LGE2024 Kagera: RC Mwassa atembea na visheti kuhamasisha Uchaguzi Serikali za Mitaa. Hii ni Rushwa!

LGE2024 Kagera: RC Mwassa atembea na visheti kuhamasisha Uchaguzi Serikali za Mitaa. Hii ni Rushwa!

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Hizi ni rushwa kuwashawishi wananchi wafanye wafanye maamuzi, iwe kwa pesa au visheti vyote ni rushwa. Kwanini vinaachwa kuendelea kufanyika? TAKUKURU mnafanya nini?

===

Screenshot 2024-10-23 075648.png

Mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa amezunguka kwenye baadhi ya vijiwe vya Kahawa katika manispaa ya Bukoba akiwasihi wananchi kushiriki uchaguzi huo.

RC Mwassa katika mizunguko hiyo amebeba visheti alivyovitengeneza mwenyewe na kuwagawia watu kwenye vijiwe vya kahawa ikiwa ni ishara ya upendo huku akifikisha ujumbea wa kushiriki uchaguzi.

Kupata vimbwanga vingine wakati wa Uchaguzi ingia hapa: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Screenshot 2024-10-23 075615.png

Ametumia mwanya huo kuwashukuru wananchi wa Kagera kwa kujitokeza kushiriki zoezi la kujiandikisha na kuwaomba wale wenye sifa kuendelea kujitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali kwakuwa tayari pazia la kuchukua fomu limeshafunguliwa.

Screenshot 2024-10-23 075629.png

Ameongeza kuwa uchaguzi wa mwaka huu atahakikisha unakuwa wa huru na haki huku akiendelea kutoa onyo kali kwa wale wenye nia ya kuleta vurugu kuwa amejipanga kuwakabili.
 
Ubunifu kazini. Safi sana lazima watu wahamasishwe wakapige kura kuchagua viongozi wanaowataka. Sioni shida au uvunjifu wa sheria hapo.
 
Ubunifu kazini. Safi sana lazima watu wahamasishwe wakapige kura kuchagua viongozi wanaowataka. Sioni shida au uvunjifu wa sheria hapo.
Kawachukilia poa sana, visheti wakishakula tu wanatoa kura! Ni watoto nini?
 
CV za ma-RCs , DCs, DACs, RASs etc ziwe ni akiwa publicized wananchi waone.
Kisha ziwe zinatangazwa watu waombe kuwepo na fursa Sawa mwenye sofa zaidi na apate badała ilivyo sasa kwa kujuana .
Asokujua hakuthamini.
 
Wakuu habari zenu!

Huko Kagera Mkuu wa mkoa Hajat Fatma Mwassa amezunguka kwenye baadhi ya vijiwe vya Kahawa katika Manispaa ya Bukoba akiwasihi wananchi kushiriki uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, kama muonavyo kwenye picha.
#Cdigital Serikali za mitaa inawafikia wananchi kwa ukubwa wake, Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. H...jpg
RC Mwassa katika mizunguko hiyo alibeba Visheti alivyovitengeneza mwenyewe na kuwagawia watu kwenye vijiwe vya kahawa ikiwa ni ishara ya upendo huku akifikisha ujumbea wa kushiriki uchaguzi.
#Cdigital Serikali za mitaa inawafikia wananchi kwa ukubwa wake, Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. H...jpg
Ametumia mwanya huo pia kuwashukuru wananchi wa Kagera kwa kujitokeza kushiriki zoezi la kujiandikisha na kuwaomba wale wenye sifa kuendelea kujitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali kwakuwa tayari pazia la kuchukua fomu limeshafunguliwa.

Aidha aliongeza kuwa uchaguzi wa mwaka huu atahakikisha unakuwa wa huru na haki huku akiendelea kutoa onyo kali kwa wale wenye nia ya kuleta vurugu kuwa amejipanga kuwakabili.
 
Back
Top Bottom