JacksonMichael
JF-Expert Member
- Mar 22, 2012
- 339
- 61
Mkuu umekusudia Mnyama yupi wa Taifa? Ng'ombe? Nyama ya Ng'ombe ina madhara bora ule nyama ya kuku kuliko kula nyama ya ng'ombe au Kitomoto nyama zote zina madhara ila nyama ya kuku ndio bora inafaa kuliwa wakati wote mkuu.
Ongeza na asali limau na maji ya uvuguvugu utaona faida yake kubwa. PUNGUZA UNENE KWA ASALI NA LIMAUMzizimkavu mie nikinywa maji asubuhi najitahidi yawe ya uvugu vugu ..naweka limao kidogo lakini lazima yarudi kama yalivyoingia
Na mida yenyewe unajiandaa kwenda job ndo unakunywa hayo maji kazi kweli
Pili naona kama wewe unazidisha malimao sana.
Nadhani yana madhara .naomba ufafanuzi juu ya hili.
Mkuu mimi Siwezi kutoa Ushauri mbaya eti niruhusu Watu watumie KITOMOTO nyama ya nguruwe la hasha wewe kama unakula hicho Kitomoto nyama ya Nguruwe shauri yako wewe na afya yako. KITOMOTO nyama ya nguruwe ina madhara makubwa kwenye afya ya binadamu si vizuri kukitumia.Kaka mbona unazunguka? KITIMOTO ndo hatari zaidi na ndio wataalamu wanavyosema! pia sio sahihi kusema kuku wapo poa? una maana gani maana kuku wa sasa wanafugwa kwa wiki 6 tu na wanakula madawa balaa nasikiwa watu wengine wanawapiga na ARV kidogo basi ananenepa hatari, kwa hiyo sidhani kama kuku hawa ndio uliowazungumzia!
Pole sana bibie kwa hayo maradhi ya vidonda vya tumbo kuhusu kunywa maji asubuhi ningelikushauri uwe unakunywa maji ya Uvuguvugu glasi moja yaliyochanganywa na asali kijiko kimoja kila siku asubuhi kabla ya kula kitu hiyo itakusaidia kuondosha mafuta mwilini mwako haswa kwenye figo na moyo. Pili kuhusu maradhi yako ya Vidonda vya tumbo jaribu kutumia dawa hiiThnx kwa kushare nasisi mambo mazuri mazuri.
Mimi hilo la kunywa maji ya uvuguvugu asubuhi sijaweza, nakunywa ya kawaida km gilasi 3 au 4 kabla sijbrush, jee hayafai au niendelee nayo hayohayo.
Then mm nina ulcer matunda mengi yananishinda, nlijaribu kupractice lkn nlishindwa, jee unanishauri nitumie nn mbadala.
Nashkuru nimeweza kupunguza vitu vya sukari na mafuta, nimelose kg km 5 hivi ndani ya mwaka m1.
Inataka moyo, kazi si ndogo.
FL, (nje ya topic) please badilisha hiyo signature yako, maana INAPOTOSHA!
Labda mimi ninaona kakupenda umwambie ukweli kuwa wewe ni mke wa mtu asikufuate fuate.na wewe bwana badala ya kubalance diet unapotoshwa na signature
hahahaha Mzizimkavu ..labda kweli kapotoshwa ..Labda mimi ninaona kakupenda umwambie ukweli kuwa wewe ni mke wa mtu asikufuate fuate.
Ongeza na asali limau na maji ya uvuguvugu utaona faida yake kubwa. PUNGUZA UNENE KWA ASALI NA LIMAU
​Unene wa mwili wa kupita kiasi (obesity) ni miongoni mwa matatizo ya kiafya yanayowasumbua watu wengi. Kuna njia nyingi za kufanya ili kupunguza unene, yakiwemo mazoezi ya viungo na kutumia baadhi ya vyakula kimpangilio.
Unene wa kupita kiasi ni hali inayomtokea mtu pale mafuta yanaporundikana kwenye ‘tishu' za mwili hivyo kusababisha matatizo kwenye moyo, figo, ini, viungio vya mwili kama vile magoti, n.k.
Halikadhalika, watu wenye matatizo ya uzito wa kupindukia huweza kupatwa na matatizo pia ya shinikizo la damu, kisukari, magonjwa ya msuli, ini na hata kibofu cha mkojo. Kwa ujumla unene siyo mzuri na ni chanzo cha maradhi mengi hatari. Kama unajali afya yako, unene ni wa kuogopwa kama ukoma.
