Jinsi ya kumuondoa mdudu aliyeingia ndani ya sikio

Jinsi ya kumuondoa mdudu aliyeingia ndani ya sikio

Pastor Achachanda

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2012
Posts
3,023
Reaction score
1,315
Habari zenu wana JF. Leo nawaletea mbinu za kumuondoa mdudu aliyeingia sikioni.

Kuna baadhi ya wadudu huwa wanapenda kuingia masikioni kama vile mende,chawa,nzi nk. Tunamuondoaje?:Tumia moja kati ya njia hizi:

1. Elekeza kichwa chako kwenye jua. Kama ni usiku elekeza kwenye mwanga wa umeme kwa muda mrefu. Kichwa chako kikigusana na mwanga kwa muda mrefu huleta joto linaloweza kumfukuza mdudu.

2. Chukua kipande kidogo cha tufaha(apple)kiweke jirani na sikio lako(next to the ear). Mdudu ikimkuta harufu ya tufaha inamtoa nje.

3. Inamisha kichwa upande kwa chini na mtu mwingine akutie mafuta ya kupikia kwenye sikio lenye mdudu. Mafuta yakisha ingia ruhusu yakae kwa muda wa dakika moja hivi halafu ruhusu yatoke. Yanapotoka yanatoka na mdudu.

4. Weka maji ya uvuguvugu sikioni ukiwa umeinama. Kaa na hayo maji dakika 3. Kisha kohoa ukiwa ukiwa umekandamiza kifua kisha inamisha sikio chini na urukeruke kichwa upande na utaona mdudu anatoka.

Yote haya kama hujafanikiwa nenda hospitali.
Pastor Achachanda.
 
njia rahisi ni kumwagia mkojo wako uliokojoa haponhapo ambao una joto...dakika sifuri mdudu atakimbia mwenyewe...inamisha sikioa mwaga mkojo kisha osha...
 
Hata hizi pamba za kusafishia masikion ni muhimu kuwa makini nazo. Nyingine siku hizi ukiingiza tu tayari inajitoa kwenye kale ka plastic holder then inabaki ndani ya sikio.

Na kuitoa ka imeingia sana ndani baadh ya wataalam wa afya wanazingua tu wanaingiza mamikasi kwa mwanga wa toch ya NOKIA kitoch daaah wanaumiza tu masikio kumbe kuna utaalam wa kutoa kwa bomba maalumu lenye maji yanayoingizwa ndani ya sikio na kutoka na kipande kilichobaki sikioni.
 
Hiyo namba 3, sina hakika nayo kwakuwa mama yangu tuliwahi kumwekea mafuta ya kupika na huyo mdudu alifia sikioni.

Tulipompeleka hospitali walimtoa kwa vifaa vyao.Ila daktari alikataza kutumia mafuta.

Mi nadhani Pastor ungefanya utafiti yakinifu kabla hujawashauri, ni kweli huduma ya kwanza inahitajika lakini iwe salama.
 
Hiyo namba 3, sina hakika nayo kwakuwa mama yangu tuliwahi kumwekea mafuta ya kupika na huyo mdudu alifia sikioni.Tulipompeleka hospitali walimtoa kwa vifaa vyao.Ila daktari alikataza kutumia mafuta.
Mi nadhani Pastor ungefanya utafiti yakinifu kabla hujawashauri, ni kweli huduma ya kwanza inahitajika lakini iwe salama.

Nimekuelewa mkuu. Inategemea na aina ya mafuta kwani mengi yana kemikali na kwa kila mdudu anabeba sumu inaitwa fs12 ambayo ikikutana na mafuta yenye kemikali kali inamkata mdudu katikati na ile fs12 inabakia ndani ya sikio ambapo inachanganyikana na nta(earwax)na kugeuka nta kamili baada ya masaa 18.

Kwa mafuta yasiyo na kemikali yanamzingira mdudu na kumtoa bila kuvunja sumu ya fs12. Rejea unapomkatakata kuku kama ukavunjishia nyongo kwenye nyama.
Akubarikini mwenyezi Mungu baba na mwana na Roho mtakatifu. Amen
 
Hata hizi pamba za kusafishia masikion ni muhimu kuwa makini nazo. Nyingine siku hizi ukiingiza tu tayari inajitoa kwenye kale ka plastic holder then inabaki ndani ya sikio. Na kuitoa ka imeingia sana ndani baadh ya wataalam wa afya wanazingua tu wanaingiza mamikasi kwa mwanga wa toch ya NOKIA kitoch daaah wanaumiza tu masikio kumbe kuna utaalam wa kutoa kwa bomba maalumu lenye maji yanayoingizwa ndani ya sikio na kutoka na kipande kilichobaki sikioni.

Ni kweli mkuu. Wachina ni wagumu kutofautisha pamba za kusafisha masikio watoto na wakubwa. Mara nyingi tunashauri mtu asitumie pamba hizi. Kutegemeana na ukubwa wa sikio.

Kama sikio ni kubwa tumia nyoya la mkiani la jogoo. Kama ni dogo kama la Lady A tumia nyoya mkiani la kuku jike(tetea). Jitahidi upate la kuku wa kienyeji.
 
Mie imewahigi kunitokea.......nikawekewa maji kwenye sikio ile
kuinamisha mdudu akatoka ......mda huo nilikuwa sijielewi nang'ang'ania
twende hosp ila kwenye wengi pana mengi nikafanikiwa kwa huo ushauri
 
niliwahi kuingiwa na kumbikumbi vile vidogo sikioni nikapata ukichaa yani kadili alivyokuwa akipiga mabawa yake mimi nilikuwa nahisi uwendaazimu, nilitafuta hospitali bila kupenda.
 
Nzuri sana hiyo, nilisikia stori ya mtu mmoja aliingiwa na kupe sikioni mwake aliweka dawa ya kuogeshea mifugo usiku kabla ya kulala alikutwa amefariki,.
 
mafuta ya kupikia yanamtoa kupe aliyejishkiza ndani ya sikio?.
 
Back
Top Bottom