Jinsi ya kutumia simu yako kama 'Remote Control'

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001

Itumie simu yako ya Android kama rimoti ya TV​



Hivi unafahamu kuwa unaweza kuitumia simu yako ya Android kama rimoti (Remote Control) kwenye kifaa cha kielektoroniki chochote kile kitumiacho rimoti?

Kuna aina nyingi sana za TV, AC au DVR kwenye matumizi yetu ya kila siku ambayo hutumia rimoti. Mara nyingi imekuwa vigumu sana kupata rimoti nyingine ya kifaa chako pale kile cha awali kinapopotea au kuharibika.

Kutokana na uvumbuzi zaidi, sasa unaweza kuitumia simu yako ya Android kutatua janga hili pale linapokufika.

Unachotakiwa kufanya ni kupakua App ya IR Universal Remote + WIFI kutoka kwenye Google Play hadi katika simu yako na kisha itakupa maelekezo ya namna ya kuiseti na kifaa cha kilektrokini chochote kile kinachotumia rimoti na hivyo kutatua maswahibu yako.
 
Wifi kwenye google play hapo sijaelewa
Nieleweshe vizuri.
Nna TCL smart tv remote imeharibika
 
Mbula: Bado kidogo watazindua ya kuongeza mapigo ya moyo yende au kupungua speed
 
Maelezo basi
 
Hiyo App Nitaidownload Lakini

Nikiwa Naondoka Na Rimoti Ya Home Naenda Nayo Bar Kutazama Mpira, Tv Ya Bar Na Ya Home Zinafanana Basi Nikawa Natumia Ile Rimoti Kuwakera Tu

,Mara Nizime Tv,

Mara Nipunguze Sauti!

Wakiwasha Mi Nazima

, Nimejikausha Ninaiminya Pasi Kuonekana,

Wanahangaika Kucheki Waya Gani Uko Loose😁

Hiyo Sana Sana Nafanyaga Nikiona Nishatoa Jero Yangu Kucheck Mpila Alafu Timu Ninayoishabikia Ishafungwa .

Nyieeee !!!!! 😂😂😂
 
aisee utakua upungufu wa akili huu
 
hakuna kitu kama icho
 
Unacopy na kupaste makala bila kufanya utafiti kuwa hilo jambo linawezekana au la
 
Kama sina kifaa kinachotumia remote nifanyaje?😂
 
Sio kila simu. Ni lazima iwe simu yenye IR blaster ndio itakubali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…