JK Kuunguruma kesho

Status
Not open for further replies.

PM.. hili la huyu mama nalisikia mara nyingi hapa lakini hakuna mtu ambaye anaweka nyeti hasa ni zipi:

a. Inawezekana vipi mtu kama Salva (kumbuka niliandika makala kumhusu yeye) anaweza kufanya kazi Ikulu bila kuwa vetted?

b. Katika utaratibu huo wa kumvet itawezekana vipi kuwa wamuangalie yeye na isiwe mke wake?

c. Ni ushahidi gani uliopo wa huyu mama kujilipua kuwa yeye ni "mkimbizi" wa Burundi?

Tangu suala hili lilipowahi kuibuliwa huko nyuma na memba mwingine wa huko London nimelifuatilia pembeni na vyote ambavyo nimebahatika kuona ni kuwa huyu mama bado ni Mtanzania na ana pasi ya Tanzania. Kama una chembe yoyote nipenyezee..
 
waliosikia hotuba yake mtuambie kasemaje.


Naogopa asijekuwa kazungumza tena vijembe vya uchochoroni kuwa kelele za mlango hazimkoseshi yeye kupata usingizi,.
 
Bado hajazungumza nadhani itakuwa jioni maana hawakutoa muda hawa waswahili... unless kama ataibukia Bungeni maana ile Gulfstream...
 
Inakuwaje mkopaji wa kawaida katika bank atozwe riba lakini mwizi/fisadi arudishe hela bila riba?

Kwanza ukizingatia ukubwa wa hela yenyewe pamoja na muda waliokaa nayo, utaona kwamba riba peke yake inatosha kulipa wazee wetu wa EAC na WALIMU.
 
Mkuu BAK, hivi katika suala hili la EPA, baada ya uchunguzi wa Ernst & Young kulikuwa na haja ya kuvuta miguu kweli na kuitisha uchunguzi mwingine?


Mkuu,hiyo ni namna yakupoteza muda tu.Mbona watuhumiwa wengine huwekwa chini ya ulinzi wakisubiri uchunguzi ukamilike wafikishwe mahakamani? kwani hawavipi?
 
Pesa za EPA ni kisehemu kidogo tu cha mapesa yaliyokombwa BOT... Naona wamefanikiwa kuweka fix kwenye EPA pekee na watu wamesahau mabilioni mengine yaliyokombwa BoT.

Kazi kweli kweli

Hakutakuwa na jipya jamani hivi mpaka sasa hamjajua the real JK?Hivi hamjui kuwa licha ya kuzungukwa na mafisadi na yeye ni fisadi pia?Tuna mambo mengi sana ya kufanya bora niangalie MNET kuliko kumsikiliza mtu asiejali watu anaowaongoza!mtu asiekuwa serious when he need to be.Mtu wa mzaha mzaha na kupenda kuchekacheka hovyo!Mtu asie badilika kuendana na hali halisi ya wakati uliopo. JK huyu huyu yupo pale alipo kwa hizo pesa za EPA kisha manategemea nini kikubwa?Mnajua kuna watu wamegoma kurudisha hizo pesa kwa kuwa zilifanya kupitia tu kwenye accounts zao lakini zilitolewa na kutumiaka kwenye Kampeni! Na huyu bwana Maregesi anao ushahidi wa kishina cha cheque iliyoandikwa pesa kupelekwa CCM from his account. Mpaka hapo msitegemee kitu chochote kuhusu EPA sana sana atazungumzia mauaji ya maalbino na kuopiga siasa kwa sanaaa kama kawaida yake takwimu nyingiiiii sizizo pimika na uhalisia. Bila kusahau Hotuba nzuri na tamu iliyojaa maneno mengi ya kisiasa ambayo kila masaa yatakapo kuwa yakienda watu wataichambua na mwisho kuiona haikuwa na kitu chochote na mapungufu mengi mfano hotuba yake ya mwisho Bungeni.

Na tungoje tuone.
 
Mmeanza kuukana uaraia wenu taratibu?

Uswahili si uraia bwan kaka. Unajua maana ya Swahili na lilipotokea neno hilo?neno hilo ni neno la kairabu "sahel" kiwa na maana "around the coast" nadhani unawajua watu wa "coast" mfano JK ni Mswahili wa Bagamoyo. Mimi siwezi kuwa Mswahili kwani natokea bara mikoa ya katikati ya Tanzania. Ila mimi ni Mtanzania!Huo ndio uraia wangu.

