Joshua alilisimamisha Jua

how reasonable is it to discredit proven facts by arguments based on conspiracy theories? maana hii ingekuwa Big news ujue, no pun intended.
 
Hivi vitabu vinaitwa vitakatifu vimetudanganya sana, ni muda wa kusema stop sasa. Tuunde dini Mpya ya kizazi cha kisasa
 
Nikurekebishe tyu sio kweli jua halizunguki kokote hamna sayansi kama hio
Ila dunia inazunguka jua while jua na solar system yote linazunguka around a centre commonly called as the black hole in the milky way galaxy
Jua linazunguka black hole? Tangu lini? Ebu tupe hizi details mi naona ni sayansi mpya kabisa kwangu
 
Biblia inatumia imani kuwaelekeza watu jambo fulani,lakn science inatumia observation and experimentation,kwa hyo kinachooandkwa kwenye Biblia Mara nyingi hakina uhusiano na kile kilichopo kwenye science!
kwaiyo joshua alisimamisha jua ambalo lilikua kwenye safari yake, au unataka kutuaminisha nini mkuu.
 
mambo ya kiimani hayalinganishwi na mambo ya kisayansi, Ya rohoni yatafunuliwa kwa walio rohoni na ya sayansi yataelezewa na wanazuoni
 
Ukizingatia copernicus theory Joshua alisimamisha mzunguko wa dunia siyo jua. ukisimamisha mzunguko wa dunia jua linaganda sehemu moja.
hayo ni mawazo yako ndugu..biblia ishasema jua lilisimama..kwani wao hawakuwa wanajua kuwa wasemacho???.
kuna ndugu kauliza.mbona mpaka leo ktk ulimwengu wa sayans kuna maneno (jua kuzama-jua kuchomoza)
ni dhahiri kuwa hiyo ndo elimu ya zamani ambayo ndiyo ilikua na ukweli.kuwa jua ndo hulizunguka dunia.
kuna kisa cha nabii Ibrahim katika uislamu kinasema.
siku moja Ibrahim alikua akipewa mitihani na mfalme mmoja.mtume Ibrahimu akamuambia yule mfalme.."MUNGU nnayemuabudu anaweza kuua na kuhuisha..".yule mfalme akataka kumuonyesha kuwa nayeye ana uwezo huo.akatoa wafungwa wawili...mmoja akamuachia huru mwingine akamchinja.akamuuliza Ibrahim .umeona.nimeua na nimehuisha...
Ibrahim akampa swala lingine..MOLA ninayemuabudu mimi hulitolea jua mashariki kila siku..hivyo kama wewe uko na uwezo kama yeye kesho asubuhi lifanye lichomozee magharibi badala ya mashariki...yule mfalme alishindwa...hii inamaana jua husafiri kulizunguka dunia...
katika maandiko yote ya kiimani.hakuna sehemu inasema kuwa dunia hutembea/zunguka.
pia kuna yule mtabiri BABA VANGA..yule mwanamke kipofu...alitabiri kuwa jua litakuja kuzima.alaf watawasha jua lao feki/artificial sun...hlivyo hii inamaana kuwa jua ni dogo na siyo kubwa kama tunavyoaminishwa.na lipo karibu tuu.si mbali kama wanavyodai....
 
Kupatikana kwa usiku na mchana kunatokana na Dunia kulizunguka Jua kwa kipindi cha SAA 24.,ktk story ya Joshua,Aliomba Jua lisimame ili mapigano yaendelee kwa muda but hiki kisa hakijaweka bayana km athari ya Jua kusimama iliathiri na sehemu nyingine ama ni ktk Eneo lile tu!!Ingawa kusimama kulikokusudiwa hapa ni kukawiza muda wa Jua kuzama,so still ht km Dunia ilikua Ipo ktk mzunguko(Scientifically) as Usual bado uwezo wa kimiujiza(Spiritual) wa jua kutozama Ilikua na power ZAIDI,.Ni issue ambayo IPO ktk kiimani ZAIDI

