TETESI ZA USAJILI DIRISHA LA JANUARY.... ALHAMISI 28/12/2017.
1.KLABU ya Liverpool Imefanikiwa kumsajili rasmi Beki wa Southampton Mdachi, Virgil Van Dijik kwa ada ya uhamisho wa pauni £75m huku atakuwa akipokea Mshahara wa pauni £180,000 kwa wiki.Imeelezwa kuwa nyota huyo atakabidhiwa jezi no.4 na atatua Anfield Jumatatu ijayo ya tarehe 1.
2.MANCHESTER UNITED imejitoa kwenye mbio za kutaka kumsajili Winga wa Atletico Madrid, Antoine Griezmann hivyo kuipa nafasi kubwa Fc Barcelona kumsajili Mfaransa huyo kwa pauni £89m.
3.CRYSTAL PALACE & BURNLEY & EVERTON zinapigana vikumbo kuiwania saini ya Mshambuliaji wa Angers ya Ufaransa, Karl Toko Ekambi.Fowadi huyo wa Cameroon amefunga mabao 9 katika Ligue 1 msimu huu.
4.WATFORD itampa mkataba wa miaka mitano Mshambuliaji wake , Abdoulaye Doucoure ambaye anatakiwa na Arsenal.
5.WINGA wa Borussia Dortmund Andre Schurrle anakaribia kujiunga na Stuttgart kwa mkopo.
6.PSG wanamtaka Kiungo wa Manchester United Marouane Fellain kwa uhamisho huru.Mbelgiji huyo atakuwa huru Jumatatu ya tarehe 1 kujiunga na klabu yoyote japo Galatasaray wanahitaji huduma yake.