Leo nimemkumbuka sana aliyekua gwiji wa elimu ya unajimu A. Mashariki na kati Hayati Shekhe Yahaha Hussein ambaye katika uhai wake alishawahi kuzungumzia habari ya mahusiano ya herifu ya mwanzo katika jina na mafanikio ya kimaisha. Katika kiswahili na kingereza kuna herufi 26 lakini alizitaja herufi kuu 12 ambazo zina mahusiano na mafanikio endapo tu herufi hizo zitakaa mwanzoni mwa jina, herufu zenyewe ni A, B, F, J, K, L, M, N, O, R, S na W.
Alitoa mifano ya watu wengi duniani ambao herufu za mwanzo za majina yao (lazima yawe mawili au kuendelea na si moja) zinaanza na herufi moja yao kati ya hizo. Eg,
1. Jakaya Mrisho Kikwete (J, K na M)
2. Julius Kambarage Nyerere (J, K na N)
3. Ally Hassan Mwinyi (A na M)
4. Abeid Amani Karume (A, A na K)
5. Benjamin William Mkapa (B, W na M)
6. Rashid Mfaume Kawawa (R, M na K)
7. Wilbrod Peter Slaa (W na S)
8. Freeman Alkael Mbowe (F, A na M)
9. Abraham Lincolin (A na L)
10. John Kennedy (J na K)
11. Juma Kassim Nature (J, K na N)
12. Juma Kasseja (J na K)
13. Nancy Sumari (N na S)
14. Wema Sepetu (W na S)
15. Raila Odina (R na O)
16. Reginald Mengi (R na M)
17. Robert Mugabe (R na M)
18. Steven Kanumba (S na K)
19. Nape Moses Nnauye (N na M)
20. Barack Obama (B na O)
Embu tumuenzi kwa kuongeza idadi ya majina ya watu wenye mafanikio ama maarufu kwa kutumia ukokotozi huu wa herufi.