Habari njema kuhusu tatizo hilo ni kwamba unaweza kujikinga nalo kwa kutumia asali na kama tayari unalo unaweza kulitibu au kulidhibiti kwa kutumia asali kwa kuchanganya na limau kwa utaratibu maalum.
Asali ni tiba nzuri ya kiasili ya kutibu tatizo la unene pamoja na shinikizo la damu, kwani hupunguza mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol) kwa kuyageuza mafuta ya ziada kuwa nishati ya mwili. Mtu unaweza kufunga kula vitu vingine na badala yake ukatumia asali na limau tu kama tiba ya unene, bila kupoteza hamu yako ya kula au nguvu ya mwili.
JINSI YA KUTENGENEZA ASALI NA LIMAU
Kuna imani potofu kwa baadhi ya watu kuhusu limau na asali kuwa ni sumu. Ukweli ni kwamba mchanganyiko huu ambao ni wa ‘alkalaini' mwilini siyo sumu bali ni tiba kwa matatizo mengi ya kiafya, likiwemo tatizo la unene.
Ili kupata mchanganyiko sahihi, weka asali mbichi kwenye kijiko kimoja kidogo kwenye glasi yenye maji ya uvugu uvugu (siyo yaliyochemka), kisha weka vijiko viwili vya juisi ya limau (saizi ya kijiko cha chai) halafu koroga na unywe mchanganyiko huo.
Kunywa mchangayiko huo asubuhi kabla hujala kitu chochote au unaweza kunywa mchangayiko huo kila baada ya mlo mkubwa au ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, mchanganyiko huo husaidia usagaji wa chakula na uondoaji wa sumu mwilini.
Katika kutekeleza mpango huu kwa lengo la kupunguza unene, usisahau kuzingatia suala la ulaji wa vyakula vyenye faida mwilini na vinavyoruhusiwa kiafya. Itakuwa ni kazi bure iwapo utatumia tiba ya asali huku ukiendelea na ulaji wa vyakula usiyokubalika kiafya. Halikadhalika mazoezi ya mara kwa mara ni suala muhimu kuzingatiwa.
COCKTAIL YA MATUNDA NA ASALI
Aidha, katika kuimarisha kinga na kuondoa sumu zaidi mwilini, unaweza kutengeneza mchanganyiko wa matunda mengi (fruit cocktail) pamoja na asali na kisha ukanywa. Kufanikisha hilo, chukua matunda kama vile epo, nanasi, zabibu, machungwa, karoti na mapera, yaandae vizuri kisha weka kwenye blenda na tengeneza juisi, bila kusahahu kuweka vijiko viwili vya asali mbichi. Tengeneza kiasi cha glasi moja na kunywa wakati ule ule kwa lengo la kupata vitamini zote bila kupotea.
Mwisho, ili kujiepusha na unene wa kupindukia, usipende kula kupita kiasi, hasa vyakula vyenye mafuta, ili hali hufanyi mazoezi wala hufanyi kazi yoyote ya shuruba. Unene ni dalili ya maradhi, jiepushe nao.
Ok, Inshaallah.Mkuu mimi Siwezi kutoa Ushauri mbaya eti niruhusu Watu watumie KITOMOTO nyama ya nguruwe la hasha wewe kama unakula hicho Kitomoto nyama ya Nguruwe shauri yako wewe na afya yako. KITOMOTO nyama ya nguruwe ina madhara makubwa kwenye afya ya binadamu si vizuri kukitumia.
Pole sana bibie kwa hayo maradhi ya vidonda vya tumbo kuhusu kunywa maji asubuhi ningelikushauri uwe unakunywa maji ya Uvuguvugu glasi moja yaliyochanganywa na asali kijiko kimoja kila siku asubuhi kabla ya kula kitu hiyo itakusaidia kuondosha mafuta mwilini mwako haswa kwenye figo na moyo. Pili kuhusu maradhi yako ya Vidonda vya tumbo jaribu kutumia dawa hii
Pata au weka vijiko viwili vikubwa unga wangano,vijiko viwili mafuta ya kupikia, nusu lita Maziwa Fresh ya Ng'ombe. Unga wa ulezi kidogo. pika uji vikombe vinne ikisha unywe kutwa mara 4 kwa muda wa mwezi moja Inshaallah kwa kudra ya Mola utapona. tumia dawa hiyo kisha unipe Feedback.
