, fundi naye haonekani!

3. Hataki Uhoji Sana Anachukia Maswali Mengi
Tapeli hapendi ukichimba sana maelezo. Ukitaka kuona vielelezo, anakwambia "bro, niamini, mbona unashuku sana?" Akiona unagundua madudu, anaweza hata kuanza kukasirika au kutukana.
Mfano: Unataka kununua pikipiki, ukimwambia akuonyeshe risiti halisi au umilikishaji, anasema "bro, unani-insult, kwani mimi mwizi?"

4. Anadai Ana "Connection" Kubwa Sana
Watapeli wanajifanya wana watu wa nguvu nyuma yao, kama vile viongozi, polisi, TRA, au mawakili, ili usiwe na wasiwasi.
Mfano: Unataka mkopo, anakwambia "mimi nawaunganisha watu Benki, nitakufanikishia bila shida." Mwisho wa siku unatoa pesa za "**process fee" **lakini mkopo wenyewe hauji!

5. Biashara Yake Inaonekana Nzuri Kupita Kiasi
Kama dili linaonekana tamu kupita maelezo, jiulize mara mbili. Tapeli atakupa bei ya kutamanisha au faida isiyo ya kawaida ili uingie kichwa kichwa.
Mfano: Unaletewa TV mpya ya inchi 55 kwa laki tatu tu eti "ni mali za mzigo ulioachwa bandarini." Ukichukua, siku moja unapewa habari kuwa umeuziwa mzigo wa wizi!

6. Anaepuka Mikataba au Stakabadhi Rasmi
Tapeli hapendi mambo ya maandishi. Ukimuomba mkataba au risiti halali, anasema "bro, umeniona si mtu wa maneno? Acha ushamba, hapa tunakubaliana kiheshima."
Mfano: Unakodisha nyumba, baba mwenye nyumba hajatoa risiti. Baada ya miezi mitatu, anakuambia hukulipa!

7. Anaogopa Kukutana Katika Maeneo Yenye Usalama
Tapeli hataki uende kwenye ofisi halali. Atakutaka mkutane sehemu zisizo rasmi kama vibanda vya kahawa au barabarani.
Mfano: Unataka kununua gari, anakwambia akutane naye kwenye parking ya mall fulani. Ukifika, anakuletea gari lakini hakupi muda wa kulichunguza vya kutosha.

8. Hakumbuki Maelezo Aliyokwambia Jana
Tapeli hana consistency. Leo akikwambia bidhaa imetoka Dubai, kesho anasema "ni za Malaysia." Ukimuuliza zaidi, anaanza kuchanganyikiwa.
Mfano: Ukinunua mashine ya kusaga, akisema ni mpya, lakini wiki ikipita unagundua imetumika miaka mitatu!

9. Anaomba Pesa Kabla ya Huduma au Bidhaa
Kama mtu anataka ulipe kabla hujapata kitu ulicholipia, hapo kuna walakini.
Mfano: Unatafuta kazi, mtu anakuambia "toa elfu hamsini nikuunganishe na kampuni moja." Ukitoa, kesho namba yake haipatikani!

10. Anabadili Msimamo Ghafla Ukiwa Makini Sana
Ukiwa makini na kuuliza sana maswali, tapeli atakimbia au atabadilisha stori haraka.
Mfano: Unapanga kununua shamba, ukiomba uhakiki nyaraka halali, anakwambia "siwezi kupoteza muda na mtu asiyetaka kuniamini."

11. Anapenda Kulia Sana au Kujifanya Ana Shida Kali
Matapeli hutumia huruma yako kama silaha. Wanaweza kujifanya wana matatizo makubwa ili uwarahisishie biashara.
Mfano: Anakupa dili la kiwanja, akisema "bro, mama yangu anaumwa, nauza kiwanja kwa bei ya hasara." Ukichukua, unakuja kugundua kiwanja hakiko kwenye jina lake!

TAFADHALI KUWA MJANJA!
Wadau wa JF, biashara ni nzuri lakini msiingie kichwa kichwa! Hakuna mtu anayeamka asubuhi kwa nia ya kukupatia dili la maisha bure. Fanya uchunguzi, usiharakishe, na ukiona dalili hata moja kati ya hizi, chukua tahadhari!
Kwa waliopigwa, pole sana. Kwa wanaopanga kufanya biashara, "usiruhusu tamaa ikupofushe!"

