Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF): Waziri Silaa ameshindwa kuwa karibu na Waandishi wa Habari

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112

Jerry Silaa, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limeeleza kutoridhishwa na kitendo cha Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, kukosa kuhudhuria mikutano muhimu ya wadau wa habari.

Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, ametoa kauli hiyo leo Novemba 7, 2024, katika Mkutano Mkuu wa Nane wa TEF uliofanyika Dar es Salaam. Waziri Silaa, licha ya kualikwa, hakuweza kuhudhuria na badala yake alimtuma Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

"Tukiwa kama wahariri, hatufurahishwi na mwenendo wa Waziri Silaa. Amealikwa kwenye Mkutano wa PST, hakufika; amealikwa kwenye tuzo za waandishi wa habari, hakuhudhuria; amealikwa Mbeya kwenye tukio la wadau wa habari, hakuwapo; na sasa Mkutano Mkuu wa TEF pia hajaja. Hii inaashiria kwamba Waziri hana nia ya kushirikiana na wadau wa tasnia ya habari."

Balile ameleza kuwa mikutano kama hii ni jukwaa muhimu ambapo wadau wa habari wanapata nafasi ya moja kwa moja kujadiliana na Waziri kuhusu mustakabali wa tasnia, na kutoonekana kwake kunakwamisha juhudi za ushirikiano.

"Mikutano hii ni fursa kwa Waziri na wadau wa habari kukutana na kuzungumzia changamoto na maendeleo ya tasnia. Kutokuwepo kwa Waziri ni dalili ya kukosekana kwa dhamira ya kushirikiana nasi."

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Nicholas Mkapa, ambaye amemwakilisha Waziri Silaa katika mkutano huo, amesema Waziri alikuwa na majukumu mengine ya kiofisi, na hivyo kumtuma yeye kuhudhuria kwa niaba yake.

Balile pia amekumbusha kuwa wakati Waziri Nape Nnauye aliposhikilia Wizara hiyo, alionesha ushirikiano wa hali ya juu kwa kuhudhuria mikutano yote muhimu ya wadau, na kuwa shirikiano huo ulikuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya tasnia ya habari.

Pia, soma:
 
Silaa ni mzee wa michongo, hapo hawezi kuja, kule ardhi alikuwa anapiga mkwara mikocheni, au mbezi, kariakoo, anaokota mbili tatu. Sasa nyie wahariri mtampa maneno tu.

Ila watu ndio watakuwa wanaelewa uwezo wake, ni tabularasa mzuri tu. Populist, sasa hiyo Wizara haina hizo
 
Waandishi uchwara Hawa wamemisi bahasha za kaki
 
Mzee wa clinic za ardhi hahahah. Ccm bhana
 
nadhani ni muhimu zaidi kwa Deodatus Balile kuachia ngazi kwa heshima.

kwa muda aliokaa uongozini, nadhani hana jipya tena pale TEF, bali bali kutoa lawama na kuendekeza uchochezi na uchonganishi baina ya nani anafaa na nani hafai kwenye wizara ya habari, kitu ambacho kina ishara ya kutafutia watu kazi kwa mamlaka za uteuzi, huku wengine wakionekana hawafai 🐒
 
Mzee wa clinic za ardhi hahahah. Ccm bhana
Kapelekwa Wizara ambayo ina mambo ya tehama yanayotawala dunia, na ina vijana wengi, ameshindwa kabisa kwenda na upepo.

Ilikuwa ni fursa ya kujenga mfumo wa uchumi wa kidigitali.

Alikuwa Ardhi, kapoteza fursa ya ku-digitise land transaction ili kuondoa migogoro. Alikuwa anatatua migogoro kwa kutembea nyumba kwa nyumba.

Ona sasa, amekosa fursa ya kuwasilisha ujumbe wa Rais kwa wahariri
 
Safi sana kaka hakika wewe unamjua kama mimi ni mzee wa michongo yule tangu akiwa meya kafany populism pale ardhi wa2 wamemuona wa maan wakat alikua anatak apewe viwanja bure had Arusha na ndo chanzo cha kuhamishwa.
 
Uzuri bosi wake ana macho kila mahali. Hatukawii kusikia tangazo kwa umma 🤣🤣🤣🤣🤣🤣. Mama hataki mchezo kazini.
 

Balile aache tabia ya unafiki na kupenda bahasha. Yaani Waziri aache kwenda bungeni ahudhurie vikao vya mishiko? Sasa alitaka sura ya Silaa au uwakilishi wa Wizara. Yaani anadiriki kudharau uwepo Naibu Katibu Mkuu? Balile ana kiburi sana! Yaani ameona Naibu huyo si kitu!

Alafu hicho kigenge kinachoitwa Jukwaa la Wahariri kazi yake ama majukumu yake ni yepi zaidi ya uchawa na bahasha??!!
 
Silaa ameshindwa kupeleka ujumbe wa Rais kwa wanajanari! Hivi anajielewa kweli?
 
Safi sana kaka hakika wewe unamjua kama mimi ni mzee wa michongo yule tangu akiwa meya kafany populism pale ardhi wa2 wamemuona wa maan wakat alikua anatak apewe viwanja bure had Arusha na ndo chanzo cha kuhamishwa.
Yeah.... Alikuwa anatoa amri kila kamishna wa ardhi wa mkoa ampe viwanja. Ulikuwa humuoni vijijini, yeye ni mikocheni, mbweni, kariakoo, mbezi, arusha, mwanza,dodoma
 
Silaa inaonekana anachagua wizara, tangia aondoke Ardhi yuko disappointed. Rais ampige chini wenye sifa na moyo wa kufanya kazi ni wengi
Ni arrogant sana, ile issue ya morogoro alipomdhihaki mwananchi ndio rangi yake ilivyo
 
Ni kutafuta rushwa pekee
 
Mnataka na huko ang'olewe? Slaa aliondolewa ardhi baada ya kukanyaga maslahi ya watu kwa maslahi ya taifa, huku akijiamini ana report kwa presidaa, kilichotokea sasa hivi anaogopa kila mtu
 
Tangu Silaa awatukane CHADEMA kuwa wanajiteka nilimdharau Sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…