Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
"Tuko katika mwaka wa pili kujaribu kujenga timu ambayo unajua sio miongoni mwa timu bora duniani", alisema kocha huyo raia wa Ureno.
"Manchester City inanunua mabeki wa kushoto na kulia kwa gharama za washambuliaji", aliongeza.
Mourinho ambaye aliteuliwa kuwa mkufunzi wa United mnamo mwezi Mei 2016 na kuvunja rekodi ya dunia alipomnunua kiungo wa kati Paul Pogba kwa kitita cha £89m, Eric Bailly kwa kitita cha £30m na kiungo wa kati Henrikh Mkhitaryan kwa £26. 3m.
Mwaka huu alimnunua Romelu Lukaku kwa £75m, beki Victor Lindelof kwa £31m na Nemanja Matic kwa £41m.