Kafulila: Huenda tuna kizazi bora zaidi kaburini kuliko hiki kilichopo leo duniani

Kafulila: Huenda tuna kizazi bora zaidi kaburini kuliko hiki kilichopo leo duniani

ISRAEL JR

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2013
Posts
1,523
Reaction score
758
Nimekutana na hii Clip ya Kafulila sijui ni ya lini na alikuwa katika tukio gani sifahamu ila nimevutiwa na hekima za hotuba yenyewe.

Katika video hii Kafulila anasema hapa duniani tuna kizazi bora zaidi kilichopo kaburini kuliko hiki kinachoishi duniani leo.

Ukisikiliza vizuri hiyo Clip Kafulila anasema, Leo tuna kizazi ambacho wazee wanahitaji kuwezeshwa kwa sababu ya uzee wao kwani wameishiwa nguvu.

Leo wanawake nao wanahitaji kuwezeshwa kwa sababu wao ni wanawake na mbaya zaidi vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa nao wanahitaji kuwezeshwa kwa sababu wao ni vijana.

Kafulila anahoji, Kipo wapi kizazi kile ambacho kijana alichukua panga, shoka na jembe ili kuukabili msitu kujitajirisha na ikiwa Serikali itakuja itamkuta ametangulia shambani?

Kafulila anashanga leo kuna majengo ya Serikali maeneo mbali mbali yalijengwa miaka ya 1960 hata kabla ya Uhuru au miaka ya 1970 wakati wahandisi wa ujenzi wakiwa wachache kabisa.

Kafulila anashanga zaidi majengo hayo ya zamani kabisa leo yanapakwa rangi tu ili kusafisha kuta lakini leo majengo mengi ya madarasa na majengo mbalimbali ya Serikali yanayojengwa na Watanzania wenyewe hayadumu.

Leo, majengo mengi baada ya miaka mitano au kumi tu yanakuwa yamejaa nyufa Kila sehemu wakati leo ndio wakati ambao wahandisi wa Kitanzania wa Ujenzi wamejaa nchini"

Huenda ni kweli kizazi kilichopo kaburini kiliipenda zaidi Tanzania kuliko kizazi hiki tunachoishi kwani ni kizazi kinachotanguliza masilahi yao zaidi kuliko masilahi ya Taifa.

FIKIRI, LEO JENGO LA MWAKA 1960 HALINA NYUFA ILA JENGO LA MWAKA 2000 LIMEJAA NYUFA TUJITAKARI KAMA TAIFA.
 
Nimekutana na hii Crip ya Kafulila sijui ni ya lini na alikuwa katika tukio gani sifahamu ila nimevutiwa na hekima za hotuba hii,

Katika video hii Kafulila anasema hapa duniani tuna kizazi bora zaidi kilichopo kaburini kuliko kuliko hiki kinachoishi duniani.

Ukisikiliza vizuri hiyo Crip Kafulila anasema, Leo tuna kizazi ambacho wazee wanahitaji kuwezeshwa kwasababu ya uzee wao kwani wameishiwa nguvu.

Leo wanawake nao wanahitaji kuwezeshwa kwasababu wao ni wanawake na mbaya zaidi vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa nao wanahitaji kuwezeshwa kwasababu wao ni vijana.

Kafulila anahoji, Kipo wapi kizazi kile ambacho kijana alichukua panga, shoka na jembe ili kuukabili msitu kujitajirisha na ikiwa Serikali itakuja itamkuta ametangulia shambani?

Kafulila anashanga Leo kuna majengo ya Serikali maeneo mbali mbali yalijengwa miaka ya 1960 hata kabla ya uhuru au miaka ya 1970 wakati wahandisi wa ujenzi wakiwa wachache kabisa,

Kafulila anashanga zaidi majengo hayo ya zamani kabisa leo yanapakwa rangi tu ili kusafisha kuta lakini leo majengo mengi ya madarasa na majengo mbalimbali ya Serikali yanayojengwa na Watanzania wenyewe hayadumu.

Leo, majengo Mengi baada ya miaka mitano au kumi tu yanakuwa yamejaa nyufa Kila sehemu wakati leo ndio wakati ambao wahandisi wa Kitanzania wa Ujenzi wamejaa nchini"

Huenda ni kweli kizazi kilichopo kaburini kiliipenda zaidi Tanzania kuliko kizazi hiki tunachoishi kwani ni kizazi kinachotanguliza masilahi yao zaidi kuliko masilahi ya Taifa.