Nani amewahi kupatwa na mtego kama huu? Hebu tuambie hapa!

Nb. 😂Wale waliotapeliwa mwenge kwa Kudanganywa na nywele uwanja ni wenu?
 
Wadau wa Jamiiforums, poleni na mihangaiko ya kutafuta tonge!

Kama hujawahi kupigwa kwenye biashara, basi ama wewe ni mjuzi wa hali ya juu, ama bado hujaingia kwa kina kwenye soko la Bongo! Wale ndugu zetu wa Kariakoo, Sinza, Tegeta na hata wale wa mikoani wanajua, "biashara ni akili" lakini pia "winga ni sehemu ya soko."

Leo nawaletea kisa cha jamaa yangu mmoja (mwenye jina nitalihifadhi kwa sababu za kiusalama). Jamaa huyu aliamua kununua gari kupitia dalali mmoja pale Mwenge. Akaambiwa gari lina hali nzuri, mwenyewe anahama nchi, bei ni ya mshikaji, na kwa bahati mbaya, "muhimu usichelewe maana kuna mtu mwingine ametangaza kulilipia kesho."

Jamaa akaenda benki fasta, akatoa pesa, akadondosha mkwanja kwa mzee wa watu! Wiki mbili baadaye, gari limepiga mluzi injini imekufa(engine ime nok), chombo kina deni la TRA na limeshakuwa reported kama "lost & found" huko polisi. Wadau, siyo kila biashara inatakiwa kumalizwa na haraka kama umeme wa TANESCO unavyokatika ghafla!

Kwa hiyo, ili tusijemaliza jasho letu bure kwa wajanja wa mjini, hizi hapa ni
"DALILI 11 ZINAZOKUONYESHA UNAFANYA BIASHARA NA TAPELI:*

1. Anakufanya Uhisi Fursa Imebaki Dakika Chache Tu
Tapeli atakutengenezea mazingira ya dharura ili uamue haraka, bila kufikiria sana. Atakwambia "Dogo, hii bidhaa iko hapa leo tu, kesho usije ukalia." Wanatumia mbinu hii kuhakikisha unafanya maamuzi bila kufanya uchunguzi wa kina.
Mfano: Unataka kununua kiwanja, dalali anakwambia kuna mzee mmoja ameshakilipia advance ila hajamalizia pesa, ukiwahi unakipata. Ukikubali bila kuhakiki, kesho unakuta mmiliki halali hajui chochote!

2. Anazungumza Lugha Nzuri Kupita Maelezo
Hawa watu wana vipaji vya kuzima hofu yako ili usijae upepo mapema kupitia maneno matamu. Atakupa "bro, mi ni mtu wa dini, sifanyi dhuluma" au atajitambulisha kama "rafiki wa rafiki yako."
Mfano: Unanunua simu, anakwambia "mimi ni fundi pia, ukiwa na shida nitakutunza, tena nina warranty ya miezi sita." Ukirudi kesho, simu haifanyi kazi, fundi naye haonekani!

3. Hataki Uhoji Sana Anachukia Maswali Mengi
Tapeli hapendi ukichimba sana maelezo. Ukitaka kuona vielelezo, anakwambia "bro, niamini, mbona unashuku sana?" Akiona unagundua madudu, anaweza hata kuanza kukasirika au kutukana.
Mfano: Unataka kununua pikipiki, ukimwambia akuonyeshe risiti halisi au umilikishaji, anasema "bro, unani-insult, kwani mimi mwizi?"

4. Anadai Ana "Connection" Kubwa Sana
Watapeli wanajifanya wana watu wa nguvu nyuma yao, kama vile viongozi, polisi, TRA, au mawakili, ili usiwe na wasiwasi.
Mfano: Unataka mkopo, anakwambia "mimi nawaunganisha watu Benki, nitakufanikishia bila shida." Mwisho wa siku unatoa pesa za "**process fee" **lakini mkopo wenyewe hauji!

5. Biashara Yake Inaonekana Nzuri Kupita Kiasi
Kama dili linaonekana tamu kupita maelezo, jiulize mara mbili. Tapeli atakupa bei ya kutamanisha au faida isiyo ya kawaida ili uingie kichwa kichwa.
Mfano: Unaletewa TV mpya ya inchi 55 kwa laki tatu tu eti "ni mali za mzigo ulioachwa bandarini." Ukichukua, siku moja unapewa habari kuwa umeuziwa mzigo wa wizi!

