Papaa Kinyani
JF-Expert Member
- Feb 25, 2013
- 1,459
- 699
Kuna watu, kama Ndalichako wanasema eti wanasiasa wasiingilie kazi za elimu. Watendaji wa elimu wafanye wanavyotaka, wanasiasa wanyamaze tu, hata kama watendaji wamefanya madudu. Kutakuwa na umuhimu gani wa kuwa na wanasiasa? Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani anaongea sana kwa kujihami sawa na wanasiasa halafu haitaki siasa. Yeye ndiye mwanasiasa namba moja. Hatujawahi kuona Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani anayeongea ongea sana kama huyu.
Watendaji katika Wizara mbalimbali kama vile Elimu hususani Baraza la Mitihani wanavurunda kazi (mitihani) kila kukicha, wananchi na wabunge wanalalamika, wao kwa kujihami wanataka wasiingiliwe na wanasiasa. Je, kukosolewa ni kuingiliwa utendaji wao? Ukatibu utendaji SIO taaluma, ni cheo cha kupewa tu. Baadhi ya viongozi wa Baraza la Mitihani achieni ngazi kulinda heshima zenu.
Isingekuwa wanasiasa hadi leo kusingekuwa na sekondari za kata, wanafunzi wasingepata mikopo ya elimu ya juu kwa wakati kwa sababu ya watendaji wabovu kama wa Baraza la Mitihani. Kila mwaka wanafunzi watajinyonga kwa matokeo mabaya yanayosabibishwa na usahihishaji wa baraza ambao labda hata taaluma zao ni dhaifu.
Nashauri serikali wangechunguza background za taaluma za viongozi wa Baraza la Mitihani, nina wasiwasi kuwa ni fake.
​
Wanasiasa mhakikishe kuwa mnawadhibiti watendaji wote wabovu kulinda heshima ya taifa.
Bravo Politicians.
Watendaji katika Wizara mbalimbali kama vile Elimu hususani Baraza la Mitihani wanavurunda kazi (mitihani) kila kukicha, wananchi na wabunge wanalalamika, wao kwa kujihami wanataka wasiingiliwe na wanasiasa. Je, kukosolewa ni kuingiliwa utendaji wao? Ukatibu utendaji SIO taaluma, ni cheo cha kupewa tu. Baadhi ya viongozi wa Baraza la Mitihani achieni ngazi kulinda heshima zenu.
Isingekuwa wanasiasa hadi leo kusingekuwa na sekondari za kata, wanafunzi wasingepata mikopo ya elimu ya juu kwa wakati kwa sababu ya watendaji wabovu kama wa Baraza la Mitihani. Kila mwaka wanafunzi watajinyonga kwa matokeo mabaya yanayosabibishwa na usahihishaji wa baraza ambao labda hata taaluma zao ni dhaifu.
Nashauri serikali wangechunguza background za taaluma za viongozi wa Baraza la Mitihani, nina wasiwasi kuwa ni fake.
​
Wanasiasa mhakikishe kuwa mnawadhibiti watendaji wote wabovu kulinda heshima ya taifa.
Bravo Politicians.