JKT baada ya form 6 ?

mohammad_othar

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
247
Reaction score
42
Inakuaje kwamba nimeambiwa na jamaa kwamba usipoenda Jkt baada ya kumaliza 6 huwezi pata chuo so watakibania vp? Maana application ni through tcu inamaana kwamba tcu wataangalia walopita jkt au ni inakuaje naomba nielezwe?
 
Acha ubishi nenda JKT, Kwani uliambiwa kuwa TCU ndio watakufanyia usajili wa Chuo au unaomba chuo kupitia TCU?. Pia wanaweza kuweka kikwazo kuwa ili uajiliwe lazima uwe ulipitia JKT hapo utafanyaje?
 
kaka kuna condition serkal imetoa kwavyuo vkuu kuwa lazma wanafnz wakguliwe vyet vya jesh ndo wapewe udahili.source VC UDSM.Kongamano la elim na uzalendo la tarh 28-6-2013 nkurumah hall udsm.
 
kaka kuna condition serkal imetoa kwavyuo vkuu kuwa lazma wanafnz wakguliwe vyet vya jesh ndo wapewe udahili.source VC UDSM.Kongamano la elim na uzalendo la tarh 28-6-2013 nkurumah hall udsm.

kakaa nimeikubal source yako(nukuu yako)
 
Inakuaje kwamba nimeambiwa na jamaa kwamba usipoenda Jkt baada ya kumaliza 6 huwezi pata chuo so watakibania vp? Maana application ni through tcu inamaana kwamba tcu wataangalia walopita jkt au ni inakuaje naomba nielezwe?

Usibebwe na upepo mdogo wa wavivu wa kufuatilia mambo. hakuna uhusiano wa kwenda jkt na sifa za kwenda chuo kikuu. kwanza unapaswa kujua kuwa wanaokwenda jkt ni wale tu ambao ni school candidates tena kutoka shule chache za serikali na ambao wamepata daraja la kwanza hadi la pili kwa masomo ya arts na daraja la kwanza hadi la tatu kwa masomo ya sayansi.

Kumbuka ili kujiunga chuo kikuu ni lazima uwe na principle mbili, hivyo hadi mtu wa arts mwenye daraja la tatu ambaye hana sifa ya kwenda jkt kwa sasa anaweza kuchaguliwa chuo kikuu. pia chuo kikuu huchukua hata wahitimu ambao ni privite candidates na hata wale wa miaka ya nyuma ikiwa ni pamoja na wa stashahada.

Ikiwa umepata nafasi ya kuchaguliwa kwenda jkt ni vema ukaenda kwani ni uzalendo na kuongeza wasifu wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…