JWTZ na ulinzi wa Katiba ya nchi

JWTZ na ulinzi wa Katiba ya nchi

Down To Earth

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
21,940
Reaction score
16,643
katika pita pita zangu nikiwa nasoma hasa chimbuko la jeshi letu la wananchi la Tanzania, nimekutana na hili, kuwa jukumu mojawapo ambalo toka JWTZ ianzishwe mwaka 1964, ni Kulinda Katiba na Uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hili jambo limepewa kipaumbele kabisa na kupewa jukumu la kwanza kabisa la jeshi letu la taifa.

wakuu naomba tuelimishane hapa kuhusiana na hili, JWTZ inahusika vipi na ulinzi wa katiba hasa hasa tukizama katika kipindi hiki kigumu tulichop cha utengenezaji wa katiba mpya?

Mpaka sasa sijaona involvement ya JWTZ katika kuhakikisha kuna amani BUNGENI huko wanakojaribu kuandika katiba mpya..

Karibuni.
 
Ni kweli ulinzi wa katiba ni moja ya jukumu kuu la jwtz, ingawa hawalitekelezi ipasavyo. Jeshi ndo la kumshughulikia rais akivunja katiba. Jeshi lilipaswa kumshughulikia yule aliyezinisha matumizi ya katiba ya zanzibar ya 2010 iliyovunja katiba ya muungano...
 
Jeshi letu linajali sana itifaki. lisichokozwe kwa uzembe wa viongozi wachache waliopewa dhamana.
Mzee wetu ndiye alipaswa kuisimamia katiba na kuilinda kwa kutoa maagizo kwa vyombo vya ulinzi.
Mzee ametoa mwanya mkubwa wa inayoitwa democracy ambayo huku duniani haipo.
Mimi ni muumini wa Biblia. Mithali 29:25 Inasema kuwaogopa wanadamu kunaleta mtego. Nadhani mnaikumbuka Kanuni hii ya uongozi; Ni bora kufanya Maamuzi mabaya kuliko kutofanya maamuzi kabisa......
 
Kwani kuilinda katiba unaelewaje mkuu?
Mimi nachojua jeshi kuilinda katiba si kufanya maamuzi juu ya utendaji wa kawaida wa viongozi.

Katiba ni sheria mama kwa hiyo jeshi hutekeleza wajibu kulingana na sheria na taratibu zilivyo za nchi na hii ndiyo kulinda katiba yenyewe.

Kumbuka jeshi ni moja kati taasisi nyeti na zinazoongozwa si kwa mihemuko ya kisiasa kama zilivyo taasisi nyingine za kawaida.

Jeshi lina kitabu chake kiitwacho JUZUU kama sijasahau. Humo zipo sheria zote za nchi na sheria za kijeshi hivyo utaratibu unaotumika jeshini wote unapatikana humo.

Kwenye kitabu hicho ndimo kwenye maandishi yanayoainisha maamuzi ambayo yatafikiwa endapo tukio fulani litatokea mf

1.Kama nchi ikivamiwa na nchi nyingine ni utaratibu gani unatakiwa ufuatwe?

2. Ni wakati gani ambapo raisi anaweza kutangaza hali ya hatari na akifanya hivyo jeshi linatakiwa litekelezeje?

3. Ni wakati gani ambapo jeshi linaweza kuchukua jukumu la kuondoa uongozi kwenye madaraka. Na mengine mengi kama hayo.

Ni vizuri kufahamu mambo haya:
Wananchi ndiyo walio iingiza serikali madarakani na pia ndio waliochagua wawakilishi wao wa kuwawakilisha bungeni. Na hii ni kutokana na haki ya kidemokrasia ambayo ni kipengele kimojawapo kwenye hiyo katiba.
Hivyo basi kwakuwa jeshi kazi yake ni pamoja na kuilinda katiba lazima iheshimu wawakilishi wote wa wananchi (Viongozi + wabunge ) bila kupendelea.

Kama pande hizi mbili hazikubaliani kwa hoja bado jeshi halina mamlaka ya kuingilia mpaka wenyewe watakapo patana au kuondolewa na wananchi kwenye nyadhifa hizo kwa njia ileile ya kidemokrasia.

Kulifikiria jeshi kwa maswala ya kisiasa sidhani kama ni njia muhimu ya kufikia malengo yaliyo tarajiwa.

Mwisho naomba nikuulize maswali mtoa mada,
Ulitaka labda jeshi liingilieje mchakato wa katiba?

Kwakuwa serikali imeweka msimamo wake itolewe madarakani kwani jeshi ndilo lililoiweka kwenye madaraka?

Kwakuwa UKAWA wamekataa kuendelea na mjadala wa katiba wapigwe na jeshi na walazimishwe kujadili? Kwani jeshi ndilo lililowachagua wabunge wanaounda UKAWA?

Vipi jeshi likiunga mkono upande mmoja wananchi waliouingiza upande mwingine kwenye hiyo nafasi watakuwa wametendewa haki gani na jeshi linaloitwa JESHI LA WANANCHI?

Mwisho nishauri tu watu tupungize jazba maana hakuna vita kiasi kwamba sasa tuanze kufikiria matumizi ya jeshi.

