Jinsi ya kupika bajia

Jinsi ya kupika bajia

Ledisia

Member
Joined
Mar 6, 2013
Posts
10
Reaction score
0
ndugu zangu napenda sana bajia ila cjui kuzipika tafadhali mwenye ujuzi nazo
 
kuna bagia za dengu na za kunde wewe wapenda zipi?
 
Mimi pia ni mpenzi wa hizo bagia ila kwa kuzitengeneza mwenyewe si kwa kuzinunua mtaani au kula hotel coz maandaliz yake sijui wanafanyaje zinakuwaga na mchanga sana.Karibu!!!!
Bajia Za Kunde

Bajia%20Za%20Kunde.jpg



VIPIMO


Kunde za kupaaza 1 ½ Vikombe (hizi kunde kwetu tunaziita (njoombo)


Vitungu vya kijani iliyokatwa katwa ½ Kikombe


Baking soda ¼ Kijiko cha chai



*Bizari mchanganyiko 1 Kijiko cha chai



Maziwa 2 Vijiko vya supu



Chumvi 1 ¼ Vijiko vya chai



Unga wa ngano 2 Vijiko vya supu



Mafuta ya kukaangia


* Unaweza kutumia bizari ya pilau (cummin) ukipenda

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA



  1. Osha na kuroweka kunde kwenye bakuli la maji ya baridi usiku mpaka asubuhi.
  2. Saga kwenye mashine (food processor) kisha mimina kwenye bakuli.
  3. Ongeza vitungu, baking soda, masala, maziwa, na chumvi.
  4. Koroga vizuri halafu tia unga kisha uchanganye pamoja.
  5. Fanya vidonge kama nchi moja kisha ukipenda bana katikati ya mikono na kidole katikati ya bajia.
  6. Kaanga kwenye mafuta ya moto mpaka ziive.
  7. Andaa bajia kwenye sahani na chatini uipendayo.

Kwa hapo unaweza kuserve kwa chai, maziwa,juice au chochote unachopenda wewe!! Niliwahi kupost ila nimeshindwa kukutupia ili uone, sasa nimeamua kucopy na kupaste best.
 
Back
Top Bottom