United ya Ferguson
JF-Expert Member
- Oct 29, 2021
- 3,132
- 6,353
Wachezaji wa Uingireza hawajawahi kuwa wa bei nafuu toka kizazi cha zamani hadi kizazi kipya, kutokea kwenye mishahara wanayolipwa hadi kwenye bei ya kuwauza sokoni. Kwanza Waingireza wenyewe wanajua kuwafanyia Uhamasishaji wachezaji wao ili wakiwa sokoni wauzike bei kubwa.
Ukishaona mchezaji wa Uingiireza ana jina elewa kabisa ukienda kumuhitaji unaenda kupasuka, haijalishi ancheza vizuri sana au kawaida. Kwa mfano rejea kwa John Stone kutoka Everton kwenda City, rejea kwa Jack Glearilish kutoka Villa kwenda City, rejea kwa Kyle Walker kutoka Spurs kwenda City, rejea kwa Rio Ferdinand kutoka Leeds kwenda Man United, mifano ipo mingi sana.
Mfano muangalie Leo Rashaford, watu wanamzihaka na wanamsema, ila linapokuja swala la kuuzwa bei yake unaweza kukimbia. Kuna kipindi Barcelona walipeleka ofa ya kumtaka Rashford, bei waliyotajiwa waliishia kujikuna vichwa tu!
Harry Maguire pamoja na shida zake zote alizonazo, timu yoyote Ile ikipeleka pua pale kumuhitaji bei itakayotajiwa huwezi kuamini kabisa kama ndio huyu Harry Maguire anayetukwana kila siku. Nenda kamguse Declan Rice wa Westaham, pesa utakayotajiwa huwez kuamini kabisa!
Dortmund baada ya kumuuza Sancho, Mr robot naona wameanza kutengeneza mazingira ya kuja kuvana pesa nyingne ya kutosha kutoka kwa kijana wa Uingireza Jude Bellingham.
Washajua kabisa hii ni pesa tena pesa ndefu kweli kweli, wao siyo wajinga kuanza kumkabidhi kitambaa cha unahodha. Washajua timu za Uingiireza zishaanza kutokwa na udenda kwa kijana wao, ni ishu ya muda tu Dormound anavuta mkwanja mrefu kotaka kwa huyu kijana wa Uingireza.
Ukishaona mchezaji wa Uingiireza ana jina elewa kabisa ukienda kumuhitaji unaenda kupasuka, haijalishi ancheza vizuri sana au kawaida. Kwa mfano rejea kwa John Stone kutoka Everton kwenda City, rejea kwa Jack Glearilish kutoka Villa kwenda City, rejea kwa Kyle Walker kutoka Spurs kwenda City, rejea kwa Rio Ferdinand kutoka Leeds kwenda Man United, mifano ipo mingi sana.
Mfano muangalie Leo Rashaford, watu wanamzihaka na wanamsema, ila linapokuja swala la kuuzwa bei yake unaweza kukimbia. Kuna kipindi Barcelona walipeleka ofa ya kumtaka Rashford, bei waliyotajiwa waliishia kujikuna vichwa tu!
Harry Maguire pamoja na shida zake zote alizonazo, timu yoyote Ile ikipeleka pua pale kumuhitaji bei itakayotajiwa huwezi kuamini kabisa kama ndio huyu Harry Maguire anayetukwana kila siku. Nenda kamguse Declan Rice wa Westaham, pesa utakayotajiwa huwez kuamini kabisa!
Dortmund baada ya kumuuza Sancho, Mr robot naona wameanza kutengeneza mazingira ya kuja kuvana pesa nyingne ya kutosha kutoka kwa kijana wa Uingireza Jude Bellingham.
Washajua kabisa hii ni pesa tena pesa ndefu kweli kweli, wao siyo wajinga kuanza kumkabidhi kitambaa cha unahodha. Washajua timu za Uingiireza zishaanza kutokwa na udenda kwa kijana wao, ni ishu ya muda tu Dormound anavuta mkwanja mrefu kotaka kwa huyu kijana wa Uingireza.