Kafulila: Rais Mkapa alijutia kuiua PSRC Parastatal Sector Reform Commission, PPP haiuzi Mali za Umma bali inazilinda kwa kipindi chote cha mkataba

Kafulila: Rais Mkapa alijutia kuiua PSRC Parastatal Sector Reform Commission, PPP haiuzi Mali za Umma bali inazilinda kwa kipindi chote cha mkataba

Jabali la Siasa

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2020
Posts
2,823
Reaction score
2,466
IMG-20241031-WA0156(2).jpg


Hiki ndicho alichoandika Director wa PPP Tanzania Bw. David Kafulila huko kwenye akaunti yake ya X zamani tweeter.

Mkurugenzi huyo ameandika haya ili kuwatoa hofu wanaodhani huenda nchi yetu ikapata hasara ya mali na fedha kwa kuingia Ubia na Sekta binafsi toka ndani au nje ya Tanzania.

KAFULILA anarejelea Serikali ya awamu ya tatu Chini ya Hayati Rais Dkt. Benjamin Mkapa ambae katika kitabu chake Cha "My Life My Purpose " anasema baada ya kuuza mali za Umma kwa ubinafsishaji yakiwemo mashirika makubwa kama NBC kwa kupitia PSRC yaani Parastatal Sector Reform Commission anakiri alifanya makosa kuifuta tume hiyo ili ifanye ufuatiliaji wa mali zake zote ilizozifanyia ubinafshaji jambo lililozaa watu kuchukua mali za umma na kuzibadilishia matumizi, kukopea benki na uharibifu mwingine mwingi.

Kafulila anasema kwenye PPP Serikali na Sekta binafsi watamiliki mradi kwa pamoja na Serikali itakuwa ndio mwangalizi mkuu wa mradi kwa muda wote wa Mkataba na hii ndio tofauti kati ya Ubinafsishaji wa kipindi cha awamu ya tatu na Ubinafsishaji huu wa awamu ya sita kwa njia salama ya PPP.

Kafulila anasema PPP haiuzi mali za umma kama ilivyokuwa kwa PSRC bali inakodisha kwa kipindi maalum na baada kukodisha Serikali haiondoki kwenye mradi kwa kipindi chote cha Mkataba.

Na kwa ile miradi mipya itakayojengwa kwa Ubia kama zile Hosteli pale CBE baada ya muda wa Ubia kuisha miradi ile inarudi kuwa mali ya Serikali kwa asilimia 100.

Hata hivyo, ingawa haimaanishi Ubinafsishaji wa awamu ya tatu lilikuwa ni jambo baya hapana kwani ilikuwa ni njia sahihi ya kujenga Uchumi wa kisasa "modern economy" lakini matatizo hayawezi kuisha kabisa ila uamuzi wa Mzee Benjamin Mkapa wa ubinafshaji umekuwa na faida nyingi kuliko hasara Leo.


Pia soma Kwani Tulifeli vipi kwenye Ubinafsishaji wa Awamu ya 2 hadi Tufaulu sasa kwenye PPP ya David Kafulila?

______
 
View attachment 3140086

Hiki ndicho alichoandika Director wa PPP Tanzania kuwatoa hofu wanaodhani nchi itapata hasara kwa kuingia Ubia na sekta binafsi toka ndani au nje ya nchi.

Pia soma Kwani Tulifeli vipi kwenye Ubinafsishaji wa Awamu ya 2 hadi Tufaulu sasa kwenye PPP ya David Kafulila?
Tatizo Kafulila hajui kitu chochote kile kuhusu masuala haya ya Miradi ya PPP hapa Tanzania. Mpaka Sasa, Serikali ya Tanzania tayari imeingia Mikataba mingi tu ya Miradi ya PPP kabla hata Rais Magufuli na Samia waingie madarakani, Je, huyo Kafulila ameshawahi kujiuliza kwamba nchi hii imekuwa ikinufaika Nini na hiyo Miradi ya PPP???

