zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
Sasa ni rasmi; yule kinda mwenye kipaji kilichotukuka anayetazamiwa kuwa mmoja wa wachezaji bora kabisa duniani Joao Felix amekamilisha uhamisho wake kutoka klabu ya SL Benfica nchini ureno na Kutua klabu ya Atletico Madrid ya nchini Uhispania.
Dau la uhamisho linatajwa kuwa €130 Million ambalo litamfanya kuwa mchezaji wa tatu ghali zaidi katika historia ya mpira akiwa nyuma ya wachezaji wa PSG Kylian Mbappe aliyegharimu €180 Million na Neymar Jr aliyegharimu €222 Million.
Kinda huyo ana umri wa miaka 19 na aliwika zaidi msimu uliopita alipocheza mechi 26 Akifunga goli 15 na kutoa Assist za magoli 9. Toka ameanza kucheza mpira professional amecheza mechi 87 akifunga goli 34 na kutoa assist za magoli 17.
Mshambuliaji huyo ambaye hucheza kama Winger pia ana uwezo mkubwa wa kudribble na kuwachenga mabeki, spidi kubwa, nguvu ya kupiga shots za mbali,mbunifu, hivyo ukiweka na umri wake basi anaweza kuwa mchezaji bora zaidi misimu ijayo.
Anahamia Atletico ili kumrithi Antoine Griezmann anayehamia Barcelona wiki ijayo kwa dau la €120 Million hivyo kurudisha pesa iliyotumika kumleta huyu kinda ambaye alikua akiwaniwa na Man City,Real Madrid, Manchester United na Juventus pia
Kiufupi La liga inaenda kuwa moto msimu ujao ukitazamia hizi sajili za kufuru zinazofanyika.
Dau la uhamisho linatajwa kuwa €130 Million ambalo litamfanya kuwa mchezaji wa tatu ghali zaidi katika historia ya mpira akiwa nyuma ya wachezaji wa PSG Kylian Mbappe aliyegharimu €180 Million na Neymar Jr aliyegharimu €222 Million.
Kinda huyo ana umri wa miaka 19 na aliwika zaidi msimu uliopita alipocheza mechi 26 Akifunga goli 15 na kutoa Assist za magoli 9. Toka ameanza kucheza mpira professional amecheza mechi 87 akifunga goli 34 na kutoa assist za magoli 17.
Mshambuliaji huyo ambaye hucheza kama Winger pia ana uwezo mkubwa wa kudribble na kuwachenga mabeki, spidi kubwa, nguvu ya kupiga shots za mbali,mbunifu, hivyo ukiweka na umri wake basi anaweza kuwa mchezaji bora zaidi misimu ijayo.
Anahamia Atletico ili kumrithi Antoine Griezmann anayehamia Barcelona wiki ijayo kwa dau la €120 Million hivyo kurudisha pesa iliyotumika kumleta huyu kinda ambaye alikua akiwaniwa na Man City,Real Madrid, Manchester United na Juventus pia
Kiufupi La liga inaenda kuwa moto msimu ujao ukitazamia hizi sajili za kufuru zinazofanyika.