Kafulila chapa kazi usitolewe kwenye reli na wapigaji

Kafulila chapa kazi usitolewe kwenye reli na wapigaji

Mtumishiwetu

Senior Member
Joined
Jul 13, 2022
Posts
196
Reaction score
346
Kwa muda mfupi ambacho Kafulila ameongoza Mkoa wa Simiyu tumeshuhudia mageuzi makubwa ikiwemo kumtaka Mkandarasi aliyejenga barabara ya Maswa- Mwigumbi chini ya kiwango kuirudia kwa gharama zake jambo ambalo watangulizi wake hawakuliona kama ni tatizo.

Kafulila amesimamia nidhamu ya ukusanyaji wa mapato kwenye Halmashauri za Mkoa wa Simiyu na kuondoa yale mazoea ya kuzigeuza halmashauri shamba la bibi fedha zinaliwa na watu wachache leo Halmashauri zote zimepaa makusanyo yake ndani ya muda mfupi wa uongozi wake na fedha nyingi zinakwenda kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi.

Sijui watangulizi wake kwanini hawakusimamia hayo, leo tunaona Kafulila anafanya ziara kwenda kwenye vijiji kukagua shughuli za maendeleo na kusikiliza na kutatua kero za wananchi jambo ambalo wananchi walizoea kuwaona viongozi wa Mkoa kwenye matukio ya ziara za viongozi wa kitaifa Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au Rais.

Kuna wahuni wameanza kujitokeza humu kumkatisha tamaa Kafulila kwa mwendelezo uleule wa kutaka akae tu ofisini asishughulike na matatizo ya wananchi na kusimamia makusanyo ya fedha za Serikali
 
CCM ni wanafiki sana .Mtaka kabla ya kuja Dodoma alikuwa Simiyu na mlisema ndiye RC bora kabisa kuwahi kutokea nchini.na kuwa Simiyu ni mfano wa kuigwa ,leo tunaambiwa mtangulizi wa kafulila hakufanya kitu.
Nadhani twende kwenye case by case tusiende kijumla jumla sana Tumeonyesha mageuzi aliyofanya Kafulila, ni vizuri kama unataka kulinganisha na mwingine ueleze hayo aliyoyafanya ya kimageuzi kama yaliyotajwa kwa Kafulila tusiende kama upepo
 
Tukumbushane,
Wakati mijadala mingine ikiendelea kama kawa,
AGENDA kuu Kwa sasa nchini ni KATIBA mpya.
Mzee ateuliwe, AAPISHWE amalizie KAZI.
RASIMU alosimamia Judge WARIOBA irudi mezani mjadala uanzie hapo.
Amen
 
Tukumbushane,

Wakati mijadala mingine ikiendelea kama kawa,

AGENDA kuu Kwa sasa nchini ni KATIBA mpya.

Mzee ateuliwe, AAPISHWE amalizie KAZI.

RASIMU alosimamia Judge WARIOBA irudi mezani mjadala uanzie hapo.

Amen
Mjadala wa Katiba tutaujadili kwa kina wakati mchakato wake utakapoanza, kwa sasa hoja zinazoendelea na kuwajibika kwa viongozi wetu kutoka ngazi ya Kijiji, Kata, Jimbo, Wilaya, Mkoa na Taifa ili kukabiliana na changamoto za sasa zinazolikabili taifa letu
 
Nadhani twende kwenye case by case tusiende kijumla jumla sana Tumeonyesha mageuzi aliyofanya Kafulila, ni vizuri kama unataka kulinganisha na mwingine ueleze hayo aliyoyafanya ya kimageuzi kama yaliyotajwa kwa Kafulila tusiende kama upepo
Mnatuona sisi mazuzu sana ,nyie ndio mnatakiwa mtuombe radhi kuwa mlitudanganya kuhusu Mtaka,au mnatudanganya kuhusu Kafulila
 
Arudi kwenye chama chake, hiyo ni nafasi ya mwana CCM, yeye ni chasaka
 
Mjadala wa Katiba tutaujadili kwa kina wakati mchakato wake utakapoanza, kwa sasa hoja zinazoendelea na kuwajibika kwa viongozi wetu kutoka ngazi ya Kijiji, Kata, Jimbo, Wilaya, Mkoa na Taifa ili kukabiliana na changamoto za sasa zinazolikabili taifa letu
Amka uangaze,

Mchakato wa KATIBA mpya Si wa kesho kwamba tunausubiri.

Mchakato ulikwama Mahali,

Tunaukwamua.
 
Tunataka katiba mpya ipatikane kwanza ilinde wachapakazi wote!
Na kuwa mwiba KWA mafisadi WOTE!
Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA!
 
HUYU ndio Aliwalipuwa Watu sijui ESCROW AU Richmond kama ndio Dawa yake ipo jioni wenye Ccm yao wameishika
 
CCM ni wanafiki sana .Mtaka kabla ya kuja Dodoma alikuwa Simiyu na mlisema ndiye RC bora kabisa kuwahi kutokea nchini.na kuwa Simiyu ni mfano wa kuigwa ,leo tunaambiwa mtangulizi wa kafulila hakufanya kitu.
CCM imejaa washirikina na majangili
 
Wewe ni mke wa Kafulila hivyo lazima umsifie mumeo, hakuna cha maana anafanya zaidi ya usanii na kutaka kujitangaza
 
CCM ni wanafiki sana .Mtaka kabla ya kuja Dodoma alikuwa Simiyu na mlisema ndiye RC bora kabisa kuwahi kutokea nchini.na kuwa Simiyu ni mfano wa kuigwa ,leo tunaambiwa mtangulizi wa kafulila hakufanya kitu.
Kabisa..
Inawezekana mtoa mada ndo Kafulila mwenyewe akijipigia promo muda mchache kabla ya kupigwa pini!
 
Back
Top Bottom