JKT Tanzania, TAKUKURU na Bodi ya Ligi ichunguze bank account na kumhoji mchezaji Mohamed Bakari

MwananchiOG

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2023
Posts
1,970
Reaction score
4,037

Winga Mohamed Bakari aliingia dk66 kuchukua nafasi ya Shiza Kichuya, dk77 alioneshwa kadi ya njano ya kizembe ambayo inashangaza na kama haitoshi dk90+3 akafanya uzembe kwa kumvuta Shomari Kapombe ambaye hakuwa na mpira wala hatari yoyote, jambo lililopelekea penati na timu yake kufungwa. Ni kama aliitaka kadi nyekundu, na alikuwa akicheza kwa maagizo maalum. JKT Tanzania chukueni hatua dhidi ya mchezaji huyu na bodi ya ligi ichunguze tuhuma hizi za upangaji matokeo.

Inafikirisha sana! Vitendo hivi ni aibu!
 
Si vizuri kukatisha Wachezaji Vijana tamaa. Alikuwa na siku mbaya kazi Kwa matukio 2 lakini si Kwa makusudi. Kichuya Mechi ilimshinda tangu dakika ya 1 hivyo sub ilikuwa sahihi.
 
Naona Bado maumivu yanaendelea..kunywa maji mengi
 
Nafikiri mngeanza kuchunguza account ya Komeni na Baca kwa ile kadi ya Azam
 
Wachezaji wengi wa hapa bongo ni malimbukeni sana halafu utakuta mtu anawatetea eti wachezaji wakigeni wanapewa kipaumbele wapo wachezaji wanaojitambua tungeendelea kuwategemea hawa wakibongo ligi yetu isingefika hapa
 
Nafikiri mngeanza kuchunguza account ya Komeni na Baca kwa ile kadi ya Azam
Zile zinaelezeka na zinaonekana wazi kwamba uchovu ulikuwa ukiwatesa wachezaji, hata na hivyo Bacca hakucheza faul zenye kutia mashaka.
 
Wachezaji wengi wa hapa bongo ni malimbukeni sana halafu utakuta mtu anawatetea eti wachezaji wakigeni wanapewa kipaumbele wapo wachezaji wanaojitambua tungeendelea kuwategemea hawa wakibongo ligi yetu isingefika hapa
Shida yao kubwa ni Njaa! Huyo unaweza kuta amepewa Laki tano tu, Timu imepambana dakika zote anakuja kuigharimu timu kizembe kabisa!
 
Nashukuru mmekuja kukiri kuwa ilikuwa penati halali. Halafu kuna yule aliunawa mpira na nadhani refa aliita penati kwa sababu yake na si huyu mnayemtuhumu.
 
Zile zinaelezeka na zinaonekana wazi kwamba uchovu ulikuwa ukiwatesa wachezaji, hata na hivyo Bacca hakucheza faul zenye kutia mashaka.
TAKUKURU WAMCHUNGUZE IBRAHIMU BAKA INAWEZEKANA ALIPEWA MLUNGULA NA AZAM.
 
Reactions: K11
Shida yao kubwa ni Njaa! Huyo unaweza kuta amepewa Laki tano tu, Timu imepambana dakika zote anakuja kuigharimu timu kizembe kabisa!
HATA IBRAHIMU BAKA NI NJAA TU NA UNAWEZA KUTA ILE MECHI YA AZAM ALIYOPEWA KADI NYEKUNDU ALIPEWA LAKI TANO TU INABIDI TAKUKURU WACHUNGUZE AKAUNTI YAKE.
 
Siamini hilo, mchezaji si computer, ya kuwa timamu kwa kila command. Utimamu wa mchezaji unategemea mambo mengi. Kama una ushahidi sawa, lakini kama ni hisia tu, humtendei haki huyo mchezaji.
 
Na refa aliye kubali goli hili la Bacca naye pia Takukuru wamtembelee
 

Attachments

  • FB_IMG_1735080127476.jpg
    71.1 KB · Views: 1
Reactions: BRN
Refa leo kapona??🤣
 
Ninyi ni nyuma kuna mwiko na ni jina mlilolichagua wenyewe kwa hiyari yenu.Hata ukijinunisha una mwiko nyuma.Chura utopolo wewe!
 
Reactions: BRN
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…