KIFIRI, LEO JENGO LA NWAKA 1960 HALINA NYUFA ILA JENGO LA MWAKA 2000 LIMEJAA NYUFA TUJITAKARI KAMA TAIFA.

= clip

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Ni siasa tu...
Maneno mengi na matamu, ila vitendo vuchungu.

Mwambie akemee viongozi wa CCM waache ufisadi.
Na kishindwa kufanya hivyo, ajiuzulu, na aje huku tukamate mashamba tujiandae kusubiri serikali ituunge mkono.
KWANI HUONI ATA PALE CHADEMA?

MZEE MAKANI ALIANZISHA CHAMA ILA BAADA YA MIAKA 10 AKANG'ATUKA,

LEO MBOWE ANATAKA KUFIA UONGOZINI,

KAFULILA IS VERY RIGHT.
 
Nimekutana na hii Crip ya Kafulila sijui ni ya lini na alikuwa katika tukio gani sifahamu ila nimevutiwa na hekima za hotuba hii,

Katika video hii Kafulila anasema hapa duniani tuna kizazi bora zaidi kilichopo kaburini kuliko kuliko hiki kinachoishi duniani.

Ukisikiliza vizuri hiyo Crip Kafulila anasema, Leo tuna kizazi ambacho wazee wanahitaji kuwezeshwa kwasababu ya uzee wao kwani wameishiwa nguvu.

Leo wanawake nao wanahitaji kuwezeshwa kwasababu wao ni wanawake na mbaya zaidi vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa nao wanahitaji kuwezeshwa kwasababu wao ni vijana.

Kafulila anahoji, Kipo wapi kizazi kile ambacho kijana alichukua panga, shoka na jembe ili kuukabili msitu kujitajirisha na ikiwa Serikali itakuja itamkuta ametangulia shambani?

Kafulila anashanga Leo kuna majengo ya Serikali maeneo mbali mbali yalijengwa miaka ya 1960 hata kabla ya uhuru au miaka ya 1970 wakati wahandisi wa ujenzi wakiwa wachache kabisa,

Kafulila anashanga zaidi majengo hayo ya zamani kabisa leo yanapakwa rangi tu ili kusafisha kuta lakini leo majengo mengi ya madarasa na majengo mbalimbali ya Serikali yanayojengwa na Watanzania wenyewe hayadumu.

Leo, majengo Mengi baada ya miaka mitano au kumi tu yanakuwa yamejaa nyufa Kila sehemu wakati leo ndio wakati ambao wahandisi wa Kitanzania wa Ujenzi wamejaa nchini"

Huenda ni kweli kizazi kilichopo kaburini kiliipenda zaidi Tanzania kuliko kizazi hiki tunachoishi kwani ni kizazi kinachotanguliza masilahi yao zaidi kuliko masilahi ya Taifa.

KIFIRI, LEO JENGO LA NWAKA 1960 HALINA NYUFA ILA JENGO LA MWAKA 2000 LIMEJAA NYUFA TUJITAKARI KAMA TAIFA.
View attachment 3031137
Chawa tu, anasanifu watu. Yeye ndio miongoni mwa watu wa hovyo anayewaza tumbi lake kwa kupiga uchawa ili mama amuone.
 
Ukitetea kulindana kwenye mambo yafanyikayo kiholela nchi inafikia hapo ilipo.
Hakuna ubora kwenye kila jambo.
Hakuna uwajibikaji.
Kila mtu anajali tumbo lake na watoto wake tu.
Ndio maana Kafulila anataka Uzalendo zaidi
 
Asante sana mkuu ni typing error tu
Hapana, hizzo siyo typing error, huo ni ujinga wa kuchanganya R na L

Tazama R iko wapi na L iko wapi, hata iwe typing error?

Danganya wajinga wengne siyo mimi.

Typo nazifahamu vilivyo na ujinga wa kuchanganya R na L naufahamu vilivyo.

Huwa sikosi "typing errors" nakosoa huo ujinga wa kuchanganya R na L. Kumbuka hilo.
 
Sijui kwanini mama hajamchukua huyu ampe uwaziri mbona angemsaidia sana
 
Hapana, hizzo siyo typing error, huo ni ujinga wa kuchanganya R na L

Tazama R iko wapi na L iko wapi, hata iwe typing error?

Danganya wajinga wengne siyo mimi.

Typo nazifahamu vilivyo na ujinga wa kuchanganya R na L naufahamu vilivyo.

Huwa sikosi "typing errors" nakosoa huo ujinga wa kuchanganya R na L. Kumbuka hilo.
Nashukuru kwa maoni yako
 
Back
Top Bottom