Elections 2010 JK alitarajia kutesa kiulaini chaguzi hii sasa apigwa na butwaa...

Elections 2010 JK alitarajia kutesa kiulaini chaguzi hii sasa apigwa na butwaa...

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Jk akitegemea historia kujirudia yenyewe alitarajia awamu ya pili itakuwa mteremko lakini siasa huwa hazitabiriki kabisa.

Kinyume na matarajio yake amekutana na ghadhabu ya wapigakura wenye kiu ya kupata kiongozi makini sifa ambayo bahati mbaya sana hana..

JK anafikiri uongozi ni kutukenulia meno yake ya bandia yaani "veneer teeth" lakini wapigakura wamemwonyesha ya kuwa uongozi si swala la sura ila ni la kuwa na uwezo wa kuwatumikia wananchi kwa unyenyekevu usio na mipaka...

Sasa JK amepigwa na butwaa na hata ahadi zake lukuki wapigakura hawana imani nazo na swali wanalojiuliza ni kuwa ni kitu gani atakifanya ambacho miaka mitano iliyopita hakukifanya?

Ni nini kilimzuia hayo yote anayoyaahidi sasa kutoyafanya hata theluthi moja kipindi chake cha kwanza.........

JK yupo kimya juu ya vita vya ufisadi na misamaha ya kodi kutoka kwa wakubwa sasa hizo fedha atazitoa wapi?

JK anawategema wamarekani ndiyo kutuletea maendeleo kweli hio ni sahihi? Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe wafadhili kazi yao ni kuongeza chachu tu na wla siyo vinginevyo................

JK hayupo tayari kuongelea ahadi zake zitaligharimu taifa kiasi gani ili kuona ya kuwa kweli yuko makini na anachoongea.................Ukweli ni kuwa anajitamkia tu ili kuwarubuni wapigakura tu................

Safari hii, JK atawafahamu watanzania kuwa siyo watu wa kuwachezea chezea kama watoto wadogo na kututishia na JWTZ amechochea petroli kwenye chaguzi hii... Vitisho vya JWTZ kamwe havitaweza hata siku moja kutumika kutuchagulia kiongozi tusiyemhitaji................

Hamu ya wapigakura kumfunza adabu inaongezeka siku hadi siku na katika kipindi cha wiki mbili tutatoa hitimisho lake bila huruma hata chembe.............
 
Worse enough ameshindwa kabisa kujitransform na kuwa JK wa 2010. He's still in 2005 mode. Na anazidi kushangaa kila kukicha. Bado anafikiria the handsome card, or else "nyota yangu inang'aa".

The guy is a big joke!
 
Jk akitegemea historia kujirudia yenyewe alitarajia awamu ya pili itakuwa mteremko lakini siasa huwa hazitabiriki kabisa.

Kinyume na matarajio yake amekutana na ghadhabu ya wapigakura wenye kiu ya kupata kiongozi makini sifa ambayo bahati mbaya sana hana..

JK anafikiri uongozi ni kutukenulia meno yake ya bandia yaani "veneer teeth" lakini wapigakura wamemwonyesha ya kuwa uongozi si swala la sura ila ni la kuwa na uwezo wa kuwatumikia wananchi kwa unyenyekevu usio na mipaka...

Sasa JK amepigwa na butwaa na hata ahadi zake lukuki wapigakura hawana imani nazo na swali wanalojiuliza ni kuwa ni kitu gani atakifanya ambacho miaka mitano iliyopita hakukifanya?

Hamu ya wapigakura kumfunza adabu inaongezeka siku hadi siku na katika kipindi cha wiki mbili tutatoa hitimisho lake bila huruma hata chembe.............

Mkuu sio haraka hivyo, joto lililopo sasa bado halitoshi kuivisha chakula, utawashangaa saana wapiga kura wa Tanzania pale matokeo ya vituo yatakapoanza kutolewa.
 
Mkuu sio haraka hivyo, joto lililopo sasa bado halitoshi kuivisha chakula, utawashangaa saana wapiga kura wa Tanzania pale matokeo ya vituo yatakapoanza kutolewa.

Nimekusoma!!!!??? wonder shall never end in Tanzania.
 
