Akihojiwa katika kipindi cha Jambo (TBC 1) cha leo tarehe 5/6/'15, waziri mwenye dhamana ya michezo nchini ametoa maoni yake kuhusu kocha msaidizi wa timu ya taifa, Taifa Stars- Mecy Maxime kuwa hafai kwa sababu bado mdogo, na kama angeulizwa yeye kuhusu kocha msaidizi angependekeza mtu kama Abdalah Kibadeni.
Kwangu mimi, naona hoja yake haina mashiko kwa kuwa kazi ya ukocha si ya kubeba matofali, bali ni ujuzi. Wapo kina Pep Guardiola ni vijana na wanafanya vizuri. Hata hao aliowataja yeye kuwa wanafaa wamekuwa makocha siku nyingi lakini sioni kigezo cha kuwapa timu ya taifa kwa kuwa hakuna jipya walilowahi kufanya hadi kustahili nafasi hiyo.
Namshauri waziri aache kufanya mambo kwa mazoea.
Kwangu mimi, naona hoja yake haina mashiko kwa kuwa kazi ya ukocha si ya kubeba matofali, bali ni ujuzi. Wapo kina Pep Guardiola ni vijana na wanafanya vizuri. Hata hao aliowataja yeye kuwa wanafaa wamekuwa makocha siku nyingi lakini sioni kigezo cha kuwapa timu ya taifa kwa kuwa hakuna jipya walilowahi kufanya hadi kustahili nafasi hiyo.
Namshauri waziri aache kufanya mambo kwa mazoea.