6. Anaepuka Mikataba au Stakabadhi Rasmi
Tapeli hapendi mambo ya maandishi. Ukimuomba mkataba au risiti halali, anasema "bro, umeniona si mtu wa maneno? Acha ushamba, hapa tunakubaliana kiheshima."
Mfano: Unakodisha nyumba, baba mwenye nyumba hajatoa risiti. Baada ya miezi mitatu, anakuambia hukulipa!

7. Anaogopa Kukutana Katika Maeneo Yenye Usalama
Tapeli hataki uende kwenye ofisi halali. Atakutaka mkutane sehemu zisizo rasmi kama vibanda vya kahawa au barabarani.
Mfano: Unataka kununua gari, anakwambia akutane naye kwenye parking ya mall fulani. Ukifika, anakuletea gari lakini hakupi muda wa kulichunguza vya kutosha.

8. Hakumbuki Maelezo Aliyokwambia Jana
Tapeli hana consistency. Leo akikwambia bidhaa imetoka Dubai, kesho anasema "ni za Malaysia." Ukimuuliza zaidi, anaanza kuchanganyikiwa.
Mfano: Ukinunua mashine ya kusaga, akisema ni mpya, lakini wiki ikipita unagundua imetumika miaka mitatu!

9. Anaomba Pesa Kabla ya Huduma au Bidhaa
Kama mtu anataka ulipe kabla hujapata kitu ulicholipia, hapo kuna walakini.
Mfano: Unatafuta kazi, mtu anakuambia "toa elfu hamsini nikuunganishe na kampuni moja." Ukitoa, kesho namba yake haipatikani!

10. Anabadili Msimamo Ghafla Ukiwa Makini Sana
Ukiwa makini na kuuliza sana maswali, tapeli atakimbia au atabadilisha stori haraka.
Mfano: Unapanga kununua shamba, ukiomba uhakiki nyaraka halali, anakwambia "siwezi kupoteza muda na mtu asiyetaka kuniamini."

11. Anapenda Kulia Sana au Kujifanya Ana Shida Kali
Matapeli hutumia huruma yako kama silaha. Wanaweza kujifanya wana matatizo makubwa ili uwarahisishie biashara.
Mfano: Anakupa dili la kiwanja, akisema "bro, mama yangu anaumwa, nauza kiwanja kwa bei ya hasara." Ukichukua, unakuja kugundua kiwanja hakiko kwenye jina lake!

TAFADHALI KUWA MJANJA!
Wadau wa JF, biashara ni nzuri lakini msiingie kichwa kichwa! Hakuna mtu anayeamka asubuhi kwa nia ya kukupatia dili la maisha bure. Fanya uchunguzi, usiharakishe, na ukiona dalili hata moja kati ya hizi, chukua tahadhari!
Kwa waliopigwa, pole sana. Kwa wanaopanga kufanya biashara, "usiruhusu tamaa ikupofushe!"

Nani amewahi kupatwa na mtego kama huu? Hebu tuambie hapa!

Nb. 😂Wale waliotapeliwa mwenge kwa Kudanganywa na nywele uwanja ni wenu?
Research nzuri mkuu 🤝
 
Nani amewahi kupatwa na mtego kama huu? Hebu tuambie hapa!


Mkuu kwani wewe upo kundi lipi?

Umetutega sana na mada zako za kuomba Ushauri, mara Umeajiri watu, Ukawa mjasiariamali, mara pop, unasomea hacking, web designing, php, IQ kubwa, java, Engineering halafu sasa unatufunda tukutambue?

Mimi nishapatwa na mtego huu. Nakiri mapema. Umenipata Mkuu.😇😇😇

I'm Innocent😇
 
Mkuu kwani wewe upo kundi lipi?

Umetutega sana na mada zako za kuomba Ushauri, mara Umeajiri watu, Ukawa mjasiariamali, mara pop, unasomea hacking, web designing, php, IQ kubwa, java, Engineering halafu sasa unatufunda tukutambue?