Mkuu sio haraka hivyo, joto lililopo sasa bado halitoshi kuivisha chakula, utawashangaa saana wapiga kura wa Tanzania pale matokeo ya vituo yatakapoanza kutolewa.

Hakuna mkuu hii ngoma tayali imewiva! Jk kinamnukia tuu mwaka huu labda atumie mabavu!!
eeeti anaahidi kujenga machinga complex zingine wakati hii iliyopo inaufisadi na haina jita kabisa! anasema atakuwa makini watu wasiuziane vyumba, alikuwa wapi mpaka wakauziana!??? Nonsense!
 
hAYA NI MATOKEO YA KUTEGEMEA NGUVU ZA MAJINI.YAMEDHIBITIWA NA WAPENDA MABADILIKO
 
Hakuna mkuu hii ngoma tayali imewiva! Jk kinamnukia tuu mwaka huu labda atumie mabavu!!
eeeti anaahidi kujenga machinga complex zingine wakati hii iliyopo inaufisadi na haina jita kabisa! anasema atakuwa makini watu wasiuziane vyumba, alikuwa wapi mpaka wakauziana!??? Nonsense!

nyumba zipi tena? mbona zote wameshauziana?
 
Mkuu sio haraka hivyo, joto lililopo sasa bado halitoshi kuivisha chakula, utawashangaa saana wapiga kura wa Tanzania pale matokeo ya vituo yatakapoanza kutolewa.
..........mshangao mwaka huu hautakuwepo kwa sababu inajulikana kuwa masanduku ya kura yatachezewa.
 
Hakuna mkuu hii ngoma tayali imewiva! Jk kinamnukia tuu mwaka huu labda atumie mabavu!!
eeeti anaahidi kujenga machinga complex zingine wakati hii iliyopo inaufisadi na haina jita kabisa! anasema atakuwa makini watu wasiuziane vyumba, alikuwa wapi mpaka wakauziana!??? Nonsense!
Huyu mtu mimi hata simuelewi. The fact kwamba kuna wamachinga ni tatizo. Wamachinga ni productive force wasted. Solution ni kuwafanya hawa wawe productive na walipa kodi wazuri.
 
Namshauri huyu Mr Misifa Kikwete abwage manyanga mapema au la nguvu ya umma itafanya kazi yake tar 31 Oct.
 
..........mshangao mwaka huu hautakuwepo kwa sababu inajulikana kuwa masanduku ya kura yatachezewa
Katavi!wizi wa kura ni jambo la hatari,usifikiri ni jambo la kuzungumza kiutani tu!madhara yake ni makubwa sana!Let us play our part as well wishers of this country and await NEC to play its part!
 
Hakuna mkuu hii ngoma tayali imewiva! Jk kinamnukia tuu mwaka huu labda atumie mabavu!!
eeeti anaahidi kujenga machinga complex zingine wakati hii iliyopo inaufisadi na haina jita kabisa! anasema atakuwa makini watu wasiuziane vyumba, alikuwa wapi mpaka wakauziana!??? Nonsense!
kama wachina wameshatoa msaada wa kujenga machinga complex, raisi yoyote ajaye atakamilisha, sio lazima ajenge yeye akiwa madarakani.
 
Mimi nasubiri nione Kigoma itakavyokuwa kama Dubai na Mwanza kama Carlfornia
 
Anaweza sema Dar kama Newyork. But how? The man has got no vision. Let us be serious, vote for changes, VOTE FOR DR. SLAA
 
Aaaaah,me nataka mabadiliko natamani watu wafungue macho yao waone wanavo danganywa
 
jk akitegemea historia kujirudia yenyewe alitarajia awamu ya pili itakuwa mteremko lakini siasa huwa hazitabiriki kabisa.

Kinyume na matarajio yake amekutana na ghadhabu ya wapigakura wenye kiu ya kupata kiongozi makini sifa ambayo bahati mbaya sana hana..

Jk anafikiri uongozi ni kutukenulia meno yake ya bandia yaani "veneer teeth" lakini wapigakura wamemwonyesha ya kuwa uongozi si swala la sura ila ni la kuwa na uwezo wa kuwatumikia wananchi kwa unyenyekevu usio na mipaka...

