Kafanikiwa kuacha Pombe,Bange,Sigara toka mwaka 1999

Kafanikiwa kuacha Pombe,Bange,Sigara toka mwaka 1999

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,106
Reaction score
12,916
Ni ndugu yangu.
Nilihangaika nae mpaka watu wakanishangaa,lakini haya niliyafanya ili wazee{wazazi}wasilemewe na mzigo.
Dogo huyu kwa sasa ni mtu mzima mwenye maisha yake ,alianza kidogo kidogo kunywa mbege wakati wa krismasi huko Moshi,akiwa darasa la tatu.
kabla ya kumaliza darasa la saba akawa tayari kushamudu bia n.k.
Form four bange, gongo n.k.
anamaliza chuo ni cha P
akapata kazi nzuri siku akilipwa anapotea wiki nzima ulevi ulevi ulevi.
kazini hadumu wanamtema,lakini cha ajabu huwa hakai kijiweni(bila kazi zaidi ya miezi 2-3)
Ana bahati sana ya kupata kazi lakini hadumu,kazunguka makampuni mengi nchi hii ya Tanzania.
Rafiki zake wamemzungusha kwa waganga wengi lakini haikusaidia kitu.
Akapata kazi shirika fulani la wazungu...wazungu wakampenda sana...wakaamua kumsaidia,manake kwa kazi jamaa ni jembe na ni kichwa hasa....lakini akigusa pombe tu;ni mtihani atataka kunywa na kunywa na kuvuta mpaka aishiwe tena anauza hata vitu vyake ili tu akalewe,Basi wazungu waka mpeleka 'sober house' mara kadhaa lakini haikusaidia.
Ameshazunguka kwenye makanisa ya mboga mboga na yasiyo ya mboga mboga.
watu wooote walimtenga ndugu jamaa na marafiki.
ALIPONAJE?
Kuna Mchungaji mmoja alituambia kwamba ulevi ni ugonjwa kama yalivyo magonjwa mengine.na matibabu yapo.......akaamua kutusaidia.
Akatufafanulia kwamba ugonjwa huu ni wa kiroho,kwa hiyo dawa yake ni 'spiritual healing'....
Basi akaamua kukaa nae na ndipo uponyaji ulivyo patikana toka mwaka 1999 wakati wa maombolezo ya Mwl.Nyerere mpaka Leo hii jamaa hayagusa kabisa,na mambo yake ni mazuri.
 
Samahani mkuu, tunaeza kuwasiliana...nina shida kama hii...tafadhali ukipata ujumbe huu tuwasiliane.
 
Ni ndugu yangu.
Nilihangaika nae mpaka watu wakanishangaa,lakini haya niliyafanya ili wazee{wazazi}wasilemewe na mzigo.
Dogo huyu kwa sasa ni mtu mzima mwenye maisha yake ,alianza kidogo kidogo kunywa mbege wakati wa krismasi huko Moshi,akiwa darasa la tatu.
kabla ya kumaliza darasa la saba akawa tayari kushamudu bia n.k.
Form four bange, gongo n.k.
anamaliza chuo ni cha P
akapata kazi nzuri siku akilipwa anapotea wiki nzima ulevi ulevi ulevi.
kazini hadumu wanamtema,lakini cha ajabu huwa hakai kijiweni(bila kazi zaidi ya miezi 2-3)
Ana bahati sana ya kupata kazi lakini hadumu,kazunguka makampuni mengi nchi hii ya Tanzania.
Rafiki zake wamemzungusha kwa waganga wengi lakini haikusaidia kitu.
Akapata kazi shirika fulani la wazungu...wazungu wakampenda sana...wakaamua kumsaidia,manake kwa kazi jamaa ni jembe na ni kichwa hasa....lakini akigusa pombe tu;ni mtihani atataka kunywa na kunywa na kuvuta mpaka aishiwe tena anauza hata vitu vyake ili tu akalewe,Basi wazungu waka mpeleka 'sober house' mara kadhaa lakini haikusaidia.
Ameshazunguka kwenye makanisa ya mboga mboga na yasiyo ya mboga mboga.
watu wooote walimtenga ndugu jamaa na marafiki.
ALIPONAJE?
Kuna Mchungaji mmoja alituambia kwamba ulevi ni ugonjwa kama yalivyo magonjwa mengine.na matibabu yapo.......akaamua kutusaidia.
Akatufafanulia kwamba ugonjwa huu ni wa kiroho,kwa hiyo dawa yake ni 'spiritual healing'....
Basi akaamua kukaa nae na ndipo uponyaji ulivyo patikana toka mwaka 1999 wakati wa maombolezo ya Mwl.Nyerere mpaka Leo hii jamaa hayagusa kabisa,na mambo yake ni mazuri.
Naomba namba za huyu mchungaji tunahitaji msaada km huu kibinafsi na familia.
 
Naomba namba za huyu mchungaji tunahitaji msaada km huu kibinafsi na familia.
0717457679 ni mzungu lakini anafahamu kiswahili....ukimpata tupe mrejesho kwa faida ya wengine...jina Anaitwa Louis Boutier ni mspanish....na anasaidia bure...ni mmisionari... chakula na sehemu ya kulala ipo..pia wanafundisha kazi/ fani mbalimbali....wanashughuli nyingi za uzalishaji ili kuendesha kituo...pia misaada mingi yatoka mamtoni....wana connection sana wengi wamesafiri.
 
0717457679 ni mzungu lakini anafahamu kiswahili....ukimpata tupe mrejesho kwa faida ya wengine...jina Anaitwa Louis Boutier ni mspanish....na anasaidia bure...ni mmisionari... chakula na sehemu ya kulala ipo..pia wanafundisha kazi/ fani mbalimbali....wanashughuli nyingi za uzalishaji ili kuendesha kituo...pia misaada mingi yatoka mamtoni....wana connection sana wengi wamesafiri.
Wako wapi
 
Au piga 0754 320084, yupo Kawe dsm, anaitwa Mwamposa. Anaombea bure na Yesu ameponya wengi kupitia Mwamposa.
 
Back
Top Bottom