JK jijengee heshima kwa kutengeneza katiba ya watu..huna cha kupoteza wapuuzie CCM!

JK jijengee heshima kwa kutengeneza katiba ya watu..huna cha kupoteza wapuuzie CCM!

Chaimaharage

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
211
Reaction score
78
Ni wazi kabisa wenzio CCM hawaitaki katiba mpya mchakato ambao uliuridhia. Waliamua kukuunga mkono kama mwenyekiti wao lakini mioyoni mwao hawaitaki kabisa kwa sababu wanajua katiba mpya ambayo itakuwa katiba ya watu ikimaanisha ushirikishwaji wao bila ubaguzi na kushirikisha mawazo yao itakuwa ndio kifo cha CCM wakati wao bado wanataka kula.

Kwa hiyo watauvuruga mchakato kwa kadri wawezavyo ilimradi mpaka tunafikia uchaguzi mwingine katiba mpya iwe bado kama tulivyo shuhudia majuzi Bungeni baadhi ya wabunge wa CCM katika michango yao wakisema uchaguzi ujao ukifanyika kwa kutumia katiba ya zamani itakuwa faida kwao. Kwa hiyo watanzania wenzangu muone kilicho nyuma ya pazia kufuatia vurugu hizi na kupuuziwa hukU. Sasa basi ndugu Jakaya umesemwa kwa mengi mabaya kiasi wengine kufikia kusema awamu hii yako inaisha na hawaoni cha maana kilicho fanyika.

Nakushauri kwa hili la katiba litakujengea heshima miaka 50 ijayo pengine hata kuwazidi watangulizi wako iwapo utatengeneza katiba ya watu. Hakika utaeshimika na kupendwa miaka yote na mabaya yote ya utawala wako yatasahaulika. Mchakato huu wewe pekee ndiye wa kuuokoa sababu kama nilivyo sema hapo juu wenzio hawaupendi na walikulaumu sana kuwasikiliza wapinzani.

Kwa kuwa utawala wako ndio unakwisha huna cha kupoteza, jijengee heshima achana nao, wewe wasikilize wananchi wanataka nini.
 
Kazi ya ccm ni kuvuruga mchakato wa katiba mpya kila wakipata nafasi, walianza kwenye mchakato wa kuwapata wajumbe wa mabaraza ya katiba, wakatengeneza maoni feki ya wanachama milioni mbili wa ccm kwa kujifungia pale lumumba badala ya kwenda kwa wanachama wao! Pia wamebariki juzi bungeni wajumbe wa bunge maalumu la katiba wateuliwe na mwenyekiti wa ccm taifa badala ya wananchi kuchagua wawakilishi wao! Watanzania wasitarajie jema kutoka ccm lihusulo katiba mpya, wapo kwa ajili ya kuharibu mchakato huo na si kuuboresha!
 
wewe kweli kimbweta. Naona sasa mnatafuta huruma ya Rais ambaye mara zote huwa mnamtangaza kuwa ni adui yenu
 
sio ccm tu ha chadema wanaisimamia katiba katika mlengo wa maslahi yao kisiasa.
lakini katiba ni kwa ajili ya taifa kwa ujumla.
 
CHADEMA ndo wanataka katiba isipatikane maana ni wao ndiyo wanazua kila kukicha ili mchakato huo usikamilike. safari hii wameongeza na maliberali wenzao CUF na safari hii wapo na Bendera Fuata Upepo (NCCR MAGEUZI)
 
sio ccm tu ha chadema wanaisimamia katiba katika mlengo wa maslahi yao kisiasa.
lakini katiba ni kwa ajili ya taifa kwa ujumla.

Sure Mkuu. kuna watu wanadhani kuwa katiba ya nchi inahusu masuala ya siasa tu. huu ni ukosefu mkubwa wa uelewa na bila shaka hizi zitakuwa akili za bavicha. katiba ya nchi ni zaidi ya siasa
 
JK kafanya mambo makubwa sana kwa sababu wewe unaona mwisho mlangoni kwenu hutayaona lakini pia katiba siyo kipao mbele kwa watanzani kipao mbele ni maji,barabara,afya,elimu bora nk kwani katiba mpya ikipatika baskeri zitakuwa hazipati pancha,mvua itanyesha kila siku,au katiba mpya ikiwatayari wanawake hawatazaa kwa uchungu tumia akili katiba itapatikana tena nzuri lakini siyo kipao mbele cha taifa bali ni kipao mbele cha chadema.
 