Mimi nishapatwa na mtego huu. Nakiri mapema. Umenipata Mkuu.😇😇😇

I'm Innocent😇
Learning is a key part of success, Mkuu. Kuuliza maswali na kuomba ushauri si udhaifu, bali ni dalili ya mtu mwenye malengo makubwa. A growth-minded person always seeks knowledge, engages in deep conversations, and challenges different perspectives.
Kujadili na kubishana kwa hoja kunapanua ufahamu, testimony zinaleta tumaini, na kuelewa mitazamo tofauti kunaharakisha maendeleo. So, siyo kila anayechangamka kwenye mada nyingi amepotea huenda ndiye anayejua anapokwenda zaidi ya wengi!
#BeYourself
 
Usisahahu na wale wenye IQ kubwa.

Wanaomaliza kusomea ......kwa miezi tisa tu.
Brother nimeona ni kujibu. Watu msichokijua ni kwamba nipo kwenye tech industry kwa zaidi ya miaka 5. Nilianza na blogging kupitia WordPress, nikapata mpunga mzuri na Adsense kipindi iyo. Wakati huo kwenye search engine nilipambana na majina makubwa kama RAJMPELLA na DARASALETU.
Baadaye, niliendesha TeleElimu website ya educational resources, ambayo ilinilipa vizuri. Lakini baada ya muda niliiondoa na kuingia kwenye mishe zingine. Mimi sipendi kuonekana hadharani, natumia jina fake for privacy puri lakini huwa natoa mafanikio ya kweli humu nimefanya biashara nyingi almost 7 years.
Nina upendo mkubwa kwa ukweli, I love deep conversation, pia truth seeking. Napenda kujifunza kutoka kwa wengine kwa sababu sichoki kutafuta maarifa, enzi hizi huwezi kuweka mayai yote kwenye kapu moja. Nadhani nimekujibu, kaka.
 
Kuna dingi aliniambia hii mashine ni ya mjerumani, lkn kwenye label imeandikwa china, nikambembeleza kwa bei yangu akakataa akasema kwanza hii kuna mtu kaitangulizia pesa mida hii hii, kesho atakuja kumalizia, leo ni mwezi wa pili nikipita pale naiona ipo ndani tuu.
 
Hii ya gari ilitaka kunikuta Kinondoni mwaka jana.

Gari ilitangazwa kwenye mtandao inauzwa. Gari ilikuwa namba EA, imenyooka na bei yake iliyoandikwa ilkuwa ya chini mno, hii ilipaswa iwe red flag ya kwanza lakini nikapuuza.

Kupiga simu aliepokea ni dalali, akasema nikiwa tayari nimwambie tukaiangalie ila ni nisichelewe gari 'hot cake'. tulikubaliana tukutane Tazara ili tuende Kinondoni, kweli nilimkuta kituoni akaingia kwenye gari safari ikaanza.

Tukiwa njiani akampigia simu mtu mwingine ambae inaelekea nae ni dalali, swali la kwanza aliloulizwa (vitochi hata kama simu haipo speaker ni rahisi kusikia sauti ya upande wa pili) kama ana uhakika unaekuja nae sio mjuaji 'red flag' ya pili.

Kufika kwenye gari sasa, gari imenyooka balaa ila imepakiwa kwenye banda ndani ya garage, kutaka test drive naambiwa nisubiri kidogo maana kuna bar karibu kuna defender ya polisi imepaki na gari haina insurance, red flag ya tatu.

Ila kipindi hicho wana force nilipe maana nilimwambia dalali wa kwanza kuwa cash ninayo kwenye gari. Walidai mwenye gari ni pastor, hakai mbali na hapo garage na anataka kusafiri jioni hiyo. Kuomba card ya gari, nikaambiwa ipo copy, pastor kapoteza original ila nisihofu kesho yake watanitolea original TRA.

Mpaka hapo nilishajua kuwa hilo gari lina walakini. Nikaamua kuangalia tu insurance kwa kutumia simu, details za gari kwa mujibu wa registration number ilikuwa Toyota Crown, wakati gari inayouzwa ni IST. Kumuuliza dalali, wote 2 kama walitaharuki na matusi yakaanza sasa kuwa najifanya mjuaji sana na nisipokuwa makini watanifanyia kitu kibaya.