NB Mwanajeshi anaweza kuwa mkereketwa wa siasa ila hii haimaanishi jeshi lina siasa.
Hapa namaanisha kama mwanajeshi ni mkereketwa wa CDM, CCM, CUF nk haimaanishi jeshi ni la chadema au ccm au Cuf!

Muda mwema!
 
Kwani kuilinda katiba unaelewaje mkuu?
Mimi nachojua jeshi kuilinda katiba si kufanya maamuzi juu ya utendaji wa kawaida wa viongozi.

Katiba ni sheria mama kwa hiyo jeshi hutekeleza wajibu kulingana na sheria na taratibu zilivyo za nchi na hii ndiyo kulinda katiba yenyewe.

Kumbuka jeshi ni moja kati taasisi nyeti na zinazoongozwa si kwa mihemuko ya kisiasa kama zilivyo taasisi nyingine za kawaida.

Jeshi lina kitabu chake kiitwacho JUZUU kama sijasahau. Humo zipo sheria zote za nchi na sheria za kijeshi hivyo utaratibu unaotumika jeshini wote unapatikana humo.

Kwenye kitabu hicho ndimo kwenye maandishi yanayoainisha maamuzi ambayo yatafikiwa endapo tukio fulani litatokea mf

1.Kama nchi ikivamiwa na nchi nyingine ni utaratibu gani unatakiwa ufuatwe?

2. Ni wakati gani ambapo raisi anaweza kutangaza hali ya hatari na akifanya hivyo jeshi linatakiwa litekelezeje?

3. Ni wakati gani ambapo jeshi linaweza kuchukua jukumu la kuondoa uongozi kwenye madaraka. Na mengine mengi kama hayo.

Ni vizuri kufahamu mambo haya:
Wananchi ndiyo walio iingiza serikali madarakani na pia ndio waliochagua wawakilishi wao wa kuwawakilisha bungeni. Na hii ni kutokana na haki ya kidemokrasia ambayo ni kipengele kimojawapo kwenye hiyo katiba.
Hivyo basi kwakuwa jeshi kazi yake ni pamoja na kuilinda katiba lazima iheshimu wawakilishi wote wa wananchi (Viongozi + wabunge ) bila kupendelea.

Kama pande hizi mbili hazikubaliani kwa hoja bado jeshi halina mamlaka ya kuingilia mpaka wenyewe watakapo patana au kuondolewa na wananchi kwenye nyadhifa hizo kwa njia ileile ya kidemokrasia.

Kulifikiria jeshi kwa maswala ya kisiasa sidhani kama ni njia muhimu ya kufikia malengo yaliyo tarajiwa.

Mwisho naomba nikuulize maswali mtoa mada,
Ulitaka labda jeshi liingilieje mchakato wa katiba?

Kwakuwa serikali imeweka msimamo wake itolewe madarakani kwani jeshi ndilo lililoiweka kwenye madaraka?

Kwakuwa UKAWA wamekataa kuendelea na mjadala wa katiba wapigwe na jeshi na walazimishwe kujadili? Kwani jeshi ndilo lililowachagua wabunge wanaounda UKAWA?

Vipi jeshi likiunga mkono upande mmoja wananchi waliouingiza upande mwingine kwenye hiyo nafasi watakuwa wametendewa haki gani na jeshi linaloitwa JESHI LA WANANCHI?

Mwisho nishauri tu watu tupungize jazba maana hakuna vita kiasi kwamba sasa tuanze kufikiria matumizi ya jeshi.

NB Mwanajeshi anaweza kuwa mkereketwa wa siasa ila hii haimaanishi jeshi lina siasa.
Hapa namaanisha kama mwanajeshi ni mkereketwa wa CDM, CCM, CUF nk haimaanishi jeshi ni la chadema au ccm au Cuf!

Muda mwema!

Mkuu Daddo umefafanua kwa ufasaha sana kwa mleta mada na wale ambao walikuwa hawajui, ila si vibaya nikaongezea kidogo kwamba, jeshi kuilinda katiba pia ina maana kuwa jeshi linatekeleza yale ambayo tayari mlishakubaliana kwa pamoja kama wananchi lakini siyo kuingilia mchakato wenu ktk kuboresha au kutengeneza mambo yenu. Jeshi linalinda yale mliyokubaliana, ndiyo maana linaitwa jeshi la wananchi
 
Mkuu Daddo umefafanua kwa ufasaha sana kwa mleta mada na wale ambao walikuwa hawajui, ila si vibaya nikaongezea kidogo kwamba, jeshi kuilinda katiba pia ina maana kuwa jeshi linatekeleza yale ambayo tayari mlishakubaliana kwa pamoja kama wananchi lakini siyo kuingilia mchakato wenu ktk kuboresha au kutengeneza mambo yenu. Jeshi linalinda yale mliyokubaliana, ndiyo maana linaitwa jeshi la wananchi

Nimependa sana mlivyojibu vizuri! Niongezee kuainisha majukumu us jeshi ni haya yafuatayo; 1)kumwangamiza adui atakayevamia mipaka ya nchi yetu ardhini, angani, au majini
2)kulinda mipaka ya nchi yeti
3)kusaidia mamlaka za kiraia katika maafa mbalimbali yakitokea
4)kusaidia kurejesha amani ikitokea fujo ndani ya nchi.

Katika kutekeleze hayo watahakikisha katiba ya nchi haivunjwi!

Asanteni
 
Back
Top Bottom