Jokate atoa ya moyoni

Fext

Member
Joined
Dec 26, 2016
Posts
47
Reaction score
49
SIKU chache baada ya msanii wa kizazi kipya, Ali Kiba, kudai kuwa anamchukulia mwanamitindo Jokate Mwegelo kama rafiki yake, mrembo huyo ameibuka na kusema huenda aliteleza kutoa kauli hiyo.

Jokate alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki hii alipokuwa anahojiwa kwenye kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Clouds Tv, ambapo mrembo huyo alisema kauli hizo huenda zimetolewa kimakosa.

“Sifikirii sana maana mimi ni mtu ‘positive’ nataka niamini hawakumaanisha, sasa sijui waliteleza au walikosea,” alisema mrembo huyo aliyewahi kushika nafasi ya pili kwenye shindano la Miss Tanzania mwaka 2006.

Mrembo huyo alikwenda mbali kwa kusema: “Unajua katika maisha huwezi kumlazimisha mtu kuona thamani yako, wanasema tenda wema nenda zako mengine ni matokeo na sipendi kulizungumzia sana maana siku hizi watu wanapenda sana kuokota maneno wanayatengeneza wanavyojua wao.”

Kiba na mama yake walimkana Jokate kwenye sherehe ya kumpongeza msanii huyo baada ya kurudi kutoka Afrika Kusini na tuzo ya MTV.

Tuzo hiyo ambayo awali alitangazwa Wiz Kid kwamba ndiye aliyeshinda lakini baadaye uongozi wa MTV wakakiri mshindi halali alikuwa ni Ali Kiba na kuahidi kumpa tuzo yake nchini Afrika Kusini.
 
Sasa aliteleza kivipi mtu hajawahi kukutambulisha kwao na mama mzazi kashasema hakuna kitu kama hiko kuteleza kunatoka wapi jiongeze mtoto wa kike angekuwa anakupenda angekupeleka kwao umri unaenda tafuta mtu sahihi hacha kupoteza mda kabla hujajuta
 
Fact[emoji108]
 
Wengine wamelelewa kuwa ni marufuku kutambulisha viboyfriend na girlfriends nyumbani, anatambulushwa mchumba sio mzinzi mwenzio!!
Kwahiyo inabidi tu uelewe, sio kila kitu ni cha kulalamika jamani.
 
umli= umri

shuleni ulienda kusomea ujinga
 
Acha Movie iendelee...[emoji3]
 
Binafsi sioni makosa ya Kiba, muda ukifika atamtambulisha tu na Joket juwa kwamba pale hukwenda kutambulishwa ilikuwa shughuli nyingine ile jikubali kama wewe ni motima wake siku ikifika mambo yatakuwa bambam ok!
 
Mi ni fan Wa dai but kwa hili kiba alifanya ujinga kichizi .

Anyway kwanza uhusiano wenyewe ulikuwa Wa kibashite bashite tu ulijengwa chini ya misingi ya bifu la kiba na dai .

We jokate punguza nyodo vijana wasomi kama wewe wanakutokea na wanahela ndefu tu unaleta nyodo unawafata hao mabashite maarufu pumbavu sana kula jeuri yako
 
Jokate ndio nani huy??au niyule wa cdm??
 
FaizaFoxy hajapita huku?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…