Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
JUMUIYA YA WAZAZI SIHA IMEADHIMISHA WIKI YA WAZAZI KWA KUPANDA MITI ZAIDI YA 100 SHULE YA MSINGI MENDAI
Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Siha Mkoani Kilimanjaro imeadhimisha wiki ya Wazazi Wilaya ya Siha kwa kupanda miti zaidi ya 100 katika shule ya msingi ya Serikali ya mchepuo wa Kingereza ya Mendai iliyopo kata ya Karansi.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Kilimanjaro Daudi Mrindoko,amesema Jumuiya hiyo itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha ushindi wa CCM 2024/2025 kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinashinda kwa kushinda.
Kwa Mujibu wa Mrindoko, kipimo Cha CCM kuweza kushinda Serikali za mitaaa,ambapo ameshauri wanachama hao kwa yeyote anayeona anatosha kuwania nafasi yoyote ya uongozi ikifika wakati akajaze fomu ya kuwania nafasi ya uongozi.
Hata Hivyo ameshauri viongozi wa Chama hicho kuyasemea maendeleo yote wanayoyafanya katika Maeneo yao wanayoyaongoza