John Munisi Katibu wa Chadema wa Jimbo la Hai, aliyepewa kesi ya ubakaji Hai afanya Misa ya Shukrani

Kwanza hujaelewa mada , niliposema ni wa kwanza sina maana ni wa kwanza kuteswa , natambua kuna viroba vya maiti vilivyookotwa baharini , hawa hawana uwezo wa kufanya ibada ya shukrani , nilimaanisha ni wa kwanza kufanya misa ya kumshukuru Mungu , lingine uliloongopa ni mwaka ambao Sabaya aliteuliwa kuwa DC wa Hai
 
Wengi hao ni wapi? Ulifanya sensa ya hao watu ukajua wanatoka wapi?

Kuhusu nilichokisema niko sahihi. Mbowe aliliongea hili kwenye kikao huko kaskazini na ndio wanaolipigia chapuo.

Mwisho, mimi ni mzima sana tu.
Kwenye jukwaa hili ni sample ya watu tunaokutana nao kwenye maisha ya kila siku. Mathalani kwa miaka miwili sasa nipo Kanda ya Ziwa, siyo mchaga, sijawahi hata kuishi mikoa ya Kaskazini.

Mimi binafsi siwezi kufurahia kifo cha binadamu mwenzangu hata kama ni mwovu. Lakini nikuthibitishie, kuna wakati nilikuwa Kahama, nikashangaa watu wakifurahia kifo cha Mwendazake. Nikauliza ni kwa nini, nikaambiwa alifanya uporaji wa fedha za matajiri kwenye accounts zao, hasa wachimbaji na wafanyabiashara wa dhahabu. Hao siyo wachaga, wengi wao ni wasukuma. Mwanza, Shinyanga, Tabora, hali ni hiyo hiyo. Mbaya zaidi, baadhi ya wanaoonekana kufurahia, japo siyo kwa uwazi sasa, ni wateule wake ambao tulikuwa tukiamini walinufaika na utawala wake wa mkono wa chuma.

Tukiacha unafiki, marehemu hakuwa na sifa ya kuitwa kiongozi. Aliendesha nchi ovyo. Hakujua maana ya uongozi shirikishi, hakujua mbinu wala kanuni za uchumi wa kisasa, aliamini anaweza kufanikiwa kwa kuongoza nchi kwa ukatili, uwongo na ulaghai. Alitumia ukatili na nguvu zaidi kuliko akili, weledi na maarifa.

Kwa kipindi chote cha miaka ya uongozi wake, vigezo vyote vya ukuaji wa uchumi, demokrasia, utawala wa sheria na haki, vilishuka chini.

Ukuaji wa uchumi aliuangusha toka 7.4% mpaka 4.5%. Ukuaji wa utalii aliuangusha toka 15% mpaka 3.6%, ukuaji wa uwekezaji aliuangusha toka 28% mpaka 4%, mauzo ya mazao ya kilimo aliyaangusha kwa 50%. Pamoja na kuleta madhara hayo kwenye uchumi, bado utawala wake uligubikwa na udikteta wa hali ya juu - kuteka, kuua, kupototeza watu, kuwabambikia watu kesi za uhujumu uchumi, kupora pesa za watu kwenye account zao za benki. Kwa hakika ulikuwa utawala wa kishetani usiotegemewa kuwepo katika jamii ya watu waliostaarabika.

Tunamshukuru Mungu, alitupa nafasi ya kujifunza kitu kupitia kwenye utawala ule dhalimu. Kama hatukujifunza, kuna siku tutampata kiongpzi aliye mwovu zaidi.
 
Haitawezekana kwa Watanzania kumsamehe Mwendazake na kundi lake , haiwezekani na wala haitakuja kuwezekana
 
Umeandika ukweli mno !
 
Hebu fikirieni kidogo. Kuna uhusiano mkubwa sana kati elimu na mwamko wa kisiasa.
Hivi 20% ya waliopendekeza mfumo vyama vingi ambao Nyerere alikubaliana nao hamjui kuwa wengi walikuwa wasomi?
Kwa maana hiyo hata wale wanaounga mkono upinzani wengi wao ni wasomi pia.
Msomi anayeponda upinzani ni msomi mchumia tumbo tu.
Hii ina maana kuwa maeneo ambayo wasomi ni wengi kama mijini na maeneo ambo yalisonga mbele kielimu upinzani unajidhihirisha.
Elimu imefanya maeneo ambayo elimu ilijikita zaidi, mnayajua, kuwa na uelewa zaidi wa kisiasa na hatimae kuunga mkono mawazo mbadala, yaani siasa mbadala, upimnzani.
Hawa watu ambao elimu ni haba ni rahisi sana kusema kirahisi ndio mzee! Na wakijengewa dhana ya chuki dhidi ya wengine wanakubali tu kama mazuzu.
Tatizo la elimu na uelewa linatufanya tuburuzwe na walioshika madaraka na hivo pia ni tatizo linalochelewesha maendeleo.
Hata sasa ni wachache tu wenye mawazo chanya na yenye tija ambao wanazidiwa sana na wajinga ambao ndio mtaji unaotumiwa na wenye mamlaka.
Namuona Mama Samia kama kiongozi tofauti sana a mbaye anapuuza mtaji wa wajinga kutawala, ni kama Nyerere alipowapa nguvu 20% mfumo wa vyama vingi ukaingia
Samia atatuvusha!
 
