Kagera: Makaburi zaidi ya 3600 kuhamishwa ili kupisha ujenzi wa kitega uchumi kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo

Kagera: Makaburi zaidi ya 3600 kuhamishwa ili kupisha ujenzi wa kitega uchumi kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Deo Ndejembi ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kuwasilisha ofisini kwake nyaraka inayoonesha ni wapi makaburi yanayopangwa kuhamishwa yanapelekwa.

Ndejembi ametoa maagizo hayo alipofika katika maeneo ya Makaburi ya Kishenge Manispaa ya Bukoba ambayo yanapangwa kuhamishwa kwa lengo la kupisha mradi wa ujenzi wa kitega uchumi kitakachoweza kuwaweka pamoja wafanyabiashara wadogo katika mji huo sambamba na kuwataka Manispaa kuwataarifu ndugu waliozika maeneo hayo kabla ya zoezi la kuhamisha kuanza.

Aidha amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga maeneo ya uwekezaji ili kuepusha kadhia ya kuanza kuhamisha makaburi huku akisisitiza sheria kuzingatiwa.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba na diwani wa kata ya Nshambya Mhe. Godson Gibson amesema kuwa makaburi hayo yapo hapo kwa zaidi ya miaka 50 na tayari wameshazui kuzika kwenye eneo hilo.

Amesema kuwa tayari kupitia Baraza la Madiwani wameshaku baliana kuhamishia makaburi hayo katika kata ya Buhembe ambako shughuli zote za mazishi zitakuwa zinafanyika huko.


Source: Wasafi FM
 
Kuhamisha makaburi yenye umri wa miaka mingi hapo ni kuhamisha mifupa tu. Ni ngumu kupata kiunzi kizima kwani mifupa yote itasambaa na kutoweza kuizika katika mpangilio wake uanze na fuvu, mbavu, miumdi. Itakuwa ni kuzika mifupa tu random. Washirikina hawatacheza mbali kupata material ya kufanyia ushirikina wao
 
Sasa kama makaburi yalijengewa ina maana huko yatakapohamishwa mengine hayatajengewa tena. Kuna makaburi yatakosa ndugu na kuna uwezokano wa mifupa mingi mchanganyiko kuzikwa katika kaburi moja. Kwanza uchimbaji wa makaburi mengi kwa wakati mmoja ni shughuli pevu, uzikaji utakuwa ni wa hovyo usio na heshima kama walevi na wahuni watapewa kufanya shughuli hiyo. Haya makaburi yana taratibu zake za kuyafukua kulingana na mila za wenye makaburi. Kuna wengine hufanya kwanza ibada za kimila kwa kuchinja kondoo, kumwaga pombe, kuvuta bangi kwa wafukuaji na mambo mengine mengi ya kienyeji hufanyika. Vinginevyo wasipozingatia mambo ya kienyeji watakutana na mizimu na hilo jengo litapata changamoto kwa kujengwa yalipokuwa makaburi. Si vizuri sana kusumbua wafu waliolala kwenye nyumba zao hizo
 
Back
Top Bottom