Hii sio ya kitaalamu bali ni mimi ninavyofanya na ndio inayonisaidia kupunguza tumbo.
Kwasababu vitu vya formula mimi huwa siwezi kuvifuata na huwa naviona vigumu sana kwahiyo huwa najaribu kuishi vile ninavyoweza.
Na kizuri zaidi ni kwamba hii sio diet ya kujinyima.
Ila unaweza usifanikiwe pia kutokana na mwili wako kwakua tumeumbwa tofauti lakini unaweza kujaribu kama itafanya kazi
.
.
Kuku Choma ni chakula kingine ambacho kinanifaa nyakati za mchana, lakini haswa hupendelea Kuku wa kienyeji ambao hawakukuzwa kwa madawa
Mara nyingi usiku naipotezea tu, pengine nalalia glass 2 za wine au beer kadhaa zisizozidi 3
Au Kuku wa kienyeji wa kuchemsha aliewekwa chumvi na ndimu na ka ndizi kamoja ka kuchemsha au kukaanga kwa mafuta kidogo sana
.
.
.
Hapo kwenye red, vileo (bia, wine, etc) vimekatazwa.
Soma Waraka wa kwanza wa Petro, mlango wa 4, kuanzia mstari wa kwanza mpaka wa mstari wa tano ( 1 Petro 04:01-05) inasomeka kama ifuatavyo:-
"
1 Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.
2 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.
5 Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa."
Kuna ulevi na unywaji?
Pombe anaweza kunywa in moderation. Ama chupa mbili za bia kwa siku au glasi moja ya mvinyo mwekundu kwa siku.
Kwanza kabisa tujue kwamba kuwa na kitambi na kuwa na mafuta(FATS) mengi mwilini ni vitu vinavyo endana kwa ukaribu sana kwani Fats nyingi mwilini hufanya storage kwenye tumbo na hata kwenda kwenye makalio(******) hii ni kwa wanaume,na kwa wanawake fat storage hufanyika kwenye misuli ya mikono ya nyuma(triceps),hips,matakoni na baadaye kuhamia kwenye tumbo,
Tafiti zinasema kuwa fats zinazokuwa tumboni ndio fats mbaya kuliko fats nyingine zote ambazo ziko mwilini,inasemekana kuwa ndio fats zinazosababisha higher cholesterol levels,higher blood sugar,heart disease and raised blood pressure.Kwahiyo sasa unapotaka kupungua jua kuwa unataka kutoa mafuta mwilini kwahiyo ili utoe mafuta ni lazima ufanye mazoezi ambayo yatatoa Fats ndani ya mwili mzima na sio sehemu moja tuu ya mwili,Unaweza ukafanya sana situps na mazoezi mengine mengi ya tumbo lakini tumbo halitapungua bali utalikomaza tuu na mwishoni litakuwa gumu zaidi hata kutoa fats zilizomo.Ningependa kuwaambia wasomaji wangu kwamba hakuna zoezi la kutoa kitambi peke yake bila kupungua mwili mzima na ni ngumu sana kutoa body Fats kama hutafanya mazoezi ya kushirikisha mwili wako wote kwa muda wa lisaa limoja au dakika 45,kwa kawaida mwili huanza kuburn Body Fats kwa ajili ya kutumika kama enegry baada ya nusu saa wakati unafanya zoezi.Kabla ya hapo mwili unakuwa unatumia the available energy, kwa mfano wakati ukiwa unakimbia au kuendesha baiskeli baada ya nusu saa mwili wako huanza kuunguza mafuta kwa ajili ya kukupa nguvu ya wewe kuendelea na ndipo hapo tunasema unaburn calories mwilini.Ushauri wangu kwa wasomaji wangu ni kwamba njia pekee ya kupungua ni kufanya mazoezi yanayo shirikisha viungo vyako vyote kwa pamoja na hakikisha unafanya kwa muda usio pungua lisaa limoja au dakika 45.Na kama unamwili wa kawaida hutaki kupungua bali unapenda kufanya mazoezi kwa ajili ya afya basi fanya mazoezi kwa nusu saa tuu kwa wiki hata mara tatu sio mbaya utaendelea kuonekana ni mwenye afya na mtanashati na unae jiamini kwa wakati wote.