Na nadhani mtu akisema mswahili ana amanisha tabia hasa za hawa jamaa zetu waswahili "watu wa pwani" umwinyi wao na ajizi kwenye mambo muhimu ndio maana ukiwa na miadi na mswahili "mwinyi" lazima ugande maana atajivutavuta wee huku time nayo ikikimbia maana time huwa haimgoji mtu.

Uswahili si Uafrika wala Utanzania back to School Kite Munganga. Tena wewe jina lako linaonyesha si mswahili ila unataka kujilipua kama mke wake salva!
 

Uswahili si Uafrika wala Utanzania back to School Kite Munganga. Tena wewe jina lako linaonyesha si mswahili ila unataka kujilipua kama mke wake salva!

Kwi kwi kwi kwi... tehe tehe tehe tehe... msifike huko wakuu
 
Siju ni kwa nini huyu jamaa huwa anatupotezea muda wetu. Bora hata akikaa kimya anaonekana ana akili kuliko akizungumza.
 

Mzee Mwanakijiji,

Huyu mama alikuwa Luton kama mkimbizi labda kama awe ameondoka sasa. Salva mwenyewe alikuwa mwendaji mzuri wa Luton. Naamini anajua vizuri kwamba mkewe kajilipua hapo.

Kwa Tanzania huenda vetting wanayofanya ni juu ya mhusika mwenyewe na wala sio wake/waume zao.

Kuna uwezekano pia huyo mama ni Mtanzania ila alijilipua kama Watanzania wengine wengi kwa faida ya familia zao. Mimi simhukumu mtu kwa hili. Kila mtu anayeishi nje amekuja kwa malengo yake. Kuna wengine wamepitia njia rahisi kama shule na kazi lakini wengine hawakuwa na nafasi hiyo ya kuajiriwa kwenye kazi ambazo zingewapatia work permit na hivyo kulazimika kutumia ukimbizi.

Siasa zetu mbaya na umaskini unawafanya watu wachukue maamuzi ya ajabu.
 


Wacha dharau wewe -kama unafahamu nini maana ya huo U-Tanzania unaojivuia. Hauwezi kuwa na U-Tanzania bila ya kuwemo U-swahili (zaidi ya asilimia 50). Kwa maana watu wa Zanzibar ambao wanafanya iwepo Tanzania unayoringia wote ni Waswahili. Usitukane wakunga na uzazi ungalipo. Sawa?
 
Jk anaguruma sasa hivi. ....sio live. Inarekodiwa baadaye mtarushiwa
 
Mheshimiwa Rais umeshaongea na WAAFRIKA kwenye bunge la Africa kule South Africa leo nakuomba[nipo chini ya miguu yako]ongelea mambo ya Tanzania tu hata ya EAC hatuyataki.Najua zaidi ya nusu ya hotuba yako itakua inahusu mambo ya nje ya mipaka yetu na hii itakupotezea wale wachache ambao bado wana imani nawe[mi ulinipoteza zamaaani].
 
Mzee Mwanakijiji,

Huyu mama alikuwa Luton kama mkimbizi labda kama awe ameondoka sasa. Salva mwenyewe alikuwa mwendaji mzuri wa Luton. Naamini anajua vizuri kwamba mkewe kajilipua hapo.

Nimelisikia hilo kuwa alikuwa Luton kama "Mkimbizi". Hakuna ushahidi wa hilo. Hakuna mahali popote ambapo amejiandikisha kuwa ni mkimbizi na passport yake bado ni ya Tanzania. Alijiupua lini na wapi?

Kwa Tanzania huenda vetting wanayofanya ni juu ya mhusika mwenyewe na wala sio wake/waume zao.

Hapana wanafanya yote mawili, kama hawafanyi basi tuna tatizo kubwa zaidi kuliko tunavyoweza kufikiria.

Kuna uwezekano pia huyo mama ni Mtanzania ila alijilipua kama Watanzania wengine wengi kwa faida ya familia zao.

Lakini yeye mke wa mtu anayefanya kazi Ikulu kwa faida gani aliyo nayo Uingereza kuliko nafasi ambayo mumewe anayo sasa? Kwani huyo mama anafanya kazi gani kiasi cha kuamua kujilipua?


Nakupata vizuri, lakini kuna ushahidi gani kuwa huyo mama alijiandikisha kama mkimbizi? Maana hizo habari ni public record.

Siasa zetu mbaya na umaskini unawafanya watu wachukue maamuzi ya ajabu.

Hili ni kweli lakini kwa huyu mama sijui ukweli ni upi hasa kwa sababu sijaona rekodi yoyote kutoka Britisha Govt kuwa aliomba ukimbizi, naweza kuangalia wapi hiyo status yake ya ukimbizi?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…