Joyce Ndalichako Amechemka, Ajipange!!!

Papaa Kinyani

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2013
Posts
1,459
Reaction score
699
Kuna watu, kama Ndalichako wanasema eti wanasiasa wasiingilie kazi za elimu. Watendaji wa elimu wafanye wanavyotaka, wanasiasa wanyamaze tu, hata kama watendaji wamefanya madudu. Kutakuwa na umuhimu gani wa kuwa na wanasiasa? Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani anaongea sana kwa kujihami sawa na wanasiasa halafu haitaki siasa. Yeye ndiye mwanasiasa namba moja. Hatujawahi kuona Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani anayeongea ongea sana kama huyu.

Watendaji katika Wizara mbalimbali kama vile Elimu hususani Baraza la Mitihani wanavurunda kazi (mitihani) kila kukicha, wananchi na wabunge wanalalamika, wao kwa kujihami wanataka wasiingiliwe na wanasiasa. Je, kukosolewa ni kuingiliwa utendaji wao? Ukatibu utendaji SIO taaluma, ni cheo cha kupewa tu. Baadhi ya viongozi wa Baraza la Mitihani achieni ngazi kulinda heshima zenu.

Isingekuwa wanasiasa hadi leo kusingekuwa na sekondari za kata, wanafunzi wasingepata mikopo ya elimu ya juu kwa wakati kwa sababu ya watendaji wabovu kama wa Baraza la Mitihani. Kila mwaka wanafunzi watajinyonga kwa matokeo mabaya yanayosabibishwa na usahihishaji wa baraza ambao labda hata taaluma zao ni dhaifu.

Nashauri serikali wangechunguza background za taaluma za viongozi wa Baraza la Mitihani, nina wasiwasi kuwa ni fake.
​
Wanasiasa mhakikishe kuwa mnawadhibiti watendaji wote wabovu kulinda heshima ya taifa.

Bravo Politicians.
 
Mtoa mada usiwe kilaza kuongea usichokijua...
Kazi ya necta ni kutunga mitihani kwa kutumia mitaala iyoandaliwa, kusimamia mitihani na kusahihisha.
Mh. DR Loyce Ndalichako kipi hajatekeleza ktk hayo?
Ndiyo kwanza kwa Raisi ya umoja wa african exam council kwa sababu kazi yake tz kaifanya vizuri.
Mtoa mada umekurupuka
 

Nadhani jina lako linatosha kutueleza wewe ni mtu wa aina gani
 
Nadhani mzimu wa ziro bado unakusumbua mtoa mada ndio maana unamtukana Ndalichako! hv wewe unazijua kazi za NECTA?? au unajua hata kirefu chake?? By the way si kosa lako ni kosa la kuwasikiliza na kuwashabikia vilaza CHADEMA.
 
ni vema upate muda wa kuandaa hoja yako ili uje na mawazo mazuri ni kweli kuna wakati NECTA inavurunda ila si sababu za kisiasa la hasha pengne ni za utendaji tu na changamoto zake,..
 
Huyu mama anajipalia makaa. Ametoa kauli hiyo wakati tayari kuna kikundi maalum cha wanasiasa kilichoundwa kumshughulikia kutokana na misimamo yake. Hivi sasa kuna mpango wa kuandaa maandamano makubwa ya kumng'oa unaoratibiwa na wanasiasa na tayari kuna uhamasishaji mkubwa unafanyika.

Baadhi ya nyaraka zilizozagaa kuhusu mpango huo hizo hapo. Kauli yake itachochea kasi ya kumshughulikia
 
Mtoa mada unachuki binafsi!wewe na jamaa zako kamwe hamtaweza kumtoa Dr Ndalichako kwa majungu yenu mnayoyapiga.................!
 
Mother fackaaaa, jaman Admin JF mko wapi? hawa watoto wanatuharbia jukwaa bwanaaa, sasa post gan hii.
 

Kakurupuka sana huyo mwadnika mada, elimu na siasa ni vitu tofauti binafsi nimemuelewa vizuri Doctor Ndalichako ningependa aendelee kuwa katibu mtendaji wa NECTA hata kwa miaka kumi ijayo maana ni kati ya wanawake shupavu sana
 
Mtoa mada unachuki binafsi!wewe na jamaa zako kamwe hamtaweza kumtoa Dr Ndalichako kwa majungu yenu mnayoyapiga.................!

Mkuu umenena. Nchi hii inataka mafisadi tu ndiyo wanaonekana watu wa maana. Ukiwa mchapakazi unapigiwa mazengwe usiku na mchana ili mradi wakuvuruge tu. Tuna safari ndefu na madaraja yote njiana yamebomoka kufika ni next tu impossible kwa style hii ya majungu tene kwenye Jukwaa la Elimu. Sasa Jukwaa la Majungu litakuwaje?
 

Wanataka viongozi mafisadi ndiyo maana hayo inayoyasema hawaoni kama ni hoja za msingi. Nchi hii imekumbwa na majanga ya ajabu sana na viongozi wamekuwa walalamikaji badala ya kuchukua hatua
 
ulipokuwa shule ulikuwa busy na facebook,kuchek pono na umalaya,je kweli ungeweza pata hata 4 ya 30?????????????? endelea kurist mdogo wangu ukikua utafaulu
 
Mtoa mada unachuki binafsi!wewe na jamaa zako kamwe hamtaweza kumtoa Dr Ndalichako kwa majungu yenu mnayoyapiga.................!

Sidhani kama ana chuki, nachoona ni kwamba kichwa chake kinafugiwa nywele tu na kutumika kucheka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…