Sure Mkuu. kuna watu wanadhani kuwa katiba ya nchi inahusu masuala ya siasa tu. huu ni ukosefu mkubwa wa uelewa na bila shaka hizi zitakuwa akili za bavicha. katiba ya nchi ni zaidi ya siasa
Chadema wanadhani katiba mpya ikipatika mbowe atakuwa rais na migomba itamea hata bila ya mvua na wao hawtaumwa homa tena,
Ni wendawazimu kupigani katiba mpaka mnafanya fujo huku wakipuuza mambo ya msingi kama ya uchumi wa taifa hili.
 
Chadema wanadhani katiba mpya ikipatika mbowe atakuwa rais na migomba itamea hata bila ya mvua na wao hawtaumwa homa tena,
Ni wendawazimu kupigani katiba mpaka mnafanya fujo huku wakipuuza mambo ya msingi kama ya uchumi wa taifa hili.

Hahahaaaaa. Kwa akili hizi za Mbowe ndiyo awe Rais wa nchi! Hapo Mungu atatulaani kweli
 
Ni kweli kuwa kama kuna kitu cha muhimu ambacho kitakuwa ni legacy ya JK ni kutengeneza Katiba mpya. Historia aidha itamhukumu au kumsifu kwa hilo. Ingelikuwa mimi, ningeweka uccm pembeni na kutengeneza Katiba ambayo haiwezi kuwa na sababu za kuirekebishwa kwa miaka 50 ijayo!
 
Chadema wanadhani katiba mpya ikipatika mbowe atakuwa rais na migomba itamea hata bila ya mvua na wao hawtaumwa homa tena,
Ni wendawazimu kupigani katiba mpaka mnafanya fujo huku wakipuuza mambo ya msingi kama ya uchumi wa taifa hili.

Mavi na mkojo vikichanganywa kwa wakati mmoja
 
Poleni Chadema, Maji ya Pua yamewafika, mnakimbilia Life Jacket linaitwa Jakaya
 
Swala la Katiba ni la kizalendo sidhani kama ni sahihi kuweka mbele ushabiki! hujui unachoshabikia utaendelea kutumika kama ndomu mpaka lini?
usiposhtuka sasa wajukuu zako watakulaumu
wewe kweli kimbweta. Naona sasa mnatafuta huruma ya Rais ambaye mara zote huwa mnamtangaza kuwa ni adui yenu

CHADEMA ndo wanataka katiba isipatikane maana ni wao ndiyo wanazua kila kukicha ili mchakato huo usikamilike. safari hii wameongeza na maliberali wenzao CUF na safari hii wapo na Bendera Fuata Upepo (NCCR MAGEUZI)

Sure Mkuu. kuna watu wanadhani kuwa katiba ya nchi inahusu masuala ya siasa tu. huu ni ukosefu mkubwa wa uelewa na bila shaka hizi zitakuwa akili za bavicha. katiba ya nchi ni zaidi ya siasa

Hahahaaaaa. Kwa akili hizi za Mbowe ndiyo awe Rais wa nchi! Hapo Mungu atatulaani kweli
 
Tatizo kubwa watanzania ni lack of education mleta mada kaongea vizuri sana na point za msingi wewe msomaji kama hujapenda basi change the chanel katiba sio ya ccm wala chadema ni ya watanzania wote kwahiyo tuwache ushabiki kwenye mambo ya msingi huu ushauri mzuri sana Rais niwakati wake wakufanya mabadiliko na watu waje kumkumbuka badae hata miaka 50 ijayo katiba hii mpya italenda maendeleo ya nchi na itaweza kuweka misingi mzuri ya sheria zitakazo wabana wala rushwa na mafisadi na watu wa sembe sasa wewe mchangiyaje unaleta mambo yako ya simba na yangu
 
Jk kafanya mambo makubwa sana kwa sababu wewe unaona mwisho mlangoni kwenu hutayaona lakini pia katiba siyo kipao mbele kwa watanzani kipao mbele ni maji,barabara,afya,elimu bora nk kwani katiba mpya ikipatika baskeri zitakuwa hazipati pancha,mvua itanyesha kila siku,au katiba mpya ikiwatayari wanawake hawatazaa kwa uchungu tumia akili katiba itapatikana tena nzuri lakini siyo kipao mbele cha taifa bali ni kipao mbele cha chadema.

Kama kuna mtanzania anae weza tumia computer/ internet na aka argue kama wewe basi kazi ipo. Kwamba hujui hayo uliyo yataja ndo katiba yenyewe........... hata kama ni ushabiki basi jenga hoja la sivo utaonekana mbulura hata mbele ya mkeo na wanao..........
 
Back
Top Bottom