Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Deo Ndejembi ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kuwasilisha ofisini kwake nyaraka inayoonesha ni wapi makaburi yanayopangwa kuhamishwa yanapelekwa.
Ndejembi ametoa maagizo hayo alipofika katika maeneo ya Makaburi ya Kishenge Manispaa ya Bukoba ambayo yanapangwa kuhamishwa kwa lengo la kupisha mradi wa ujenzi wa kitega uchumi kitakachoweza kuwaweka pamoja wafanyabiashara wadogo katika mji huo sambamba na kuwataka Manispaa kuwataarifu ndugu waliozika maeneo hayo kabla ya zoezi la kuhamisha kuanza.
Aidha amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga maeneo ya uwekezaji ili kuepusha kadhia ya kuanza kuhamisha makaburi huku akisisitiza sheria kuzingatiwa.
Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba na diwani wa kata ya Nshambya Mhe. Godson Gibson amesema kuwa makaburi hayo yapo hapo kwa zaidi ya miaka 50 na tayari wameshazui kuzika kwenye eneo hilo.
Amesema kuwa tayari kupitia Baraza la Madiwani wameshaku baliana kuhamishia makaburi hayo katika kata ya Buhembe ambako shughuli zote za mazishi zitakuwa zinafanyika huko.
Source: Wasafi FM
Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Deo Ndejembi ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kuwasilisha ofisini kwake nyaraka inayoonesha ni wapi makaburi yanayopangwa kuhamishwa yanapelekwa.
Ndejembi ametoa maagizo hayo alipofika katika maeneo ya Makaburi ya Kishenge Manispaa ya Bukoba ambayo yanapangwa kuhamishwa kwa lengo la kupisha mradi wa ujenzi wa kitega uchumi kitakachoweza kuwaweka pamoja wafanyabiashara wadogo katika mji huo sambamba na kuwataka Manispaa kuwataarifu ndugu waliozika maeneo hayo kabla ya zoezi la kuhamisha kuanza.
Aidha amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga maeneo ya uwekezaji ili kuepusha kadhia ya kuanza kuhamisha makaburi huku akisisitiza sheria kuzingatiwa.
Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba na diwani wa kata ya Nshambya Mhe. Godson Gibson amesema kuwa makaburi hayo yapo hapo kwa zaidi ya miaka 50 na tayari wameshazui kuzika kwenye eneo hilo.
Amesema kuwa tayari kupitia Baraza la Madiwani wameshaku baliana kuhamishia makaburi hayo katika kata ya Buhembe ambako shughuli zote za mazishi zitakuwa zinafanyika huko.
Source: Wasafi FM