Kagera: Padri Elipidius hadi afanyiwe uchunguzi wa ugonjwa wa akili. Ni kuhusu kesi ya mauaji ya Albino Noela Asimwe

Kagera: Padri Elipidius hadi afanyiwe uchunguzi wa ugonjwa wa akili. Ni kuhusu kesi ya mauaji ya Albino Noela Asimwe

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Washitakiwa tisa (9) wanaotuhumiwa kuhusuka na mauaji ya kikatili ya mtoto mwenye ualbino Marehemu Noela Asimwe Novat aliyekuwa na umri wa miaka miwili na nusu mkazi wa kata ya kamachumu ya Wilaya ya Muleba mkoani Kagera wamefikishwa mbele ya jaji wa mahakamani kuu ya Tanzania kwa ajili ya kusomewa shitaka linalowakabili na maelezo ya awali ya kesi hiyo kabla haijaanza kusikilizwa.

Washtakiwa hao wamefikishwa mbele ya jaji wa mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Bukoba Emanuel Ngingwana aliyekubaliana na maombi yaliyowasilishwa na upande wa jopo la mawakili wa utetezi ya mtuhumiwa namba moja padri Elipidius Rwegoshora kutosomewa mashitaka yanayomkabili hadi atakapofanyiwa uchunguzi wa ugonjwa wa akili.

Jopo la mawakili wanne wa upande wa utetezi likiongozwa wakili msomi Projestus Mulokozi awali liliiiomba mahakama isitishe zoezi hilo kwa kuwa mteja wao kwa sasa hana uwezo wa kuongea vizuri pamoja na kuelewa anachokifanya kwa maana hiyo hawezi kujitetea kwa usahihi hivyo wakaomba kupokelewa kwa maombi ya upande wa utetezi

Aidha mawakili wa Jamhuri wakiongozwa na wakili wa Serikali mwandamizi, Waziri Magumbo anayeshirikiana na mawakili wengine wa Serikali ambao ni pamoja na Erick Mabagala na Matilda Assey hawakuweka pingamizi la aina yoyote walikubaliana na uamzi uliotolewa na mahakama wa kusikitisha zoezi.

Jaji Ngigwana aliamua mtuhumiwa apelekwe Isanga akapimwe akili hivyo,alieeleza kuwa watuhumiwa wote watasomewa mashtaka ya kesi inayowakabili kwa pamoja baada ya kupatikana matokeo ya uchunguzi wa ugonjwa wa akili wa mtuhumiwa namba moja padre Elipidius Rwegoshora ambapo kesi hiyo itatajwa tena Desema 11, 2024.

Watuhumiwa wengine ni Novat Venant (24) ambaye ni Baba mzazi wa mtoto Asimwe,Ramadhan Selestine, Nurdin Masoud, Rwenyangira Burukad, Dastan Burchard, Faswiu Athman, Gozibat Arikad na Dezdery Everigist amabo wote wamerudishwa Lumande.

Pia soma: Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji
 
Naona hii mbinu ya kisheria aliyokuja nayo anaenda kuchomoka kwenye hii kesi.. pasipo kujali kwamba ni mwehu kweli ama laaah.
 
achomoke kwa njia gani labda yaani waseme alifanya kosa bila kukusudia?au amepata ukichaa akiwa mahabusu hivyo hawezi kufungwa? huyo ndiyo mzuri anaenda kunyongwa hata maumivu hatasikia si kichaa? kosa walilofanya ni kubwa wasituchezee hawa
 
Naona hii mbinu ya kisheria aliyokuja nayo anaenda kuchomoka kwenye hii kesi.. pasipo kujali kwamba ni mwehu kweli ama laaah.
Eti..Mwehu anaombaje kwenda kuchunguzwa wehu wake?Padri Mpweke..chezea useja wewe.
 
Hili tukio ukilifuatilia kwa undani utagundua huyo Padre kitambo tu alishakuwa na matatizo ya afya ya akili (na hii ni kawaida kwa binadamu yeyote yule).
Na ndiyo maana Paroko wa Parokia husika aliamua kumchukua swahiba wake aliyesoma naye, na kukaa naye Parokiani huku akiwa haruhusiwi kutoa sakramenti ndani ya Kanisa.

