Jumuiya ya wazazi mnaipeleka wapi ccm!

M-bongo

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2008
Posts
338
Reaction score
71
Baada ya heka heka kubwa na vurugu za hapa na pale zikiambatana na mipasho kibao kwenye vyombo vyetu ya habari( sio udaku) japo kwa sasa naanza kupata wakati mgumu kutofautisha vipi ni vyombo vya udaku na vipi si vyombo vya udaku!
Naandika hili ili wote watakaoona kuna umuhimu basi nipate mawazo yao. Jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi wiki iliyopita ilimaliza uchaguzi wake kwa kujaza nafasi mbali mbali ikiwemo ile ya Mkiti ambapo Balozi Mhina alimshinda mpinzani wake mkuu Bwana Bulembo! baada ya uchaguzi mengi yamesemwa mengine yakiwa ya kweli mengine yakiwa ni kuendeleza zile siasa zetu za maji taka! binafsi ningependa kupata mawazo hapa kwa kuamini kuwa hapa JF kuna wale waliokunywa maji ya Bendera (CCM) kama inavyoaminka na wengine wasiotaka hata kusikia jina hilo, hoja yangu hapa ni kuwa WAZAZI wametumia kigezo kipi kumchagua balozi Mhina mwenye umri wa lala salama? Mzee asiye weza kufanya hata mikutano mitatu ya ya hadhara ya kampeni kwa siku moja! Balozi Mhina ataweza kupambana na ZITO KABWE JUKWAANI KULE KIGOMA! BALOZI MHINA ATAWEZA KUPAMBANA NA NA NDESA kwenye kampeni Moshi! na kumuacha mtu kama Bulembo eti hana Elimu, aliyesema ukiwa Mkiti wa wazazi wa CCM utakuwa na vipindi chuo kikuu cha Muhimbili nani? wazazi wanaweza kutuambia nini juu ya F.S aliyepata uwaziri mkuu akiwa na Diploma ya kilimo? au A.L.M aliyepata kuwa waziri wa mambo ya ndani akiwa na cheti cha ualimu! na mifano mingi kibao. kibaya zaidi kinachozuka CCM muda huu ni kila mtu akiungwa mkono na watu wengi eti FISADI! FISADI, FISADI, FISADI. ninachokijua mimi ABDALA MAJURA BULEMBO angeweza kufanya kazi nzuri zaidi ya kuongoza jumuiya ya wazazi kuliko Mzee Mhina. katika mazingira ya kisiasa ya leo kumuacha Bulembo na kumchagua Mzee Mhina si elewi kabisa CCM inakwenda wapi! any way let me call it a story! nimalizie kwa msemo mmoja wa kisukuma na kinyamwezi MBITI YA TYULULUKA HA SHIGULU, YA MBULA NHALE! ( kwa kawaida fisi hupenda kusimama juu ya kichuguu kwa muda mrefu, ukimuona fisi kasimama juu ya kichuguu na kushindwa kuhimilikisha kuteleza basi ujue mvua imesha kubwa sana
 
M-bongo mbona walalamika sana au nawe ulikuwa Dodoma nini? na kama kashindwa Bulembo si uchaguzi au, na swala la kuwa alichaguliwa ni mzee we ina kuhusu nini! hata kama huyo hataweza kuhimili mikiki mikiki ya kampeni si ndio bomba ili tuwachape vizuri maana sikio la kufa halisikii dawa! malalamiko yako wengine hayatusaidii kama mnachemsha wengine ndo furaha yetu, twa subiri kwa hamu
 
Kuna habari kutoka Raia mwema hapa... ndio huyu jamaa yako alitaka kufanya vitu nini?
Mashushushu wazima mamilioni ya mgombea

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…