Leo ndo Leo Uwanja mkuu wa taifa uliopo Dar Es Salaam, wale mabingwa wa Vodacom Premier League Young Africans Sports Club Watakipiga na timu ya Gor Mahia kutoka Kenya katika kombe la kagame, mchezo ambao unatarajiwa kutoa mwonekano wa timu ya Yanga baada ya usajili wao.
Katika mchezo huo timu zote zinaonekana kuwa ni bora hasa ukiangalia takwimu zao kwenye msimamo wa ligi zao.
Yanga imemaliza msimu katika ligi kuu ya Tanzania ikiwa nafasi ya kwanza ambapo ilifanikiwa kuvuna jumla ya pointi 55, katika michezo 26 iliyocheza imeshinda michezo 17, imefungwa michezo 5 na kutoa sare 4.
Wakati huo wapinzani wao Gor Mahia wanaongoza ligi nchini kenya wakiwa wamecheza mechi 18, wameshinda14, draw 4, na hawajapoteza mechi hata moja.
Hivyo, kwa takwimu hizo inaonyesha kuwa leo tutashuhudia kandanda safi na la kikubwa.
kila la kheri "Yanga"
Usikae mbali na jukwaa kwa updates za dakika 90 za mchezo huo.