Dr. Wansegamila
JF-Expert Member
- Feb 3, 2012
- 2,968
- 8,139
Mara nyingi nimekuwa nikiona threads humu ndani watu wakiulizia unawezaje kuhesabu siku na kujua zile siku za hatari ambazo mwanamke anaweza kushika mimba; naomba leo nitoe somo kidogo.
Kwanza,napenda tufahamu yafuatayo.
1. Ili njia hii iweze kuwa effective ni muhimu kwa mwanamke akawa na mzunguko ambao haubadiliki badiliki(regular menstrual cycle).
2. Njia hii ni less effective kwa wasichana walio chini ya miaka 25 na ambao bado hawajawahi kushika ujauzito kwa sababu wanawake hawa mara nyingi wanakuwa na very irregular menstrual cycles(mizunguko yao ya hedhi inabadilika badilika sana).
Sasa tuanze somo;kwa wanawake wenye mzunguko wa siku 28,siku ya kupevuka kwa yai ni siku ya 14,na yai baada ya kupevuka lina uwezo wa kuwa hai kwa wastani wa masaa 72;pia mbegu za kiume zinakuwa hai kwa wastani wa masaa 48-72. Lakini pia,yai linaweza kupevuka siku mbili kabla au baada(yaani siku ya 12-16). Kwa mahesabu hayo basi, siku za hatari ni kuanzia siku ya 9 mpaka ya 19;ndani ya siku hizi hutakiwi kufanya mapenzi bila kinga kama hutaki kushika mimba. So either usifanye mapenzi katika siku hizi au utumie kinga.
Kwa wale wanawake ambao mzunguko wao si wa siku 28,wao siku ya kupevuka yai wahesabu kwa kuchukua jumla ya siku za mzunguko wao kutoa 14(mfano kama mzunguko wako ni siku 32;chukua 32-14=18,kwa hiyo siku ya 18 ndo siku ya yai kupevuka).
Njia hii inawafaa zaidi wale wanawake ambao huwa wanajua siku ambazo mayai yanapevuka kwa sababu huwa wanapata maumivu kidogo ya upande wa kulia/kushoto wa tumbo('ovulatory pain'-si wanawake wote wanapata hii hali).
Ahsanteni sana. Nakaribisha maswali.
Kwanza,napenda tufahamu yafuatayo.
1. Ili njia hii iweze kuwa effective ni muhimu kwa mwanamke akawa na mzunguko ambao haubadiliki badiliki(regular menstrual cycle).
2. Njia hii ni less effective kwa wasichana walio chini ya miaka 25 na ambao bado hawajawahi kushika ujauzito kwa sababu wanawake hawa mara nyingi wanakuwa na very irregular menstrual cycles(mizunguko yao ya hedhi inabadilika badilika sana).
Sasa tuanze somo;kwa wanawake wenye mzunguko wa siku 28,siku ya kupevuka kwa yai ni siku ya 14,na yai baada ya kupevuka lina uwezo wa kuwa hai kwa wastani wa masaa 72;pia mbegu za kiume zinakuwa hai kwa wastani wa masaa 48-72. Lakini pia,yai linaweza kupevuka siku mbili kabla au baada(yaani siku ya 12-16). Kwa mahesabu hayo basi, siku za hatari ni kuanzia siku ya 9 mpaka ya 19;ndani ya siku hizi hutakiwi kufanya mapenzi bila kinga kama hutaki kushika mimba. So either usifanye mapenzi katika siku hizi au utumie kinga.
Kwa wale wanawake ambao mzunguko wao si wa siku 28,wao siku ya kupevuka yai wahesabu kwa kuchukua jumla ya siku za mzunguko wao kutoa 14(mfano kama mzunguko wako ni siku 32;chukua 32-14=18,kwa hiyo siku ya 18 ndo siku ya yai kupevuka).
Njia hii inawafaa zaidi wale wanawake ambao huwa wanajua siku ambazo mayai yanapevuka kwa sababu huwa wanapata maumivu kidogo ya upande wa kulia/kushoto wa tumbo('ovulatory pain'-si wanawake wote wanapata hii hali).
Ahsanteni sana. Nakaribisha maswali.