Kabudi na Lukuvi hawapo kwenye mfumo rasmi wa shughuli za serikali. Ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi

Kabudi na Lukuvi hawapo kwenye mfumo rasmi wa shughuli za serikali. Ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi

MGOGOHALISI

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2011
Posts
3,294
Reaction score
4,920
Hii tunarudia kumwambia raisi Samia na washauri wake (ambao katika hili sioni kama walimshauri) kuwa kama ulishaamua kuwatema hawa watu basi endelea na msimamo wako. Ni hiari ya raisi kuteua na kutengua wala halazimishwi. Ila inapotokea kelele za nje kuonekana tishio kwa maamuzi yake asitumie pesa za umma kuzima hizo kelele.

Serikali ina mifumo rasmi ya kazi na kuajiri. Kama raisi alishaona Kabudi na Wengine hawafai kuendelea nae angewaacha tu kwa sababu ile ile aliyoisema hadharani.

Lakini sasa tunawaona hawa watu wakiendelea kutumia mali ya umma huku nafasi zao zikiwa hazieleweki serikalini. Haya ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi. Sio lazima Kabudi na Lukuvi waendelee kuwepo viunga vya ikulu. Kwanza ni wabunge wenye majimbo yao. Wanaweza kuendelea kuwatumikia wananchi huko majimboni.

Huu usemi wa kusema eti una kazi maalumu wakati sababu ya kubadili baraza ilishajulikani isiwe sababu ya kutumia kodi zetu vibaya. Namaliza kwa kusema Lukuvi na Kabudi sio lazima waendelee kuwepo viunga vya ikulu. Ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi, ni kuwapotezea muda kutumika majimboni kwao.
 
843DCCE9-4C40-43F1-8C53-971D4DC599DC.jpeg
 
Mwanzoni tulijua kuwa hao wawili walipumzishwa ili wapate nafasi ya kujiandaa. Baadae wamekaribishwa sebuleni. Sasa wanaoenda kujiamdaa ni kina nani
 
Ninacho kiona ni uoga alionao kutoka kwa Lukuvi kwenye chaguzi za ndani ya chama na nje ya chama.
 
Upande mmoja chief hangaya anaongoza nchi asiyo ijua vyema ... amekuwa bara kitambo lakini kwa majukumu mahususi sio general hajui utamaduni wa kila eneo.... hata aina ya watu anaowaongoza hawajui.

Ana struggle kuongoza wakati huo anahofu ya kupoteza. Anajaribu kupunguza nguvu ya kila anaemuona ni tishio kwake. Ukiangalia kwa jicho la tatu hata kesi ya mbowe ni mkakati wa uoga wake. Mikopo ni uoga, tengua tengua ya kina Lukuvi yote ni muendelezo wa uoga. Speaker Ndugai ni uoga. Kuwaingiza JK company nk. Hatuitaji rais wa aina hii kwa sasa hana muda wa kuangalia maslahi ya nchi zaidi ya kulinda kiti.

Kibaya zaidi ameruhusu hisia kuongoza akili... hii ina maana gani... mosi hana muda wa kutafakari wala kupata ushauri kwa watu tofauti kuhusu nani amsaidie nini na wapi.. technical know how.

Ukiangalia teuzibzake unabaki kushangaa tu mfano Tume ya madini kumweka Janeth Ruben (former Barrick HR manager) kuwa mkuu wa tume ni ujinga wa mwaka... hana uwezo wa kuleta mabadiliko chanya kwenye sector.

Kumuondoa Prof Manya pia ni kudhindwa kuelewa watu gani wakusaidie nini wapi. Huu ni mfano mdogo tu wa kushindwa kufanya maamuzi sahihi.
 
Hii tunarudia kumwambia raisi Samia na washauri wake (ambao katika hili sioni kama walimshauri) kuwa kama ulishaamua kuwatema hawa watu basi endelea na msimamo wako...
Hata hivyo sijaona wakiapa/ kuthibitisha kutumikia cheo chochote. Na bado sifahamu ni majukumu gani rasmi waliyopewa! Siasa za nchi hii ni kama series za filamu za kimarekani au kikorea.
 
Mimi nimependa hili wazo la mama kuwa na watu independent watakaomshauri maswala mbalimbali, kwenye hili jopo la watu,Angeweka na watu wa diaspora as well
 
Back
Top Bottom