Sasa jk amepigwa na butwaa na hata ahadi zake lukuki wapigakura hawana imani nazo na swali wanalojiuliza ni kuwa ni kitu gani atakifanya ambacho miaka mitano iliyopita hakukifanya?

Ni nini kilimzuia hayo yote anayoyaahidi sasa kutoyafanya hata theluthi moja kipindi chake cha kwanza.........

Jk yupo kimya juu ya vita vya ufisadi na misamaha ya kodi kutoka kwa wakubwa sasa hizo fedha atazitoa wapi?

Jk anawategema wamarekani ndiyo kutuletea maendeleo kweli hio ni sahihi? Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe wafadhili kazi yao ni kuongeza chachu tu na wla siyo vinginevyo................

Jk hayupo tayari kuongelea ahadi zake zitaligharimu taifa kiasi gani ili kuona ya kuwa kweli yuko makini na anachoongea.................ukweli ni kuwa anajitamkia tu ili kuwarubuni wapigakura tu................

Safari hii, jk atawafahamu watanzania kuwa siyo watu wa kuwachezea chezea kama watoto wadogo na kututishia na jwtz amechochea petroli kwenye chaguzi hii... Vitisho vya jwtz kamwe havitaweza hata siku moja kutumika kutuchagulia kiongozi tusiyemhitaji................

Hamu ya wapigakura kumfunza adabu inaongezeka siku hadi siku na katika kipindi cha wiki mbili tutatoa hitimisho lake bila huruma hata chembe.............

pole sana uliyosema yote ni kinyume chake teh teh teh
 
Mkuu sio haraka hivyo, joto lililopo sasa bado halitoshi kuivisha chakula, utawashangaa saana wapiga kura wa Tanzania pale matokeo ya vituo yatakapoanza kutolewa.

.
Mkuu napingana na wewe kwa hili kwani maneno haya ya mda bado yamekuwa yakitumiwa na wanapropaganda wa ccm. Kwa kila jambo kuna wakati na wakati wa kuipa ccm talaka ni huu. Sii tu kwamba joto la mageuzi nchini halitoshi kuivisha chakula ni kwamba limepanda kupitiliza hata kuunguza chakula. Na kadri siku zinavyosonga ndivyo joto linapanda kwa kas zaidi.
 
Jana katufunga kamba kwamba atajenga reli toka Tegeta hadi Ubungo. Na kueleza eti ujenzi wa njia ya mabasi yaendayo kasi umeanza kwa msaada wa World Bank??!! Wadau (pengine mimi tu sijui) hivi ni sehemu gani hapa DSM ulipoanzia huo ujenzi ili niakajionee mwenyewe
 
Ndugu zangu safari hii mtu hachomoi. Safari imeiva, tunawaomba wazee wetu wana diplomasia kina mzee Salimu A Salimu, Mzee Malichela, Mzee Ruksa wasimamie haki ya Watanzania isichezewe maana mwanzo wa moto ni cheche. Kura zetu zisiibiwe jamani, kuwe na uwazi, haki na ukweli. Maana hatuna imani na watu wenye nyuso zilizo kakamaa na bila soni kwa wizi wa kimacho macho bila haya na kutetea vile vile hao wezi sugu. Hawa watu ni wakati muafaka wa kuwagalagaza. Naongeza wazo muhimu saana JAMANI EEHE POPOTE MLIPO TUOMBE TUPATE KATIBA MPYA ITAKAYO KIZI MATAKWA JAMII YA WATAWALIWA NA WATAWALA YENYE MISINGI YA DEMOKRASIA NA UTU. HILO NI MUHIMU SAANA KWA UKOMBOZI KAMILI WA WATANZANIA. TUSIZUBAE WACHA WAWEWESEKE LETU NI MOJA NI KUTOA HUKUMU YA HAKI TAR 31/10/2010. TANZANIA NI YETU SISI WATANZANIA NA VIZAZI VYETU YATUBIDI TUWAJIBIKE KWA UKOMBOZI WA NCHI HII.
''What counts is not necessarily the size of the dog in the fight -it's the size of the fight in the dog.
Dwight Eisenhower"
 
Back
Top Bottom