Kilichokuja kutokea ndiyo hicho sasa cha kujiwa na ujasiri wa ajabu wa kumshawishi baba yake mtoto kushiriki kufanya hilo tukio la mauaji ya mtoto wake kwa ahadi ambazo mtu mwenye akili timamu na ya kufikiria, asingeweza kuziamini!


Eti kupewa milioni 30 na kununuliwa gari la kifahari la V8!! Na baba wa mtoto naye eti akakubali kumuua mtoto wake kirahisi tu!! Kwa hiyo ni jambo zuri vipimo vikafanyika, ili ukweli ujulikane.
Maana hata kama ataonekana ana changamoto ya afya ya akilii, bado haimpi haki ya kushiriki kuutoa uhai wa binadamu mwingine. Bado sheria itachukua mkondo wake.
 
Kajitoa ufahamu.Kumbe huko makanisani tunapewa communio na watu wasio na akili. Hii ni strategy tu ya kuchomoka adhabu ya kifo ,kifungo cha maisha.
Mkuu umepotea. Wapi? BTW hilo tatizo inawezekana kalipata baada ya kuwekwa gerezani. Mahakama itaangalia kama alikuwa ana akili timamu wakati anafanya kitendo. Nina matumaini makubwa kuwa hatachomoka kwani utetezi wa kutokuwa na akili huwa mgumu sana kwa mashtakiwa kushawishi mahakama. Na hasa ukiangalia simulizi za huu mkasa, inaonekana alikuwa na akili kipindi hicho ila baada ya kuwekwa rumande ndiyo amechanganyikiwa.
 
Kanisa Lina mbinu nyingi za kuwalinda watu wake!

Nadhani hii mbinu ni kijasusi na kimedani sana aiseh!

Ina maana washtakiwa wanaweza kula mvua za kutosha ispokua padre ambaye ni mgonjwa wa akili!!

Hivi yule padri alieshiriki mauaji ya kimbari kule Rwanda 1994 Kwa kuwaonyesha walipojificha watutsi kanisani wale interahamwe alipimwa akili kama zipo sawa!!?

Kanisa takatifu la mitume!
 
Hili tukio ukilifuatilia kwa undani utagundua huyo Padre kitambo tu alishakuwa na matatizo ya afya ya akili (na hii ni kawaida kwa binadamu yeyote yule).
Na ndiyo maana Paroko wa Parokia husika aliamua kumchukua swahiba wake aliyesoma naye, na kukaa naye Parokiani huku akiwa haruhusiwi kutoa sakramenti ndani ya Kanisa.

Kilichokuja kutokea ndiyo hicho sasa cha kujiwa na ujasiri wa ajabu wa kumshawishi baba yake mtoto kushiriki kufanya hilo tukio la mauaji ya mtoto wake kwa ahadi ambazo mtu mwenye akili timamu na ya kufikiria, asingeweza kuziamini!


Eti kupewa milioni 30 na kununuliwa gari la kifahari la V8!! Na baba wa mtoto naye eti akakubali kumuua mtoto wake kirahisi tu!! Kwa hiyo ni jambo zuri vipimo vikafanyika, ili ukweli ujulikane.
Maana hata kama ataonekana ana changamoto ya afya ya akilii, bado haimpi haki ya kushiriki kuutoa uhai wa binadamu mwingine. Bado sheria itachukua mkondo wake.
Ni kweli unenacho.
 
achomoke kwa njia gani labda yaani waseme alifanya kosa bila kukusudia?au amepata ukichaa akiwa mahabusu hivyo hawezi kufungwa? huyo ndiyo mzuri anaenda kunyongwa hata maumivu hatasikia si kichaa? kosa walilofanya ni kubwa wasituchezee hawa
Anyongwe kwa kupanga njama za mauaji? We umesikia wapi
 
Back
Top Bottom