Fact check.

Kuhusu uchumi, umeongea uongo mwingi na hii inanipa sababu ya ku disqualify hoja zako zote. Bank ya Dunia wenyewe wanakiri uchumi wa Tanzania uliporomoka mwaka jana kutoka wastani wa 7% hadi 4.5% kwa sababu ha covid na sio kwa sababu ya sera za uchumi.

Kwa sababu hiyo tu inanifanya ni conclude kua yote uliyoyasema ni ya uongo.

Jaribu kuja na hoja zinazokaribiana na ukweli basi.
 

Hawawezi kukuelewa hawa wahuni.
 
Una uwezo mdogo sana ! Ulifikaje JF ?
We nijibu kwa hoja acha kusema nina uwezo mdogo. Toa hoja kama huna endelelea kubwabwaja. Mnaandika comment utakifiri mmekatwa vichwa hamwezi kureason. Vichwa vyenu vipo tu kama mawe vikichosha misuli ya shingo.
 
Watu walitumia wajinga kama mtaji namba moja kisiasa. Hao wajinga walibatizwa kwa jina 'wanyonge' walipita barabarani kugawia wanyonge kiduchu tu manoti ili wajinga wengine waone utawala unawajali. Wanyonge hao waliruhusiwa kutandika biashara zao katika barabara zilizojengwa kwa gharama na kwa malengo tofauti. Haijalishí, hata magari yakishindwa kupita sawa tu. Wenye maduka halali wakishinddwa kuuza sawa tu. Ili mradi wanyonge warudhike. Haijalishi waridhike hadi lini.
Vitambulisho vya mchinga vikatolewa yote hayo ku win sapoti ya wanyonge. Haikutosha, ubabe nao ukatumika kuhakikisha ni chama kimoja tu kiashika hatamu.
 
Wengi tu watafanya misa ya shukurani maana lile tanuli la moto ambalo wengi lilituwakia kwa miaka 5 halipo tunafulahia maisha tena upya kwenye Tanzania ya samia upendo umerejea ashukuliwe Mungu kwakufanya mapinduzi baridi kupitia mzena army
Halafu anakuja mtu hapa na kusema Sabaya anaonewa......Mungu ni Mkuu sana na Nia zake hazichunguziki wala utendaji wake wa kazi
 
Vinana wa chadema tungeni uongo unaoendana na uhalisia.

Leo nimeona mnamuombea M7 afe eti ni dikteta, sasa kama ni kutaka madikteta wafe mbona hamumuombei mwenyekiti wenu afe maana na yeye ni dikteta. Kiongozi yeyote aliekaa madarakani zaidi ya miaka 10 hata kama anashinda uchaguzi ni dikteta anatakiwa kufa.

Mnapoomba madikteta wafe msimuache/msimsahau mwenyekiti wenu kwani nae anatakiwa afe.
 
Lazima alikula hicho kibinti ndio ikawa rahisi kumlundika ndani. Asijidai hakufanya kitu.
 
yaani mliovyo wajinga kwa kiwangoi cha juu sana nyie kuwapa madaraka itakuwa ndoto maana hao watu wa kipato cha chini wafanya biashara ndogondogo mtawapa shida yaani wata pata tabu sana mtawanyanyasa mno kama mnaona kupanga vitu barabarani ni kosa eti imejengwa kwa garama nyie ni makatili kuliko katili mwenyewe tunawaogopa mtawamaliza wamachinga hamtakaa muingie ikulu hata siku moja mpaka mtakapojirekebbisha na kauli zenu za chuki
 
Chadema bana hayo matendo mlikuwa mnafanyiwa mnalalamika utawala wa jiwe, sasa hivi mpo huru bado mnamshambulia Rais, Samia.
 
Tatizo la chadema ni kuamini serikali inawatengenezea matukio na wala hawaamini kama hata Sabaya kwa sasa anatengenezewa matukio,yaani eti chadema hua ni Malaika wasio na dhambi.

Wachaga mna matatizo sana tena makubwa na yasiyo hata na maana yoyote.
Tuondolee utaahira wako hapa
 
Sisi tunachojua ni kuwa dhalim yupo motoni anavuna alichopanda hapa duniani hayo mengine ya kwenu nyie wajane wake
 
kwani kila mtu anaye pata rapsha za maisha ni siasa!?,Basi hata sabaya ni kesi ya kisiasa! Tukubaliane katika Hilo!! au nasema uongo ndg zangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…