JKCI yatoa ufafanuzi madai ya baadhi ya Watumishi wao kutoa huduma kwa kujuana

JKCI yatoa ufafanuzi madai ya baadhi ya Watumishi wao kutoa huduma kwa kujuana

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetoa ufafanuzi kuhusu hoja ya Mwanachama wa JamiiForums aliyetoa malalamiko yake kuhusu baadhi ya huduma za Watumishi wa hapo.

Kusoma zaidi alichoeleza Mdau bofya hapa ~ Tumepata huduma mbovu JKCI upande wa VIP, baadhi ya Watumishi wanahudumia Watu kwa kujuana

Mwanachama huyo alisema upande wa Idara ya V.I.P ya JKCI hawana mawasiliano mazuri na Wagonjwa, pia wanapoulizwa wanakuwa wakali na kutotoa majibu mazuri jambo ambalo anaona linaweza kusababisha matatizo baina ya pande mbili hizo.

UFAFANUZI WA JKCI
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa JKCI, Anna Nkinda anasema “Hakuna kujuana katika utoaji wa huduma zetu, zinatolewa kwa haki, Watumishi wetu wote wanatimiza majukumu yao inavyotakiwa.

“Huduma ya V.I.P ni nzuri na wastani tunaona Wagonjwa 40 kwa siku wa Idara hiyo, hata Wagonjwa wa kawaida wote wanapewa vipaumbele, hakuna huduma za kujuana.

“Mgonjwa akifika mapema anapata huduma mapema pia, hakuna usumbufu wanaopata kwa kuwa watu wetu wanajielewa, hakuna suala la upendeleo.

“Huduma inatolewa sawa kwa mtu yeyote, ukifika wanakihudumia kama wanakujua siku nyingi, watakupokea vizuri na utapata huduma nzuri.

“Ikitokea mtu amejisikia vibaya na yupo kwenye foleni anamwambia Nesi anapata huduma haraka.”
 
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa JKCI, Anna Nkinda anasema “Hakuna kujuana katika utoaji wa huduma zetu, zinatolewa kwa haki, Watumishi wetu wote wanatimiza majukumu yao inavyotakiwa.

“Huduma ya V.I.P ni nzuri na wastani tunaona Wagonjwa 40 kwa siku wa Idara hiyo, hata Wagonjwa wa kawaida wote wanapewa vipaumbele, hakuna huduma za kujuana.
Imejibiwa kisiasa, alitakiwa aje na facts zisizotia shaka
 
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetoa ufafanuzi kuhusu hoja ya Mwanachama wa JamiiForums aliyetoa malalamiko yake kuhusu baadhi ya huduma za Watumishi wa hapo.

Kusoma zaidi alichoeleza Mdau bofya hapa ~ Tumepata huduma mbovu JKCI upande wa VIP, baadhi ya Watumishi wanahudumia Watu kwa kujuana

Mwanachama huyo alisema upande wa Idara ya V.I.P ya JKCI hawana mawasiliano mazuri na Wagonjwa, pia wanapoulizwa wanakuwa wakali na kutotoa majibu mazuri jambo ambalo anaona linaweza kusababisha matatizo baina ya pande mbili hizo.

UFAFANUZI WA JKCI
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa JKCI, Anna Nkinda anasema “Hakuna kujuana katika utoaji wa huduma zetu, zinatolewa kwa haki, Watumishi wetu wote wanatimiza majukumu yao inavyotakiwa.

“Huduma ya V.I.P ni nzuri na wastani tunaona Wagonjwa 40 kwa siku wa Idara hiyo, hata Wagonjwa wa kawaida wote wanapewa vipaumbele, hakuna huduma za kujuana.

“Mgonjwa akifika mapema anapata huduma mapema pia, hakuna usumbufu wanaopata kwa kuwa watu wetu wanajielewa, hakuna suala la upendeleo.

“Huduma inatolewa sawa kwa mtu yeyote, ukifika wanakihudumia kama wanakujua siku nyingi, watakupokea vizuri na utapata huduma nzuri.

“Ikitokea mtu amejisikia vibaya na yupo kwenye foleni anamwambia Nesi anapata huduma haraka.”
Atutolee ujinga!! kwani asikubali kuwa huduma ni mbovu? na apokee malalamiko ,Kisha aseme atayafanyia kazi!
 
Yaani mtu kasema kabisa katoa hela ndio mambo yakaenda fasta fasta huyu anakanusha nn sasa badala ya kukubali hayo mapungufu na kuyafanyia kazi.
 
Nilitegemea mkuu wa JKCI aombe mawasiliano rasmi na mtoa malalamiko ili aweze kubotesha huduma hapo hospitali.
Nurse wengi ni wakorofi na huduma utolewa kwa kujuana hasa kwenye hospitali za serikali.
 
Nilitegemea mkuu wa JKCI aombe mawasiliano rasmi na mtoa malalamiko ili aweze kubotesha huduma hapo hospitali.
Nurse wengi ni wakorofi na huduma utolewa kwa kujuana hasa kwenye hospitali za serikali.
Tanzania Hilo Jambo sahau...
 
Asa ndio jibu gani hilo!

Ni bora wasingejibu kabisa.
 
tatizo wanaotoa maelezo ya ufafanuzi au kukanusha ni maboss na viongozi wa juu ambao wanakaa tu ofisini wakisoma mafaili na kusaini nyaraka..wakati wanaolalamikiwa ni wafanyakazi na watoa huduma..na hata hao watoa huduma wakiulizwa kuhusu kunyanyasa wateja hawawezi kukubali.. kama vp uongozi waweke kamera sehemu kama hizo za kupokelea wateja na reception pamoja na sheria kali za adhabu angalau inaweza kupunguza hizo shida
 
Amejibu kipumbavu sana,nadhani wangechunguza madai alafu ndo aje kuropokwa
 
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetoa ufafanuzi kuhusu hoja ya Mwanachama wa JamiiForums aliyetoa malalamiko yake kuhusu baadhi ya huduma za Watumishi wa hapo.

Kusoma zaidi alichoeleza Mdau bofya hapa ~ Tumepata huduma mbovu JKCI upande wa VIP, baadhi ya Watumishi wanahudumia Watu kwa kujuana

Mwanachama huyo alisema upande wa Idara ya V.I.P ya JKCI hawana mawasiliano mazuri na Wagonjwa, pia wanapoulizwa wanakuwa wakali na kutotoa majibu mazuri jambo ambalo anaona linaweza kusababisha matatizo baina ya pande mbili hizo.

UFAFANUZI WA JKCI
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa JKCI, Anna Nkinda anasema “Hakuna kujuana katika utoaji wa huduma zetu, zinatolewa kwa haki, Watumishi wetu wote wanatimiza majukumu yao inavyotakiwa.

“Huduma ya V.I.P ni nzuri na wastani tunaona Wagonjwa 40 kwa siku wa Idara hiyo, hata Wagonjwa wa kawaida wote wanapewa vipaumbele, hakuna huduma za kujuana.

“Mgonjwa akifika mapema anapata huduma mapema pia, hakuna usumbufu wanaopata kwa kuwa watu wetu wanajielewa, hakuna suala la upendeleo.

“Huduma inatolewa sawa kwa mtu yeyote, ukifika wanakihudumia kama wanakujua siku nyingi, watakupokea vizuri na utapata huduma nzuri.

“Ikitokea mtu amejisikia vibaya na yupo kwenye foleni anamwambia Nesi anapata huduma haraka.”
Anything with Kikwete on it hakina baraka, ni kukipotezea tu.
 
Back
Top Bottom