Kipindi hicho yule dalali tuliemkuta kasimama mlango wa nyuma wa gari niliyokwenda nayo kama anaetaka kufungua maana kulikuwa na begi dogo nahisi akiamini ndio kulikuwa na pesa, ukweli sikuwa nimebeba pesa yeyote.

Kwa bahati nzuri simu yangu iliita, nikaunganisha tu kumwambia aliepiga kuwa maneno yako kweli, zungukeni tu mje hapa. Ndani ya sekunde wale madalali walipotea, kila mtu na njia yake.

Kwa kifupi, likija swala la biashara haijalishi una uhihitaji wa hiyo bidhaa kiasi gani epuka sana papara na if it seems too good to be true, chances are it is.
 
Kuna dingi aliniambia hii mashine ni ya mjerumani, lkn kwenye label imeandikwa china, nikambembeleza kwa bei yangu akakataa akasema kwanza hii kuna mtu kaitangulizia pesa mida hii hii, kesho atakuja kumalizia, leo ni mwezi wa pili nikipita pale naiona ipo ndani tuu.
😂Aise ujanja ujanja wa kwenye biashara
 
Hii ya gari ilitaka kunikuta Kinondoni mwaka jana.

Gari ilitangazwa kwenye mtandao inauzwa. Gari ilikuwa namba EA, imenyooka na bei yake iliyoandikwa ilkuwa ya chini mno, hii ilipaswa iwe red flag ya kwanza lakini nikapuuza.

Kupiga simu aliepokea ni dalali, akasema nikiwa tayari nimwambie tukaiangalie ila ni nisichelewe gari 'hot cake'. tulikubaliana tukutane Tazara ili tuende Kinondoni, kweli nilimkuta kituoni akaingia kwenye gari safari ikaanza.

Tukiwa njiani akampigia simu mtu mwingine ambae inaelekea nae ni dalali, swali la kwanza aliloulizwa (vitochi hata kama simu haipo speaker ni rahisi kusikia sauti ya upande wa pili) kama ana uhakika unaekuja nae sio mjuaji 'red flag' ya pili.

Kufika kwenye gari sasa, gari imenyooka balaa ila imepakiwa kwenye banda ndani ya garage, kutaka test drive naambiwa nisubiri kidogo maana kuna bar karibu kuna defender ya polisi imepaki na gari haina insurance, red flag ya tatu.

Ila kipindi hicho wana force nilipe maana nilimwambia dalali wa kwanza kuwa cash ninayo kwenye gari. Walidai mwenye gari ni pastor, hakai mbali na hapo garage na anataka kusafiri jioni hiyo. Kuomba card ya gari, nikaambiwa ipo copy, pastor kapoteza original ila nisihofu kesho yake watanitolea original TRA.

Mpaka hapo nilishajua kuwa hilo gari lina walakini. Nikaamua kuangalia tu insurance kwa kutumia simu, details za gari kwa mujibu wa registration number ilikuwa Toyota Crown, wakati gari ni IST. Kumuuliza dalali, jamaa wote kama walitaharuki na matusi yakaanza sasa kuwa najifanya mjuaji sana na sipokuwa makini watanifanyia kitu kibaya.

Kipindi hicho yule dalali tuliemkuta kasimama mlango wa nyuma wa gari niliyokwenda nayo kama anaetaka kufungua maana kulikuwa na begi dogo nahisi akiamini ndio kulikuwa na pesa, ukweli sikuwa nimebeba pesa yeyote.

Kwa bahati nzuri simu yangu iliita, nikaunganisha tu kumwambia aliepiga kuwa maneno yako kweli, zungukeni tu mje hapa. Ndani ya sekunde wale madalali walipotea, kila mtu na njia yake.

Kwa kifupi, ikija swala la biashara haijalishi unahitaji bidhaa kiasi gani epuka sana papara na if it seems too good to be true, chances are it is.
Ni kweli mkuu, jamaa yangu mmoja aliwahi kupigwa 20M border huko Rombo alitaka kununua fuso aise wahuni sio watu wazuri kabisa aliliwa 20M hadi Leo hii akijaribu kudai haiwezekani huwa ananiambia ipo siku atavizia chungu apige maana huyo jamaa anasumbua, jamaa yangu huwa anasema kila akifika kwa huyo jamaa anaambiwa since 2020 mwamba yupo Kenya na familia yake haijawahi kumwona
 
Back
Top Bottom