Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 373
- 829
Meneja wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Hispania, Jorge Vilda ameshambuliwa vikali na wadau wa soka baada ya kuonekana akimshika vibaya kocha wa kike wakati wa kusheherekea ushindi wa Kombe la Dunia la Wanawake 2023.
Video ya sekunde 10 iliyosambaa mitandaoni imemuonyesha Meneja huyo akimshika kifuani mfanyakazi wa kike wa timu hiyo kwa namna isiyofaa.
Vilda ambaye ni mchezaji wa zamani wa Real Madrid amekuwa akilalamikiwa na wachezaji wa zamani na wa sasa kwa tabia mbalimbali ambazo zisizofaa.
Tukio hilo limeongeza hasira na wasiwasi kwa mashabiki na wadau wa soka nchini Hispania ambao mara kwa mara wamekuwa wakichukizwa na tabia za Meneja huyo.
Itakumbukwa kuwa wadau mbalimbali bado wanafuatilia hatima ya kitendo cha Rais wa Shirikisho la soka la Hispania Luis Rubiales kumpiga busu mdomoni mchezaji wa kike Jenni Hermoso juzi wakati wa kusheherekea ushindi wa kombe la dunia.
Video ya sekunde 10 iliyosambaa mitandaoni imemuonyesha Meneja huyo akimshika kifuani mfanyakazi wa kike wa timu hiyo kwa namna isiyofaa.
Vilda ambaye ni mchezaji wa zamani wa Real Madrid amekuwa akilalamikiwa na wachezaji wa zamani na wa sasa kwa tabia mbalimbali ambazo zisizofaa.
Tukio hilo limeongeza hasira na wasiwasi kwa mashabiki na wadau wa soka nchini Hispania ambao mara kwa mara wamekuwa wakichukizwa na tabia za Meneja huyo.
Itakumbukwa kuwa wadau mbalimbali bado wanafuatilia hatima ya kitendo cha Rais wa Shirikisho la soka la Hispania Luis Rubiales kumpiga busu mdomoni mchezaji wa kike Jenni Hermoso juzi wakati wa kusheherekea ushindi wa kombe la dunia.