NB;Kwa miaka ya HV karibuni imegundulika pia Jua hujizungusha ktk mhimili wake japo kwa taratibu sn
 
Hivi vitabu vinaitwa vitakatifu vimetudanganya sana, ni muda wa kusema stop sasa. Tuunde dini Mpya ya kizazi cha kisasa
Wewe umenifanya nicheki kwa uangalifu mkubwa sn kwa post yako
 
Shareef Conscious Kupatikana kwa usiku na mchana kunatokana na Dunia kulizunguka Jua kwa kipindi cha SAA 24.,
Siyo sahihi.Dunia inazunguka jua kwa siku 365 mwaka mzima. Dunia pia inazunguka kama feni. Mzunguko huu kipindi masaa 24. (Rotational motion about its axis ) Mzunguko wa saa 24 ndio chanzo cha jua kuchomoza na kutua.
 
Mkuu umecopy hadi codes za website!
 
mkumbuke halikusimama jua peke yake, mwezi nao ulisimama. Je ni kwanini Joshua alipoomba Jua lisimame na Mwezi nao ukasimama?

kupitia maandiko ya kitabu BIBLIA, JUA NA MWEZI ndio vitu pekee vitupatiavyo MUDA, SIKU na MAJIRA YA MWAKA.

kuna Usemi "BORA KUSHUHUDIA KULIKO KUHADITHIWA" je sisi tunachoshuhudia ni Jua kutembea Kuizunguka Dunia au tumeambiwa Dunia inatembea kulizunguka Jua?

hakuna kipya chini ya Jua........ kwa maneno haya, hivi jua lipo wapi? na juu ya jua kuna nini? na wakati wa usiku kwa sisi huku juu panakuwa wapi?

Biblia inaelewana na kila awezae kuisoma, na ndio maana ina wasomaji wengi kuliko kitabu chochote kile ukijuacho. hivyo kila mmoja ana namna ya aielewavyo, lakini kuna maandiko mengine ni lazima uelewa ufungane kwa kila aliyeisoma kwa mfano AMRI ZA MUNGU, hakuna maana nyingine ya kuitafsiri USIIBE, USIZINI nk, hivyo hivyo Hata Joshua alipoomba Jua lisimame, alimaanisha Jua maana kila mmoja wetu huliona Jua likitembea, sasa kama aliyefanya Joshua aone Jua limesimama, alikua kaisimamisha Dunia, hapo hakuna ajuae. Kikubwa Jua lilisimama. na sio jua tuu, mwezi nao ulisimama.

sasa kama tunakubali mwezi unaizunguka dunia tunakataaje Jua kuizunguka dunia ilhali, namna tuuonavyo Mwezi ukiwa katika safari yake hauna tofauti na jua na kunawakati vyote vinapita katika njia moja, yaanillipopita jua na mwezi kupita palepale.

waandishi wa Biblia hawakuwahi kudanganya, ila kama kuna uongo katika kitabu hiko tuwalaumu waliokitafsiri. na tukumbuke inachofanya SAYANSI ni kuprove uhalisia wa dunia na vilivyomo kiasilia, ndio maanawatu waliweza kuchimba mafuta mpaka kupata lami ya kuiweka katika SAFINA kabla hata hao wanasayansi hawajawazwa kuzaliwa, ila sifa wanapewa wao kwa ugunduzi hewa.

JUA= tunapata masaa, rejea mababu zetu, ila Sayansi imetucholea mistari.
MWEZI= una siku 28 tuu hazizidi wala kuongezeka, kama lilivyo jua na siku 30 tuu, ila wanasayansi wametuletea kalenda.

sasa watashindwaje kutuletea habari za dunia kujizungusha na kulizunguka jua kuliko tunavyona dunia haizunguki na Jua ndilo linaizunguka dunia?

JUA ndilo linaloizunguka dunia ili tupate masaa, kwa hiyo ni sawasawa tuu kuwa Joshua aliomba jua lisimame ili masaa yasimame apambane.

Hivyo Yani!!
 
isijekua Jua lilisimamishwa February ndio maana huu mwezi unasiku pungufu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…