Jokes za kwenye magroup ya whatsapp ziko lame sana.

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Nipo kwenye group la sekondari. Kwenye hili hakuna kabisa cha maana zaidi ya vichekesho visivyochekesha. Sijui wao wanaona vinachekesha. Hapa nimetika kusoma kichekesho kibovu sana. Angekuwa jukwaani ningemrushia chupa!!!. Tena unakuta kuna memba mmoja yeye ndiyo anaongoza kutumia vichekesho visivyochekesha. Inabifi tu kubaki kukeep intouch na washkaji.
Kama na wewe ni bingwa wa kutupia vichekesho kwenye magroup na unaona mrejesho siyo kivile jitafakari.
 
Inawezekana vinachekesha wewe ndiye unayachukulia maisha serious saana mkuu.
 
Kuna group la kiofisi niliwahi kuwepo, admin wako wawili na wote ni washabiki wa Arsenal, ikifungwa wanabadili settings ili admin pekee ndo aweze kupost kitu. Watu wakawa wanakereka ila hawaongei, ikaja siku ya siku likatengenezwa group (copy ya hilo), ikawa inasubiriwa siku ya Arsenal kufungwa. Tulijitoa wote tukajiunga group jipya na jamaa hawakuwekwa.
 
Uki-left wanaanza kukujadili aah siku hizi mambo yake si mazuri bwana?na blah blah blah nyiiingi!

Wakati mmoja wakaniunga huko kutokana na hakuna cha maana kinachojadiliwa mle nikaamua kujitoa,basi ikawa nikijitoa wananirudisha nikijitoa wananirudisha kama mara tatu hivi wakaniacha.

Siku hiyo nikakutana na class mate wangu mmoja ktk story story ikaibuka habari za lile group,jamaa alinionyesha text jamaa wakijadiliana kwamba mimi mambo yangu siyo mabaya sana na kwamba niliendaga Nigeria kufanya sijui mikataba gani sijui ili nipate hela{huko Nigeria wala ndoto za kufika sina},nilichoka na kilichonisikitisha zaidi waliokuwa wanashadadia sana toka tumeachana mlango wa darasa miaka 18 nyuma hatukuwahi kuonana uso kwa macho,wala hayo maisha waliyokuwa wanaaminishana kwamba ninayo sikuwa nayo.

Hii ni aina tu ya ujinga wa kupotezeana muda na kusengenyana hakuna la maana.

Sent using Redmi Note 5
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…