A
Anonymous
Guest
Habari za Asubuhi ?
Ninatanguliza shukrani kwa jukwaa hili la fichua UOVU.
Nimewahi kwenda kupata msaada kwenye ofisi ya mtendaji wakata ya Nyaruzumbura , Wilaya Ya kyerwa, Mkoa Kagera, nilichokutana nacho huko kinatisha sana
Rushwa imetawala vyakutosha kuanzia kwa MTENDAJI WA KATA, MTENDAJI WA KIJIJI PIA MWENYEKITI WA KIJIJI, wakikaa kutengeneza suluhu wanatengeneza kwa kutafuta pesa zao mfukoni kana kwamba mtendaji wa Kata hawalipwi na serikali kwa ajili yakuhudumia wananchi
Kule katani wameamua kufanya sehemu ya kufungia watu na kuwapa adhabu za hapa na pale, kiukweli hilo jambo limeniumiza sana.
Ukienda pale lazima utoe kuanzia laki na kuendelea na wanakwambia baada ya suluhu na wao wanahitaji hela ya muda walioutumia pale kwenye suluhu jambo ambalo ukiwapa ile pesa haiandikiwi sehemu, binafsi niligoma kuwapatia kitu wakanitisha watanionesha
Hivyo Niombe Mkuu Wa Wilaya Kyerwa atembelee kuona yanayoendelea kwenye kata ya Nyaruzumbura maana Rushwa imekithiri kuliko sehemu zote nilizopita.
Afisa mtendaji wa kata anatumia madaraka kupiga watu na wakuonea na hana uwezo wa kusuluhisha maana ni mtu anayeegemea pande moja.
Yangu ni hayo.
Ninatanguliza shukrani kwa jukwaa hili la fichua UOVU.
Nimewahi kwenda kupata msaada kwenye ofisi ya mtendaji wakata ya Nyaruzumbura , Wilaya Ya kyerwa, Mkoa Kagera, nilichokutana nacho huko kinatisha sana
Rushwa imetawala vyakutosha kuanzia kwa MTENDAJI WA KATA, MTENDAJI WA KIJIJI PIA MWENYEKITI WA KIJIJI, wakikaa kutengeneza suluhu wanatengeneza kwa kutafuta pesa zao mfukoni kana kwamba mtendaji wa Kata hawalipwi na serikali kwa ajili yakuhudumia wananchi
Kule katani wameamua kufanya sehemu ya kufungia watu na kuwapa adhabu za hapa na pale, kiukweli hilo jambo limeniumiza sana.
Ukienda pale lazima utoe kuanzia laki na kuendelea na wanakwambia baada ya suluhu na wao wanahitaji hela ya muda walioutumia pale kwenye suluhu jambo ambalo ukiwapa ile pesa haiandikiwi sehemu, binafsi niligoma kuwapatia kitu wakanitisha watanionesha
Hivyo Niombe Mkuu Wa Wilaya Kyerwa atembelee kuona yanayoendelea kwenye kata ya Nyaruzumbura maana Rushwa imekithiri kuliko sehemu zote nilizopita.
Afisa mtendaji wa kata anatumia madaraka kupiga watu na wakuonea na hana uwezo wa kusuluhisha maana ni mtu anayeegemea pande moja.
Yangu ni hayo.