Tayari kuna Mikataba mingi ya Miradi ya PPP kati ya Tz na Makampuni mbalimbali kutoka nchini China, Je, Tanzania mpaka Sasa inanufaika nini kutokana na kuwepo kwa Miradi hiyo ya Ubia Kati ya Tz na China?? Kwanza huyo Kafulila mpaka Sasa anaijua Miradi hiyo ya Ubia ambayo tayari ipo kwenye utekelezaji tangu miaka mingi iliyopita??

Kafulila aache kupiga Domo na kupiga Propaganda za Siasa kuhusu suala hili la Miradi ya Ubia Kati ya Serikali na Sekta Binafsi, kwani hili ni suala gumu ambalo liko nje ya uwezo wake wa akili, na hata kwenye hii Serikali iliyopo Hakuna Watu ambao wako competent enough wa kuweza kuli-handle suala hili la Ubia. Wengi waliopo hawana uelewa wa kutosha kuhusiana na masuala haya ya Ubia na jinsi Miradi ya Ubia inavyoweza kutekelezwa kwa kuzalisha faida.
 
View attachment 3140086

Hiki ndicho alichoandika Director wa PPP Tanzania kuwatoa hofu wanaodhani nchi itapata hasara kwa kuingia Ubia na sekta binafsi toka ndani au nje ya nchi.

Pia soma Kwani Tulifeli vipi kwenye Ubinafsishaji wa Awamu ya 2 hadi Tufaulu sasa kwenye PPP ya David Kafulila?
Tanzania hatuna uongozi wa kizalendo ndiyo maana wizi bado upo ambao tumelitengenezea neno fulani hivi, (ufisadi), watu wakiiba wanaundiwa tume ambazo zingine tangia ziundwe hazikuwahi kuleta majibu

Baada ya kusema hayo tutafute namna nzuri ya kuweka mambo yetu sawa ndiyo tuikaribisha ppp kwa mikono miwili kwa maneno mengine hadi Tanzania tuache tabia ya unyumbu wa kisiasa

Unnyumbu wa kisiasa ni tabia ya wanaopewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza, kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi na uoga kwa viongozi wao bila utii, (unafiki), a.k.a kujizima data, tuseme kuahirisha kufikiri kizalendo

Tafsiri ya unyumbu wa kisiasa kwa kimombo ni human herding in politics.

Human herding in politics is an occurrence of entrusted people suspending their individual reasoning because of flattering, working towards group objectives and fear of their leaders, (hypocrite)

Tume za kuchunguza ufisadi Tanzania zinaundwa nyuma ya mikamera lakini majibu ya tume nyuma ya pazia, (kwenye kijaruba),

Napenda kuwakumbusha wanao ziunda hizo tume kwamba tume ni kwaajili ya umma majibu lazima tuyafahamu, (Commission of inquiries are for the public interests)
 
Sheria ya PPP inataka ushirikishwaji wa mradi tangu mwanzo kabisa wa mradi
Kwa maneno mengine baada ya kuufahamu mradi vizuri kupitia andiko la mradi, (businesses plan), kama kuna marekebisho yafanyike ama kuyatolea ufafanuzi kablabya kuanza mradi
 
  • Thanks
Reactions: YAY
Kama PPP itahusika tangu mwanzo wa mradi mpaka mwisho wa mradi hilo nalipongeza ila kinachohitaji ni Uzalendo zaidi kwa Taifa lenu
Kwenye uwekezaji PPP ni nzuri ndio maana hata China wanaipenda
 
View attachment 3140086

Hiki ndicho alichoandika Director wa PPP Tanzania kuwatoa hofu wanaodhani nchi itapata hasara kwa kuingia Ubia na sekta binafsi toka ndani au nje ya nchi.

Pia soma Kwani Tulifeli vipi kwenye Ubinafsishaji wa Awamu ya 2 hadi Tufaulu sasa kwenye PPP ya David Kafulila?
Nashukuru

Kafulila yuko sahihi kabisa ila kwa Culture ya Watanzania ni Heri uimarishe sekta binafsi Ili upate Kodi kuliko hii PPP yenye mchanganyiko

Mifano ni TBL na Sigara 😄😄
 
Back
Top Bottom